Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, March 18, 2018

MGANGA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO AFUNGA KAMBI YA WATOTO NA VIJANA YA AGPAHI MJINI MOSHI

 Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dr. Magoma ambaye ndie alikua mgeni rasmi katika hafla ya kufunga kambi ARIEL CAMP 2018, akiingia huku akiwa ameambatana na watoto, vijana, wafanyakazi wa AGPAHI pamoja na wauguzi waliokua wakiwaangalia watoto na vijana wakati wakiwa kambini.

Mmoja kati ya watoto waliohudhuria katika ARIEL CAMP 2018 akisoma risala mbele ya mgeni rasmi.

Mwakilishi wa wahudumu wa afya walioambatana na watoto, Bwana Aron Chasamawe kutoka Hospitali ya Wilaya ya Geita akizungumza kwa niaba ya wahudumu wengine.


Meneja Mawasiliano wa Shirika la AGPAHI, Bi Jane Shuma akizungumza kwa ufupi lengo la ARIEL CAMP 2018.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dr. Magoma akiongea wakati wa kufunga mafunzo ya watoto na vijana katika hafla fupi ya ufungaji wa kambi hiyo inayopewa jina la ARIEL CAMP 2018.
 
Hawa ni watoto walioweza kuigiza kama familia inayoishi vizuri kwa kula mlo kamili na pia kula kwa wakati sahihi.

 Hawa ni watoto walioweza kuigiza kama familia inayoishi maisha duni, ambapo baba wa hii familia alionekana kuendekeza pombe kuliko kuijali familia.


Miss ARIEL CAMP 2018 akipewa mkono wa pongezi na mgeni rasmi Dr. Magoma.

Watoto waliopata nafasi ya kuwawakilisha wenzao katika tendo la kukata cake wakiwa na mgeni rasmi.

 
Mgeni rasmi alipata nafasi ya kuwakabidhi zawadi za mabegi zilizokua zimeandaliwa na shirika la AGPAHI, kwaajili ya watoto na vijana wote waliohudhuria kwenye ARIEL CAMP 2018.



  Mgeni rasmi pia aliwatunuku vyeti wahudumu wote wa afya waliokua wameambatana na watoto katika   kufanikisha kambi hiyo.





Meneja Mawasiliano wa Shirika la AGPAHI, Bi Jane Shuma akimkabidhi mgeni rasmi zawadi.

      
       Jumatatu ya Tarehe 12/13/2017 Shirika lisilo la Kiserikali la Arial Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI)   lilianza kambi maalumu ya watoto na vijana wa Mikoa mitatu ya Tanzania kati ya Mikoa sita inayofanya kazi na shirika la AGPAHI. Leo ikiwa imetimia siku ya tano tokea mafunzo hayo ya kambi ya watoto yaanze.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dr. Best Richard Magoma alifunga mafunzo hayo ya watoto na vijana katika hafla fupi ya ufungaji wa kambi hiyo inayojulikana kama ARIEL CAMP 2018 huku ikiwa na kauli mbiu “KIJANA EPUKA TABIA HATARISHI ZINAZOWEZA KUSABABISHA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU.”

Meneja Mawasiliano wa Shirika la AGPAHI, Bi Jane Shuma aliweza kuzungumza kwa ufupi lengo la kambi kwa ambalo ni kutoa msaada wa kisaikolojia kwa watoto na vijana. Washiriki wakiwa kambini hupata mafunzo ya afya pamoja na kushiriki kwenye michezo mbalimbali. Aliweza kutoa shukrani za dhati kwa walezi walioambatana na watoto, daktari bingwa wa watoto, mtaalamu wa saikolojia, muelimishaji rika na wafanyakazi wa Shirika hilo kwa ushirikiano wao walioonesha katika kipindi chote cha kambi.

Mbali na mafunzo ya darasani, Meneja Mawasiliano aliweza kuzungumzia juu ya matembezi yalifanyika kwa washiriki wa Kambi kutembelea  Kiwanda cha Soda cha Bonite Bottlers ltd, na kutembelea Kijiji cha Uru Msuni, kilichopo katika kata ya Uru Kaskazini wilaya ya Moshi vijijini na kujifunza mila na tamaduni za wachaga, kilimo cha kahawa na migomba.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dr. Magoma, katika hotuba yake aliweza kutoa pongezi kwa shirika la AGPAHI kwa kuchagua Mkoa wa Kilimanjaro kufanyia mafunzo hayo huku akiwapongeza watoto na vijana kwa kuweza kujifunza na kuonesha kwa vitendo kile walichojifunza kwa siku zote hizo.

