Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, June 23, 2014

VITA KUBWA DHIDI YA UJANGILI WA WANYAMA PORI NCHINI TANZANIA

Jamii hapa nchini  imetakiwa kushirikiana na serikali katika kuwafichua majangili wa wanyama pori katika hifadhi za taifa hapa nchini hali ambayo inalitia hasara taifa kwa kupunguza idadi ya watalii , pia kupoteza rasilimali ambayo ni urithi kwa vizazi vilivyopo na vile viajavyo.


Afisa wanyamapori wa malihai club Tanzania Saidi Mshana , ametoa kauli hiyo alipofanya ziara katika hifadhi ya taifa ya mlima kilimanjari (KINAPA), akiandamana na wanafunzi ambao ni wanachama wa club  hiyo  wapatao 160 , wanaosoma katika shule za sekondari za mikoa minne ya  kanda ya kaskazini kwa lengo la kupinga ujangili wa wanyama pori.

Bw. Mshana amesema vita vya  ujangili  wa wanyama pori ni vikubwa hapa nchini hivyo kila mtanzania anawajibu wa kushirikiana na serikali katika vita hivyo kwa kutoa taarifa kwenye vyombo husika pindi wanapobaini  mtandao wamajangili ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya wanafunzi Joshua John wa Arusha na Salome Jumbe wa Kilimanjaro  wamesema, umefika wakati sasa kwa serikali  kuchukua hatua madhubuti ikiwemo kutunga sheria zenye adhabu kali ili kila atakayebainika kujihusiha na mtandao ujangili ,aweze kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Aidha baadhi ya wanfunzi walioshiriki katika ziara hiyo Abubakari Molel wa Arusha na Emiliana Msodoka wa Tanga mkoani wameiomba wizara husika kuhamasiha jamii kushiriki katika utalii wa ndani kwa  kutoa matangazo kupitia katika vyombo mbalimbali vya habari pia kutoa elimu kuanzia shule za msingi na maeneo ya vijijini ili jamii iweze kunufaika na rasilimali zilizopo katika nchi yao.   

No comments:

Post a Comment