Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, April 30, 2013

HIZI HAPA NAFASI MPYA ZA KAZI KWA WATANZANIA...!

JOB ANNOUNCEMENT (CONTRACT)
Job Title: Coffee Liquorer (2 post)
Reports To: Chief Liquorer
Employment status: Contract Job
Duration: Six months (Renewable)
Duties and responsibility
Participate in coffee roasting outturns and pre-auction cupping preparations.
Safe keep and update liquoring files of catalogues.
Writing bulking instruction and dispatch to factories.
Conduct pre-auction inspections and draws auction samples from curing factories.
Participate in liquoring and classification of coffee from factories.
Carries out coffee roasting outturns and pre-auction cupping preparations.
Participate in safe keep and update liquoring files of catalogues.
Writes bulking and classification reports.
Performs any other duties as may be assigned by Supervisor
Qualification
Holder of Bachelor Degree/Advanced Diploma in Agro Business, Food Science, Nutrition, Business
Administration or its equivalent from a recognized University/Institution with at least three (3) years
working experience in the same field from a reputable organization


MODE OF APPLICATION
Applicants have to attach current Curriculum Vitae (CV) which includes names, addresses, reliable
telephone numbers and email addresses of academic and work related references.
Applicants should indicate three reputable referees with their reliable contacts.
Testimonials, transcripts and results slips will not be accepted
Deadline for application is 10th JUNE, 2013 at 3.30 pm
Applications hard copy letters in English to be delivered to the following address:-
The Director General
Tanzania Coffee Board,
P. O. Box 732
MOSHI
Soft copy application letter plus scanned CV sent at info@coffeeboard.or.tz
Tanzania Coffee Board is an equal opportunity employer, females are encouraged to apply.
TANZANIA COFFEE BOARD
P.O. BOX 732, MOSHI TANZANIA
Tel (027)27 52324
Fax (027)27 52026
E-mail: info@coffeeboard.or.tz
Web: www.coffeeboard.or.tz
Telegrams
COBOT MOSHI
JOB ANNOUNCEMENT (CONTRACT)
Job Title: Sales and Promotion Officer (1 post)
Reports To: Principal Internal Promotion Officer
Employment status: Contract Job
Duration: Six months (Renewable)
Duties and responsibility
Develop work plan and budget for local coffee promotion.
Responsible for sale and distribution of the Tancafe Brand.
Develop programme for expansion of coffee consumption locally through different outlets such as
supermarkets, tourist hotels, colleges, government offices, etc.
Develop work plan and budget for establishment of coffee roasting unit (CRU) Coffee Bar/Shop.
To Monitor and compile report for total internal coffee consumption in the country.
Performs any other duties as may be assigned by Supervisor
Qualification
Holder of Bachelor Degree/Advanced Diploma in Business Administration (Sales or Marketing) or its
equivalent from a recognized University/Institution with at least three (3) years working experience in the
same field from a reputable organization
MODE OF APPLICATION
Applicants have to attach current Curriculum Vitae (CV) which includes names, addresses, reliable
telephone numbers and email addresses of academic and work related references.
Applicants should indicate three reputable referees with their reliable contacts.
Testimonials, transcripts and results slips will not be accepted
Deadline for application is 10th JUNE, 2013 at 3.30 pm
Applications hard copy letters in English to be delivered to the following address:-
The Director General
Tanzania Coffee Board,
P. O. Box 732
MOSHI
Soft copy application letter plus scanned CV sent at info@coffeeboard.or.tz
Tanzania Coffee Board is an equal opportunity employer, females are encouraged to apply.
TANZANIA COFFEE BOARD
P.O. BOX 732, MOSHI TANZANIA
Tel (027)27 52324
Fax (027)27 52026
E-mail: info@coffeeboard.or.tz
Web: www.coffeeboard.or.tz
Telegrams
COBOT MOSHI


JOB ANNOUNCEMENT (CONTRACT)
Job Title: Internal Auditor (1 post)
Reports To: Chief internal Auditor
Employment status: Contract Job
Duration: Six months
Duties and Responsibilities:
- Reviewing internal controls and submitting recommendations to superiors.
- Executing audit programmes.
- Ensuring that internal control systems are adequate to avert perpetration of frauds,
misappropriation and embezzlements.
- Preparing audit reports based on the audit findings.
- Reviewing the effectiveness of managerial controls and implementation of systems, policies
and practices for the Institute.
- Preparing internal audit programmes in accordance with generally accepted audit standards
and international audit standards.
- Providing technical guidance and assistance to subordinates.
- Leading and direct in special checks and investigations.
- Monitoring audit work in order to ensure that works schedule are executed efficiently.
- Preparing progress reports of special audits carried out.
- Performing any other duties as assigned by his/her superior.
Qualification
Holder of Bachelor Degree or Advanced Diploma in Accountancy, B.com (Accounting) or its
equivalent from a recognized Institution with at least (3) years relevant working experience from a
reputable organization