“Nimefarijika sana kuona mkiwa na tumaini kuu, hakika niwapongeze walezi wenu waliokua nanyi kwa siku zote hapa na kuwafundisha vyema, Nimetazama igizo lenu, limeelezea kile mlichojifunza na kudhihirisha kuwa mmeelewa. Sasa mkawe mabalozi wazuri kwa wenzenu maana nimepewa taarifa kuwa mpo zaidi ya watoto elfu tano (5,000) kwenye klabu mnazotokea na ninyi ni wawakilishi wa kundi hilo kubwa.” Alisema Dr. Magoma.

Kwa upande mwingine, mwakilishi wa wahudumu wa afya walioambatana na watoto, Bwana Aron Chasamawe kutoka Hospitali ya Wilaya ya Geita aliweza kuzungumza kwa niaba ya wahudumu wengine na kutoa pongezi za dhati kwa watoto kwa kuweza kuwa wasikivu na kuonesha nia ya kujifunza na wamepokea kile ambacho walitarajia kuwapatia katika Mafunzo. Pia hakusita kuonesha shukrani zake za dhati kwa shirika la AGPAHI kwa kuweza kuchagua watoto na vijana kama kundi muhimu katika vita dhidi ya Virusi Vya Ukimwi.
“Ni jukumu letu kuwasaidia vijana hawa, Ni vijana wenye hari, moyo wa kujituma na ndoto za kufika mbali na nina hakika watafika mbali” Alimaliza kwa kusema Bwana Chesamawe.

Dr. Magoma alimaliza ufungaji wa kambi hiyo kwa kuweza kuwapatia watoto na vijana zawadi ambazo ziliandaliwa na Shirika la AGPAHI pamoja na kuwatunuku vyeti wahudumu wote wa afya waliombatana na watoto na kufanikisha kambi hiyo.

Kilimanjaro Media iliweza kuzungumza na mmoja wa watoto hao baada ya kukamilika kwa kambi hiyo ambaye aliweza kuelezea furaha yake kwa kuweza kuwa mmoja wa watoto ambao wamewakilisha kundi kubwa la watoto  wenzao.
“Mimi nimetoka Tanga nimekuja katika kambi, lakini nilivyotoka Tanga na ninavyorudi ni tofauti, nimejivunza mambo mengi sana katika kambi hii.

Saturday, March 17, 2018

Mobile Week Kutoa Simu za Kisasa kwa Bei Cheee

Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (kati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Simu (Mobile Week) itakayofanyika Machi 24 - 30 na kutoa ofa kabambe ya punguzo la bei kwa manunuzi simu za kisasa za mkononi kupitia tovuti ya Jumia (www.jumia.co.tz). Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Jumia, Zadok Prescott pamoja na Meneja Uhusiano wa Tecno, Eric Mkomoye (kushoto).


Mkurugenzi Mtendaji wa Jumia, Zadok Prescott (wa pili kulia)

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Simu (Mobile Week) itakayofanyika Machi 24 - 30 na kutoa ofa kabambe ya punguzo la bei kwa manunuzi simu za kisasa za mkononi kupitia tovuti ya Jumia (www.jumia.co.tz). Waliombatana naye ni Mkurugenzi wa Samsung Tanzania, Suleiman Mohammed (wa kwanza kulia), Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (wa pili kushoto) pamoja na Meneja Uhusiano wa Tecno, Eric Mkomoye (kushoto).


Mkurugenzi wa Samsung Tanzania, Suleiman Mohammed (wa kwanza kulia)

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Simu (Mobile Week) itakayofanyika Machi 24 - 30 na kutoa ofa kabambe ya punguzo la bei kwa manunuzi simu za kisasa za mkononi kupitia tovuti ya Jumia (www.jumia.co.tz). Ameambatana na
Mkurugenzi Mtendaji wa Jumia, Zadok Prescott (wa pili kulia)


Meneja Mawasiliano wa Tigo Tanzania, Woinde Shisael (wa pili kushoto) pamoja na Meneja Uhusiano wa Tecno, Eric Mkomoye (kushoto).
Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Wiki ya Simu (Mobile Week) itakayofanyika Machi 24 - 30 na kutoa ofa kabambe ya punguzo la bei kwa wanunuzi wa simu za kisasa za mkononi kupitia tovuti ya Jumia (www.jumia.co.tz).
Tigo Tanzania na Jumia wanaungana kutoa punguzo la hadi asilimia 60% kwa simu za kisasa

Ofa za moja kwa moja hadi GB 18 za intaneti kutoka Tigo kwa kila simu itakayonunuliwa kupitia Mobile Week.

