Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, August 6, 2014

KARIBU UPATE VIPIMO NA MATIBABU YA MACHO BURE

Habari njema kwa watanzania wote wenye matatizo ya macho winaoishi mkoa wa Kilimanjaro na maeneo ya karibu. Huduma hii ya kuvanyiwa vipimo vya macho na kupewa dawa au miwani inatolewa na madaktari kutoka Marekani wanaofahamika kwa jina la “Artists for world peace”. Huduma hiyo inapatikana bure na kwa mtu yeyote mwenye matatizo ya macho, anaweza kufika katika kijiji cha onan kuna katika kituo kipya cha afya kinaitwa “Good Hope” ila wakazi wa eneo hilo la kibosho wamezoea kupaita kwa “mayatima” kwa kuwa mmiliki wa kituo hicho ana kituo cha kuwalelea watoto yatima kinachofahamika kwa jina la “Good Hope”. Unaweza kupanda haice (daladala) zinazoelekea kibosho ubwe, katika stand kuu ya mabasi Moshi mjini kisha ukawaambia wakushushie kibosho ubwe au kwa raphael, ukishuka utaona pikipiki (bodaboda) unauliza kwenye huduma ya miwani, wakazi wote wa eneo hilo wanapafahamu na watakuelekeza, na kwa wale wenye usafiri binafsi wanaweza kufika bila tatizo lolote maana barabara ni nzuri. Na kwa mtu yeyote mwenye kuhitaji kupata maelekezo ya ziada anaweza kupiga namba hii +255 (0) 764 505 284 ni namba ya mama ni na anaitwa Josephine Machuwa. Na huduma itatolewa tena kuanzia tarehe 8 August 2014 hadi tarehe 10 August 2014 yaani ijumaa, jumamosi na jumapili kuanzia saa tatu asubui mapaka saa kumi na mbili jioni.

No comments:

Post a Comment