MODE OF APPLICATION
Applicants have to attach current Curriculum Vitae (CV) which includes names, addresses, reliable
telephone numbers and email addresses of academic and work related references.
Applicants should indicate three reputable referees with their reliable contacts.
Testimonials, transcripts and results slips will not be accepted
Deadline for application is 10th JUNE, 2013 at 3.30 pm
Applications hard copy letters in English to be delivered to the following address:-

TANZANIA COFFEE BOARD
P.O. BOX 732, MOSHI TANZANIA
Tel (027)27 52324
Fax (027)27 52026
E-mail: info@coffeeboard.or.tz
Web: www.coffeeboard.or.tz
Telegrams
COBOT MOSHI
The Director General
Tanzania Coffee Board,
P. O. Box 732
MOSHI
Soft copy application letter plus scanned CV sent at info@coffeeboard.or.tz
Tanzania Coffee Board is an equal opportunity employer, females are encouraged to apply.

Sunday, April 28, 2013

KAMPUNI YA MARENGA INVESTMENT YAWEZESHA MAANDALIZI YA SIKU YA WAANDISHI WA HABARI DUNIANI...!

Kikosi cha timu ya Marenga investment.

 Timu ya Marenga inverstment na Waandishi wa habari zikiwa tayari kwa ukaguzi kabla ya kuanza kwa mechi

 IKIWA Kesho  waandishi wa Habari kote Duniani wanaadhimisha siku yao, ndani ya Mkoa Kilimanjaro waandishi wa habari wamesheherekea  Maandalizi ya siku hii kwa bonanza kubwa ambalo limedhaminiwa na Kampuni ya Marenga investment. Bonanza hilo lilizikutanisha timu ya mpira wa pete ya wanawake ya waandishi wa habari dhidi ya Timu ya Wafanyakazi wa Marenga Investanisha Timu ya mpira wa pete ya wanawake ya waandishi wa habari dhidi ya Timu ya Wafanyakazi wa Marenga Investment wakati  katika  Matokeo ya mchezo huo wa awali uliochezwa mnamo wa saa  saa nane kamili na matokeo ikawa ni timu ya waandishi wa habari walishinda kwa vikapu na 35 Marenga vikapu 12.
Baada ya mchezo huo ulifuatiia mchezo wa mpira wa miguuuu ambapo timu ya wafanyakazi wa Marenga walichuana na timu ya wafanyakazi wa Marenga investment walichuana na timu ya waandishi wa habari waliibuka kidedea kwa ushindi wa bao 5 - 3 dhidi ya Marenga investment. Hataa hivyo mgeni rasmi alikua ni Katibu wa chama cha soka Kilimanjaro ndugu  Mohamedy Mussa Alisema Alisema huu ni wakati wa Wafanyabiashara na wadau wa michezo kujitoa katika michezo na kufufua michezo ndani ya mkoa Kilimanjaro huku akitoa pongezi za dhati kwa Kampuni ya Marenga Investment iliyopo Kiboriloni mjini  Moshi kwa kudhamini  Bonanza hilo.

Kocha wa Timu ya  Marenga investmentakiwa na Maginga mwenye jezi ya blue wakitoa maelezo kwa timu ya wanawake kabla ya kipindi cha pili.

Timu ya wanawake waandishi wa habari ikiwa tayari kabla ya mechi.

Saturday, April 27, 2013

MUANDISHI AMERUDI....,





                                                  NYEMO CHILONGANI

Katika Maisha kila mtu anaweza, Fikra za kuwa upo peke yeke kwa kile anachokifanya pasipo kujua kuwa kuna watu wenye uwezo kama yeye na zaidi ya yeye katika kufanya jambo analofanya tatizo ni hajapata fursa ile uliyo nayo. Katika zunguka zunguka yangu jijini Dar es Salaam. Hapo ndipo nikajikuta nimetokea Tandale. 
Vijana waliokaa chini ya nuzo ya umeme ambayo juu yake wametundika bendera yenye jina la Kempu ya vijana wa eneo lile huku wakiwa kimya kumsikiliza kijana mmoja aliyeonekana ni muongeaji sana. Nilijisogeza na kutaka kusikiliza kama naweza pata chochote cha kuandika kulingana na kazi yangu. Nilijikuta nikivutiwa na hadithi alizokua anapiga yule kijana, Uhalisi wa hadithi ulinifanya kutaka kumjua zaidi. Baada ya kumaliza kisa kimoja cha Mwanamke wa ndoto nilijikuta nikimpa mkono na kumuomba tuongee pembeni.
"Naitwa Qassim Mwinyi niMuandishi wa habari sijui wewe unaitwa nani?"
"Naitwa Nyemo Chilongani"
Alijibu kwa uchangamfu nikagundua kitu kingine kwa kijana huyu ni jasiri na mwenye kujiamini sana.
"Ile hadithi umeitoa wapi?
"Ah natungaga mwenyewe"
"Eh kwani una hadithi ngapimpaka sasa"
"Nina hadithi zaidi ya Elfu mbilinimeziweka tu nyumbani"
"Dah ningependa kusoma moja ya hadithi zako"
"Ok usijali kwa kuwa wewe ni Muandishi nitakupa hadithi moja inaitwa Muandishi Amerudi"
"Kwanini umechagua kunipa hadithi hiyo niisome"
"We nenda kasome kisha ukiweza wape wasomaji wako wasome"
Alinipahadithi ikiwa katika cdnilienda nyumbani sikutaka kupumzika nikafungua kompyuta mpakato na kufungua hadithi ile.  Nilianza kusoma kwa shauku mpaka naimaliza nilijikuta nikilia zaidi ya mara nne. Nimeona nisiisome mwenyewe Anzia kesho hadithi hii itawajia Hapa.