Dar es Salaam, 15 Machi, 2018.
Wateja watafurahia punguzo kubwa la bei hadi 60% kwa simu za kisasa (smartphone) kupitia Jumia Mobile Week (wiki ya simu) itakayofanyika kwenye mtandao wa manunuzi ya bidhaa wa Jumia (www.jumia.co.tz). Pamoja na punguzo hili kubwa la bei, simu zote za kisasa zitakazouzwa katika promosheni hii zitakuwa na ofa ya hadi GB 18 ya intaneti bure kutoka kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali ya Tigo Tanzania.

Katika uzinduzi wa gulio hilo la simu kwa njia ya mtandao, Jumia pia walizindua Ripoti ya Sekta ya Simu za Mkononi Tanzania inayoonesha kuwa asilimia 83% ya Watanzania walitembelea mtandao wa Jumia kupitia simu zao za mkononi, ikilinganishwa na asilimia 17% tu waliotumia kompyuta. Matokeo haya yanadhihirisha kuwa Watanzania wengi wamevuka kigezo cha matumizi ya kompyuta na badala yake wanatumia teknologia ya simu za mkononi kutekeleza shughuli zao za kila siku.

Akitangaza ushirikiano huo kabambe jijini Dar es Salaam, Meneja Mawasiliano wa Tigo, Woinde Shisael alisema kuwa Mobile Week itakayoanza 24 – 30 Machi ndio muda muafaka zaidi wa kununua simu ya kisasa kwa sababu simu zote zitapatikana kwa bei nafuu zaidi ambazo hazijawahi kutokea nchini, huku kila simu ikiwa na ofa ya hadi GB 18 za intaneti kutoka Tigo.

‘Tigo inaongoza katika mageuzi ya maisha ya kidigitali. Lengo letu ni kuongeza idadi ya watumiaji wa simu za kisasa nchini huku tukihakikisha kuwa wateja wetu wote wanapata huduma bora, za uhakika za mtandao. Huduma bora za kidigitali zinaanza na vifaa bora, ndio maana ushirikiano wetu na Jumia utahakikisha kuwa kila mmoja anapata simu mpya ya kisasa pamoja na ofa za intaneti zitakazomwezesha mtumiaji kuwa sehemu ya maisha ya kidigitali,’ alisema.

Akifafanua jinsi ya kupata ofa hizi za simu, Mkurugenzi Mtendaji wa Jumia Tanzania, Zadok Prescott aliwashauri wateja kutembelea tovuti ya www.jumia.co.tz ambapo watapata aina mbali mbali za simu kutoka kwa wauzaji mbali mbali. Baada ya hapo wanaweza kuchagua aina ya simu wanayoipenda na kutoa maelekezo ya sehemu ambapo wangependa kuletewa simu yenyewe na watoa huduma wa Jumia. Wasiokuwa na huduma za mtandao wanaweza kupiga simu namba 0800 710024 bila gharama yoyote ili kutoa maombi ya simu wanayoitaka.

‘Nawahamasisha nyote mchangamkie ofa kabambe za simu zitakazopatikana katika mtandao wa Jumia katika kipindi hiki cha Mobile Week. Tunafurahia kuleta pamoja baadhi ya kampuni kubwa zaidi za simu duniani kama vile Tigo, Samsung, Tecno na Infinix kushiriki katika gulio hili la kila mwaka. Kwa pamoja tumefanikiwa kuwaletea ofa ambazo hazijawahi kutokea kwa simu za kisasa, ikiwemo simu zenye uwezo wa 3G zitakazopatikana kuanzia TZS 50,000/- pekee na zile za 4G zitakazopatikana kwa chini ya TZS 150,000/- tu,’ Zadok alisema.

‘Wateja wana uhuru wa kuja kuchukua simu zao kutoka katika ofisi za Jumia ama wanaweza kuletewa simu zao mahali popote walipo. Malipo kwa ajili ya simu yatafanyika kwa njia ya Tigo Pesa au kwa pesa taslim mara tu baada ya mteja kupokea simu aliyoagiza na sio vinginevyo. Hii inaondoa hofu ya kutapeliwa,’ Zadok alimaliza.