HAYA NDIO MAHAFALI YA SABA YA CHUO CHA GREEN BIRD WILAYANI MWANGA...!

 
Wahitimu wa chuo cha Green Bird wakiingia ukumbini.


Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya Green Bird Education ndugu Juma H. Mndeme akitoa neno la shukrani.


Wanafunzi waliohitimu katika chuo cha Green Bird wakikabidhiwa vyeti.

LEO tarehe 27 April 2013 ni siku ya mahafali ya saba ya wahitimu wa kozi ya ualimu na kozi ya Biashara katika chuo cha Green Bird kilichopo wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro. Chuo cha Green Bird ni chuo kilicho ndani ya taasisi ya Green Bird ambayo inajumuisha shule ya bweni ya Green Bird Girls na Green Bird Boys ambayo inatoa elimu ya kidato cha kwanza mpaka kidato cha sita, pia ndani ya taasisi hii hii kunatolewa elimu ya awali ya kindergarten na elimu ya msingi. Katika chuo cha ualimu cha Green Bird kunatolewa kozi ya ualimu kwa daraja la cheti na diploma na pia kuna kozi ya biashara. Leo katika mahafali ya Wahitimu wa Kozi ya Ualimu na Biashara kulikuwa na wageni mbalimbali na Mgeni Rasmi alikua ni Afisa elimu wa Wilaya ya Mwanga Ndugu Mwenda.

Katika hotuba ya mgeni rasmi  ambaye ni afisa elimu wilaya ya Mwanga amewaomba wahitimu baada ya kufanya mitihani wafikirie kuomba vituo vya kazi katika wilaya ya Mwanga kwani wilaya ya Mwanga inawahitaji sana na pia ametoa shukrani kwa taasisi ya elimu ya Green Bird pamoja na Kalua Development Trust Fund kwa kuweza kushirikiana na jamii ya wilaya ya Mwanga kuhakikisha elimu inayotolewa na taasisi ya Elimu ya Green Bird inawanufaisha watu wa wilaya ya Mwanga pia alitumia fursa hiyo kuwaasa wazazi kuwapa watoto wao elimu huku akimwaga sifa kwa Green Bird kwa kiwango chao cha ada hasa kwa ngazi ya chuo ambacho ni kiwango cha chini kuliko vyuo vyote vya watu binafsi. Na elimu wanayotoa ni zaidi ya vyuo vingine.
 
Hata hivyo Mwenyekiti wa Kalua Development Trust Fund Mama Mndeme alitumia fursa hii kuwaasa wahitimu wakawe mifano bora huko wanakwenda na elimu waliyopata ikawe manufaa kwa taifa. Pia mkuu wa chuo cha ualimu Green Bird Madame Saumu Khalifa katika hotuba yake ameeleza maendeleo ya chuo hicho pamoja na mipango ya baadae ikiwa lengo la chuo ni kuhakikisha kinakua chuo kikuu baada ya mwaka mmoja.

Huyu ndio aliyekua mshereheshaji wa maafali ya Green Bird anaefahamika kwa jina la Casim Mwinyi.(Babi)

HUYU NDIO PRODUCER WA SauzWest Productions KATIKA HARAKATI ZA KUKUZA MUZIKI...!

Upande wa kulia ni MarkDen  akiwa na wasanii wa mkoani Kilimanjaro


MarkDen akifanya kazi katika studio ya SauzWest Productions

             MUZIKI wa Tanzania umezidi kufanya vizuri siku hadi siku na kuwapatia vijana wengi sana ajira ikiwepo kuwapa mafanikio makubwa kama kumiliki nyumba za kifahari na kuendesha magari mazuri na ya gharama. Lakini chakushangaza ni kwamba kwa mkoa wa Kilimanjaro imekua kama ni balaa kwa kuwa ndio mkoa mkongwe kwa upande wa kaskazini ambao haujapata mafanikio katika mziki wa kizazi kipya ukifananisha na mkoa kama Tanga na Arusha. Nilifanya juhudi za kuweza kumtafuta mmoja kati ya maproder ambao ni mkongwe sana kwenye fani ya kuandaa muziki. Nadhani wakazi wengi wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro mtakua mnamfamu.

Jamaa huyo anaitwa  Mark Denning maarufu kama MarkDen anaishi Mabruda Street, Soweto Moshi na Najihusisha na Utayarishaji wa Muziki katika Studio za SauzWest Production. Na ana miaka kumi (10) kwenye utayarishaji wa muziki alianza kujifunza kutengeneza ala za muziki mwaka 2003 alipokua anasoma Chuo cha JRIIT (Aptech) na kuanza kazi studio ya Kwanza inayoitwa Nad Records mwaka 2007 hadi 2009 aliendelea kupractice bila kuwa na studio hadi alipofungua studio yake mwenyewe July 2012 inayofahamika kwa jina la SauzWest Productions.
 
Baada ya kufahamu hayo machache pia nilimuuliza ni vikwazo gani unavyokutana navyo kwenye kazi zako? "Vikwazo ni vingi kama unavyojua Mkoa wetu kwa tasnia hii ya burudani bado haijakua kwa kiwango kinachohitajika kwa hiyo kusikiza mbali inakua ngumu ila sasaivi naona wasanii baadhi wameamua kuwa serious na kazi zao kwa hiyo itafanya muziki wa Kilimanjaro upande kidogo, kikwazo kingine ni kipato kwani kama kipato kingekua kizuri tungekua tumeshafika mbali kwa kufanya kazi nzuri na kuzifanyia promosheni ya kutosha, Kikwazo kingine ni Tanesco ambao wamekua wakivuruga program za studio Pale huduma yao inapokuwa haipo na kuna ratiba studio Kwa kweli vikwazo vipo ila nimejipanga kupambana navyo." Alijibu MarkDen
 
Nilitaka watu wafahamu kwamba ni nyimbo gani ambayo umeitengeneza ambayo unahisi kama ndio imekufanya ukapata heshima kubwa sana kwenye shuhuli yako ya kuandaa muziki? "Nimefanya kazi nyingi nzuri…siwezi kusema moja ila kuna kazi kama Tupo Maficho niliifanya mwaka 2008 ndani ya Nad Records iliweza kunipaheshima kwenye media za huku kaskazini hasa A Town ila kwa sasa kuna kazi nimezitoa zinakubalika sana kwenye Radio za Moshi na bado tunaendelea kuzisambaza inaitwa Moshi_The Revolution Army pamoja na Shinikizo la Mawazo ambazo zote zimetoka SauzWest production na pamoja na kazi ya kutengeneza SOUNDTRACK ya Documentary ya KAULI NGO wa Marekani kwa hiyo kazi nyingi zipo nab bado tunajaribu kuangalia ipi ni Bora tuirelease." Alijibu MarkDen

Unadhani kati ya producer na msanii ni yupi anatakiwa kuheshimika endapo nyimbo itafanya vizuri? "Nadhani Producer ndio inabidi aheshimike japokua pia msanii nilazima nae apewe sifa zake kama amefanya kazi nzuri ila umaliziaji na utundu na akili ya Producer katika Mixing na Mastering ndio vinabidi kuheshimika zaidi kwa hiyo Producers inabidi waheshimike zaidi japokuwa nyimbo ikifanya vizuri msanii huwa ndio anafaidika zaidi." Alijibu MarkDen

Hapa mkoa wa Kilimanjaro unahisi kama wasanii, producers na watangazaji au maDJs mnaushirikiano mzuri kwenye kufanikisha harakati za muziki? 
"Swali Zuri kwa kweli kuna ushirikiano kidogo sana baina ya hao watu Umewataja inahitajika kuanzisha ushirikiano endelevu na wenye nia moja ya kupandisha muziki wetu juu na hii bila ushirikiano wa kutosha baina yetu inakua ni vigumu sana kufanikiwa….Hii ikiwa sawa basi harakati zetu zitaeleweka zaidi." Alijibu MarkDen

Unadhani nini kifanyike ili kuweza kuleta mafanikio ya muziki katika mkoa wa Kilimanjaro?