Ukuaji wa simu za kisasa (smartphone) unatoa fursa kubwa kwa matumizi ya mtandao kutoa huduma mbali mbali kwa Watanzania kupitia mifumo kama Jumia. Hivi karibuni idadi ya watumiaji wa simu za mkononi nchini ilifikia watu milioni 40, huku idadi ya wanaotumia mtandao ifikia watu 23 milioni.

“Idadi ya watu wanaotumia simu za kisasa inakua kwa kasi siku hadi siku. Hii ni hatua muhimu katika maendeleo ya simu za mkononi, ila upatikanaji wa vifaa vya kisasa bado ni changamoto kubwa. Jumia imejikita kuhakikisha kuwa Watanzania wote wanapata simu za kisasa, hasa katika kipindi hiki cha Mobile Week,” Zadok alibainisha

Friday, March 16, 2018

YALIYOJIRI KWENYE KAMBI YA WATOTO – MOSHI, KILIMANJARO


Afisa Rasilimali watu (HR) wa kiwanda cha Bonite Bottlers Ltd, akiwakaribisha watoto na vijana kutoka katika shirika la AGPAHI  na kuwapa maelekezo ya utangulizi kabla ya kuingia ndani ya kiwanda hicho.

Picha ya pamoja ya wafanyakazi, wototo, vijana kutoka katika shirika la AGPAHI wakiwa na wahudumu wa afya waliokua wameambatana nao katika ziara ya kutembelea kiwanda cha Bonite Bottlers Ltd. 
    
Peter Zakaria, Msimamizi wa Mradi wa Kilimani Coffee Culture Tourism Enterprise maarufu kama  Kahawa Shambani akiwakaribisha watoto kutoka katika shirika la AGPAHI kwa kuwapa kila mmoja kikombe cha kahawa.

Deogratias Michael mmoja kati ya wafanyakazi katika Mradi wa Kilimani Coffee Culture Tourism Enterprise  akiwapa maelekezo namna ambavyo zao la kahawa linavyolimwa kuanzia ngazi ya awali mpaka linapofikia hatua ya kuvunwa na kuandaliwa kwajili ya kutumika kama kinywaji.

 Mmoja kati ya wafanyakazi katika Mradi wa Kilimani Coffee Culture Tourism Enterprise  akiwaonesha watoto kahawa.

Picha ya pamoja ya wafanyakazi, wototo, vijana kutoka katika shirika la AGPAHI wakiwa na wahudumu wa afya walipotembelea Mradi wa Kilimani Coffee Culture Tourism Enterprise maarufu kama  Kahawa Shambani.
Baadhi ya wafanyakazi wa AGPAHI wakipatiwa maelezo ya namna ambavyo Kliniki ya Watoto na Familia (CCFCC) inavyotoa huduma.
Baadhi ya wafanyakazi wa AGPAHI wakiwa katika picha ya pamoja na wahudumu wa afya siku walipotembelea Hospital ya KCMC katika Kliniki ya Watoto na Familia (CCFCC)

 

Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) leo limeendelea na mafunzo ya vijana yanayoendelea Mjini Moshi, Mkoani Kilimanjaro.
Siku ya Alhamisi, 15 Machi 2018, Watoto na Vijana walipata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali ndani ya mji wa Moshi ikiwa ni siku maalumu ya mafunzo ya nje ya Darasa. Mji wa Moshi ni mji wa kitalii unaosifika kwa usafi wa Mazingira, na ndipo ulipo Mlima mrefu kuliko yote Barani Afrika, Mlima Kilimanjaro na pembezoni mwa mji huu kuna Viwanda mbalimbali vinavyozalisha bidhaa mbalimbali.

Asubuhi ya Leo watoto waliweza kufurahia mandhari halisi ya Mji wa Moshi pamoja na kutembelea kiwanda cha Bonite Bottlers Ltd, kilichopo mjini Moshi kinachotengeneza soda jamii ya Cocacola. Baada ya kufika kiwandani hapo walipokelewa na Afisa Rasilimali watu (HR) wa kiwanda hicho na kuweza kuwakaribisha ndani ya kiwanda hicho.

Watoto na Vijana walitembelea sehemu ya uhifadhi wa maji machafu yanayotoka kiwandani na kusafishwa tena kwa ajili ya matumizi mengine nje ya matumizi ya uzalishaji kiwandani. Uhifadhi wa maji haya ni jitihada ya utunzaji wa mazingira wa kiwanda hicho.