"Nadhani hii inaanzia kwa msanii ndio inaendelea kwamba wasanii wa Kilimanjaro
wajitahidi kuwa serious na kazi hii.Msanii akishakuwa vizuri inaelekea studio kwa producers kufanya kazi zenye viwango na baadae managers wawaandalie wasanii wao Video nzuri na baadae madj na watangazaji wa redio za nyumbani Kilimanjaro kuwasaidia wasanii nyimbo zao kusikika na kupata air time ya kutosha ndipo mapromoters wenye nia njema wajitokeze nakutengeneza matamasha ili kila mtu afaidi huu mziki wetu uliojificha. " Alijibu MarkDen

Wewe kama producer ni juhudi gani binafsi ambazo unazifanya kufanikisha mziki hususani wa wasanii wanaotokea Kilimanjaro? 
"Najitahidi sana kuwaelekeza wasanii ambao bado hawajatoka jinsi ya kujipanga kufanya kazi nzuri na pia kuwasadia wasanii kwa kuwatoza fedha kidogo ambayo inawezesha tu uendeshaji na ufanyaji wa kazi yake.Kwa sasa narekodi kwa kiasi kidogo sana cha fesha." Alijibu MarkDen

Wewe ni producer na pia unaimba, Kuna lawama kwamba nyie maproducers ambao mnaimba na mna studio huku mikoani huwa mnawarekodia wasanii wachanga kwenye studio zenu alafu nyie mnaenda kwenye studio kubwa zilizopo dar es salaam na kurekodi ngoma kwenye production nzuri? 
"Mimi pia ni msanii na nilianza kwanza kuwa msanii miaka ya 1998 na nikiwa na marehemu BT Boy na kundi letu la Dark Gz ila mnamo mwaka 2006 nilianzisha kundi la wasanii waimbaji na wanaorap ambao pia kwenye kundi hilo kuna maproducers wanne, Kundi la The Revolution Army linaloundwa na Mimi Mwenyewe MarkDen pamoja na
· Madi LegendinTown (Rapper/Writer)
· ST/STIM/Mfupa (Rapper/Writer)
· Sige Art (Paint artist/Rapper/Singer/Writer/Producer)
· Matata Deo (Singer/Rapper/Producer/Writer)
· Chie Nassa (Rapper/Singer/Writer/Producer)
· Nacz (Rapper/Writer/ )
Kwahiyo baada kuanza kuimba na kurap ndio nilipo anza kutayarisha muziki na tokea nimekua na studio sijawahi kurekodia Dar mara ya mwisho ilikua mwanzoni mwa mwaka 2007 niliporekodi track yangu pale Aiges Records nikimshirikisha Ngwea na Mez B kwa hiyo sio tabia yangu labda kwa maproducers wengine."
Alijibu MarkDen

Mtu akitaka kukupata kufanya kazi na wewe anaweza kukupaje? 
"Unaweza kunitafuta kwenye namba yangu ya mkononi ambayo ni 0717935546 ama ukaniandikia email kwenda mcdenning@gmail.com ama aje studio iliyopo Mabruda Street karibu na Makanyaga Pub Soweto Moshi.Pia unaweza kunipata facebook kwa Username Mark Denning na page la label ya studio kwenye https://www.facebook.com/SauzWestProduction na pia unaweza kusikiliza nyimbo nilizotayarisha kwa kupitia http://www.reverbnation.com/markden pamoja na http://www.hulkshare.com/SauzWest_Product na pia twitter kwa account ya #sauzwestproduct" Alijibu MarkDen


logo ya SauzWest Productions

Friday, April 26, 2013

HAYA NDIO MAKOSA YALIYOMKOSESHA MBUNGE WA ARUSHA MJINI GODBLESS LEMA DHAMANA...!

Mh. Godbless Lema Mbunge wa Arusha Mjini kulia akiwa na vyombo vya sheria.

Hakika sikutaka kukurupuka kuposti kitu chochote leo kuhusu kadhia hii… kwanza sikuamini kama Jeshi letu pamoja na Mkuu wangu wa mkoa wa Arusha alikuwa na kesi ya kumfikisha Mbunge Kipenzi cha wana Arusha maakamani.

Lakini kubwa zaidi nilijuwa busara za Mkuu wetu huyo ambaye ni mtoto wa aliyekuwa msaidizi wa Katibu mkuu wizara ya utumishi (mama yake) japo angalikuwa na busara hata chembe kama mama yake, nakili wazi uwezo wake niliubeba zaidi ya uwasilia wake ulivyo.

Naomba niwasilishe kwanza mashtaka ya Kamanda mpambanaji G. Lema nikirudi nitajadili na kuwaletea maojiano ya mkuu wetu wa mkoa alivyo zungumza na Radi 5 leo pamoja na Video ambazo polisi walilazimika kufanya upekuzi wa masaa kadha kuzitafuta nyumbani kwa Lema.

Kwa mujibu wa wakili wa mbuge wa Arusha Mwanasheria Humphrey Mtui makosa aliyoshitakiwa nayo Lema ni haya:-



1. Kosa la kwanza ni kuwaambia wanafunzi wa chuo cha uhasibu alipoenda kuwatuliza kuwa ‘dhambi kubwa kuliko zote ni woga ‘.Haki hutafutwa na kupiganiwa ikiwa jambo unalipigania ni la msingi na linafaa kupiganiwa (Worth fighting for). {HAPO KOSA NI UCHOCHEZI}

2. Kosa la pili ni pale alipotamka kuwa ‘’Tumemtafuta mkuu wa mkoa juu ya Matatizo yenu na mlivyoshuhudia hapa amechukua muda mrefu na kuingia kama vile anaingia kwenye send-off. Hawa ndiyo viongozi wetu ambao hawajali matatizo ya wananchi’’ {HAPO KOSA NI UCHOCHEZI}

3. Kosa la Tatu ni pale alipotamka kuwaambia wanafunzi kuwa ‘’Mimi Mbunge wenu nipo sambamba nanyi hadi mpate haki yenu na ikiwa mkuu wa mkoa hatakuja hapa kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa mkoa nitawaongoza hadi ofisini kwake ili mpate majibu na haki yenu kwani ni haki yenu ya msingi kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ambayo niliapa kuilinda Bungeni na pia inaruhusiwa kwa mujibu wa kikanuni na kifalsafa katika utekelezaji wa utawala bora wa kidemokrasia ambao msingi wake ni kusikilizwa na kulinda haki za binadamu’’ {HAPO KOSA NI UCHOCHEZI}

Hayo ndiyo makosa mabayo yamemyima Mh. Lema  dhamana. hayo ndiyo makosa yaliyosababisha polisi watumie fedha za walipa kodi kumvamia usiku kurusha fataki badala ya kutumia busara ya kumuita tu kituoni na kusababisha taharuki maeneo hayo na ndani ya nyumba yenye ndugu jamaa na hata mtoto mwenye miezi mitano huku polisi wakitumia nguvu na kukiuka sheria

Huo umeitwa uchochezi baada ya mkuu wa mkoa kumtumia ujumbe wa mkononi kupitia simu yake kupitia namba 0752960276 aliyotishia kumbambikizia kesi anayoitaka yeye.

KAULI YA ZITTO KABWE BAADA GODBLESS LEMA KUKAMATWA NA POLISI ...!


BREAKING NEWS: Mbunge wa Arusha Mjini kupitia chama cha Demokrasia ma Maendeleo (CHADEMA) Ndugu "Godbless Lema" usiku wa jana kuamkia leo saa8 amefikishwa Central Police bila kufahamika chanzo...
 Hii inatupa wasiwasi na kubaini kua kuna mchezo nyuma ya pazia unaochezwa na kundi la watu wa chache katika siasa upande wa pili wa upinzani kibaya zaidi ni ma'askari waliovamilia nyumbani kwa mbunge usiku wa jana na kulipua mabomu na wakiwa na silaha kali utadhani wamekwenda kumkamata jambazi au mtu mwenye kesi ya mauaji kitu ambacho sio kizuri. 
#Pole kwa familia ya Godbless Lema.

PICHA NA MAELEZO YA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA MUUNGANO UWANJA WA UHURU JIJINI DAR ...!

1
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama lililoandaliwa maalum kwa ajili maadhimisho ya miaka 49 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika kwenye uwanja wa Uhuru leo jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyama vya Siasa na Mabalozi pamoja na wageni waalikwa mbalimbali ili kushuhudia maadhimisho hayo.(PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-UWANJA WA UHURU)

4
Rais Wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kulia akiwa na viongozi wengine katika jukwaa kuu kutoka kushoto ni Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Idd, Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

7
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya Kikwete akiingia uwanjani katika gari maalum huku akisindikizwa na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange.


Vikosi vilivyo pita na kutoa heshima mbele, kikosi cha Ulinzi JWTZ, kikosi cha  Jeshi la Ulinzi JWTZ, Kikosi cha Jeshi la Kujenga taifa JKT na Kikosi Maalum Cha Bendera kikitoa heshima zake bele ya Rais Jakaya Kikwete.

17
Watoto wa halaiki wakionyesha ujumbe mbalimbali kuhusu Muungano wetu mbele ya Rais Jakaya Kikwete na maelfu ya Watanzania waliohudhuria katika maadhimisho hayo.

MZEE WA MIAKA 49 AMLAWITI MWANAFUNZI WA DARASA LA TANO MWENYE ULEMAVU WA AKILI...!

MKAZI mmoja wa Kitasha Mengeni wilayani Rombo aliyefahamika kwa jina la Balthazar Pankras Swai mwenye umri wa miaka 49 anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wa darasa la tano mwenye ulemavu wa akili. Na taarifa kutoka katika jeshi la polisi zinadhibitisha kutokea kwa tukio hilo usiku wa kuamkia tarehe  25 Aprili 2013 katika kijiji cha Aleni Chini.

Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro limesema kitendo hicho cha kikatili alichofanyiwa
mwanafunzi huyo wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Mengeni wilayani Rombo, kimemsababishia mtoto huyo maumivi makali katika sehemu zake siri. Mbinu iliyotumika kumkamata mzee huyo ni polisi wakishirikiana na polisi jamii wa kijiji hicho kwa usimamizi wa Mwenyekiti Correntini Masawe.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mtuhumiwa pia ni mhalifu sugu kwani alishawahi kufungwa gerezani miaka ya nyuma kutokana na matukio ya kihalifu  huku wakilaani kitendo alichokifanya mtuhumiwa na kuvitaka vyombo vya dola kuchukua mkondo wake.

ALICHOKIANDIKA LEMA AKIELEZEA UKWELI WA TUKIO ZIMA KUHUSU FUJO ZILIZOTOKEA CHUONI ARUSHA...!

 
Mbunge Wa Arusha Mjini Godbless Lema Akiwatuliza Wanafunzi Wa Chuo Cha Uhasibu Arusha
 
Majira ya saa nne asubuhi 24/04/2013 nilipokea taarifa kutoka Chuo cha Uhasibu juu ya tukio la mauaji ya mwanafunzi yaliyotokea jana usiku kwa kuchomwa kisu eneo karibu na chuo , nilipita Chuoni hapo baada ya kusikia taarifa hiyo , nilikuta
Wanafunzi wengi sana wakiwa wamekusanyika pamoja wakiwa na jazba huku Kamanda wa Jeshi la Polisi Wilaya akijaribu kuwasihi watulie wakati walipokuwa wanatafuta muafaka wa kuzuia jazba ambayo ilikuwa ina lengo la kuandamana kwenda kwa Mkuu wa Mkoa.

Nilipata faragha ya kuongea na Mwalimu aliyekuwa pale ( Dean of Student ) pamoja na OCD na wote walinieleza tatizo lilivyoanza na kuomba nitumie busara kuzuia jazba na maandamano hayo yaliyokuwa yamepangwa kuelekea kwa Mkuu wa Mkoa niliongea na wanafunzi na niliwasihi watulie na nilifanya jitihada za kumtafuta Mkuu wa Wilaya na Mkuu wa Mkoa na kwa bahati nzuri nilimpata Mkuu wa Mkoa na kumweleza juu ya kifo hicho na kile ambacho wanafunzi wanakusudia kufanya kuandamana kwenda ofisini kwake. Nilimuomba afike ili aweze kutuliza hali hile na pia atoe kauli juu ya tukio hilo baya la kuhuzunisha kwani ikizingatiwa kuwa ni zaidi ya mara moja matendo kama haya yamekuwa yakitokea na hakuna hatua zozote zimekuwa zikichukuliwa kuwahakikishia Wanafunzi Usalama wao na mali zao.

Mkuu wa Mkoa pamoja na mimi kumpa taarifa mapema aliahidi kufika mapema jambo ambalo halikufanyika na wanafunzi walianza kuwa wakali na nilifanya jitihada na hekima za hali ya juu kuvuta subira za wanafunzi hao ili Mkuu wa Mkoa afike . Baada ya Mkuu wa Mkoa kufika Makamu wa Chuo aliniomba niwaandae wanafunzi kumsikiliza Mkuu wa Mkoa na yeye alikwenda kumchukua Mkuu wa Mkoa na kumpa mukutasari wa tukio zima na hali halisi ya kilichokuwa kinaendelea na kimsingi Mkuu wa Mkoa alipofika Wanafunzi walitaka apande juu kuongea mahali ambako tulitumia kama jukwaa kwa maongezi wakati wote lakini badala yake mambo yafuatayo yalianza kutokea 

1) Mkuu wa Mkoa alikataa na kunitaka nishuke chini mahali alipokuwa yeye na timu yake ya ulinzi na usalama Mkoa kwa kweli nilitii na nilipotaka kuongea nae alinidharau na kuniambia hawezi kuongea na wanafunzi wahuni wasiokuwa na nidhamu maneno ambayo yaliwatia wanafunzi hasira zaidi na nilimsihi na kumuomba Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa (RSO) kumshawishi Mkuu wa Mkoa kukubali kuongea nao kwani hali ilivyokuwa ni dhahiri kwamba wanafunzi wale walikuwa na jazba ya hali ya juu na hivyo hekima na unyenyekevu ndio ilikuwa njia pekee ya kutuliza hali hile. 

2) Mkuu wa Mkoa alitoa masharti kwamba asingeweza kuongea nao bila kipaza sauti na wanafunzi wote waende jengo lililokuwa karibu na Utawala na wakisha kaa atakuja kuongea nao jambo ambalo wanafunzi waligoma kwa imani kwamba jengo hilo lisengeweza kuchukua wanafunzi wengi na mimi niliaga naondoka kwenda msibani na wanafunzi waligoma nisiondoke mpaka watakapo sikilizwa na kwa kweli nilitii maombi baada ya kunizuia na kukaa mbele ya gari yangu.

3) Tulipokwenda eneo la kukutania na mara hii ilikuwa ni nje jirani ya jengo la utawala wanafunzi walikusanyika wakimsubiri Mkuu wa Mkoa na kabla hajafika nilitwa na yeye mwenyewe ili tuweke msimamo wa pamoja kama viongozi lakini badala yake alitumia Polisi kunitisha na kuhaidi kuwa nitamtambua kuwa yeye ni Serikali ,tulitofautiana tena nilipokataa hofu hiyo na ghafla tuliamua kwenda eneo la kuongea na wanafunzi na ndipo yafuatyo yalitokea “

Mkuu wa Mkoa wakati anaanza kuongea alianza kusema maneno yafuatayo “ Mnaona hiki Kifua na huu mwili wangu , na hapo ndipo hali ilipochafuka na kuamsha vurugu kubwa kutoka kwa Wanafunzi waliokerwa na kauli yake na Polisi wa walimchukua na tafrani kati ya Polisi na Wanafunzi ikapamba moto hali iliyosababisha mabomu ya machozi kulipuliwa kwa wingi kila kona ya chuo na kila mtu kuanza kukimbia kuangalia usalama wake nikiwemo mimi .
Nimesikiliza Mkutano wake na Waandishi wa Habari na leo nimesoma nakusikiliza vyombo mbali mbali vya habari kwamba ninatafutwa na Polisi kwa amri ya Mkuu wa Mkoa , nimeshangaa sana japo sio kumshangaa Mkuu huyu wa Mkoa kwani ufahamu na uwezo wake naujua ulivyo katika kufikiri na kutatua mambo ya msingi na muhimu , kwa jinsi nilivyomsikia na kumuona alivyokuwa anashughulikia tatizo lile lililotukutanisha jana pale Chuoni , kwa kweli nilishangazwa sana na kuogopa kama hekima ya Mkiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa angeweza kushughulikia tatizo lile kwa namna ile ya Kiburi , Dharau na Majivuno ambayo hakika ilikuwa ni chanzo cha wanafunzi kukataa kumsikiliza na ndipo alipoamua kuondoka huku zomea zomea ikiendelea kushamiri vizuri . Mabomu yalianza kupigwa , wanafunzi walipigwa na kunyang’anywa pesa , simu , na lap top na vitu mbali mbali ambavyo Polisi walikuwa wanaona vina thamani kwao , nilikuwa ninatazama mambo haya huku roho yangu ikiwa inauma sana kwamba wanaopaswa kulinda usalama wa raia na mali zao ghafla waligeuka kuwa vibaka wa kuumiza raia na kupora mali zao .

Ninawapa pole wanafunzi kwa msiba wa rafiki yao na siku ya jana ilikuwa ni siku ya Serikali kutumia busara kurudisha matumaini kwa wanafunzi wale pamoja na raia , lakini badala yake wafiwa walipotaka kudai haki zao za kulindwa , walipigwa , walidhalilishwa na Chuo chao kufungwa bila sababu ya msingi wala kuzingatia mambo muhimu .

Ifahamike kuwa Chuo cha Uhasibu Arusha kina wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali za nchi hii, na amri ya mkuu wa mkoa kufunga chuo na kuamuru wanafunzi watawanyike ifikapo saa kumi na mbili jioni , huu ni ukosefu wa upendo , hekima , busara na utu ikizingatiwa kuwa sababu na mchochezi wa vurugu hizi ni Mkuu wa Mkoa kukosa maarifa na hekima.

Nimepokea ujumbe katika simu yangu kutoka kwenye simu yangu ya kiganjani kutoka kwa Mkuu wa Mkoa inayonitishia na kuweka maisha yangu kwenye hali ya hatari na ujumbe huo unasema “ UMERUKA KIHUNZI CHA KWANZA , NITAKUONYESHA KUWA MIMI NI SERIKALI ULIKOJIFICHA NITAKUPATA NA NITAKUPA KESI NINAYOTAKA MIMI “ Mwisho wa kunukuu .

Mwisho, Ninamshukuru kijana aliyerekodi tukio lote kuanzia mwanzo mpaka mwisho na hivi tutanza kusambaza video cd hizo Nchi ili watanzania wajue ukweli na Mh Rais aone utendaji mbovu wa wateule wake na vile nilitake Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria , maadili ,taratibu na kanuni za kazi na sio kuendesha Jeshi kwa matakwa ya kisiasa , kufanya hivi ni kuhatarisha usalama na utulivu wa Nchi yetu . 

“ Che Guavera alisema “ if you tremble indignation at every injustice then you are a comrade of mine “ 

Wanafunzi jipeni moyo bado kitambo kidogo Taifa hili litabadilika .


Godbless J Lema ( MP)