Pia baada ya kuona mfumo huo wa maji walipata fursa ya kutembelea sehemu ya uzalishaji wa maji ya kunywa ya Kilimanjaro ambayo yanatengenezwa na kiwanda hicho, sambamba waliweza kuona utengenezwaji wa chupa za maji, vifuniko na upakiaji wa maji katika vifungashio vyake. Mbali na maji waliweza kuona utengenezwaji wa soda wa kampuni ya Coca Cola na walipata fursa ya kunywa soda zinazotengenezwa kiwandani hapo.

Safari haikuishia hapo, baada ya kumaliza ziara katika kiwanda cha soda safari nyingine ilianza ya kutembelea Kijiji cha Uru Msuni, kata ya Uru Kaskazini katika wilaya ya Moshi Vijijini na kuweza kujifunza mila na tamaduni za wachaga ambao ndio wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro. Watoto waliweza kujifunza kilimo cha kahawa hadi kufikia hatua ya kutumika kama kinywaji.

Ndugu Peter Zakaria, Msimamizi wa Mradi wa Kilimani Coffee Culture Tourism Enterprise maarufu kama Kahawa Shambani aliwapokea watoto wa Kambi na kuwaeleza historia fupi ya Kahawa  Shambani. Pia walijifunza historia ya wachaga wanaoishi ndani ya jamii ya watu wa Uru sambamba na faida ya zao la kahawa na faida ya mradi huo kwa kijiji.

Kwa mwaka tunapokea wageni zaidi ya 1,400 ambao wanatembelea kujifunza, asilimia 60-70 ya malipo yanayolipwa na wageni hutumika katika miradi ya maendeleo ya kijiji.” Alisema Peter. Mbali na maelezo hayo watoto na vijana walipata fursa ya kwenda shambani kuona kahawa na kujifunza namna ambavyo kahawa inalimwa, utunzaji wake, Uvunwaji pamoja na uandaaji wa kahawa kwa ajili ya matumizi ya kinywaji.

Kupitia safari hiyo watoto na vijana walifurahi kufahamu kuhusu jamii ya wachaga pamoja na elimu waliyopata juu ya zao la kahawa. Pia waliweza kuona mlima Kilimanjaro kwa ukaribu zaidi ambapo watoto na vijana walionekana kuufurahia sana mlima huo mrefu kuliko yote barani Afrika. Huku shukrani za pekee wakiipa shirika la AGPAHI pamoja na wafadhili waliowezesha wao kuweza kupata fursa ya kujifunza.
Vilevile, katika juma hilo la kambi ya watoto, wahudumu wa afya pamoja na wafanyakazi wa AGPAHI walitembelea Kliniki ya Watoto na Familia (CCFCC) iliyopo katika Hospitali ya KCMC mkoani Kilimanjaro.

Lengo kuu ilikua ni kujifunza jinsi kituo cha matunzo na matibabu cha KCMC kinavyotenda kazi. Kliniki hii ilifurahisha wengi kwani ni kubwa na ina vitengo vyote vya muhimu. Inahudumia familia nzima kwa wakati mmoja na huduma za muhimu kama kumuona daktari, kuchukua dawa, kuchukuliwa vipimo vya magonjwa nyemelezi na uzazi wa mpango vyote hupatikana ndani ya jengo moja.

Washiriki walijifunza jinsi kituo cha CCFCC kinavyotoa kipaumbele katika kutoa huduma za kisaikolojia kwa watoto na vijana. Watoto na vijana wana siku maalum ya kukutana ambapo hupata elimu, msaada wa kisaikolojia na kuangaliwa na daktari mwenendo wa afya zao.…mkusanyiko huu hufanyika mara moja kwa mwezi. Safari hii imekua na manufaa makubwa kwa wahudumu wa afya waliotoka vituo mbalimbali vya mikoa ya Tanga, Geita na Mwanza.

Serikali yajipanga kupokea mradi wa Global Learning XPRIZE


Serikali imesema inajiandaa kuupokea mradi wa ‘Global Learning XPRIZE’ unaowawezesha watoto walio nje ya mfumo rasmi kujifunza stadi za msingi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kupitia Michezo iliyowekwa kwenye tableti, kutoka kwa wadau wanaoufadhili baada ya kumalizika muda wa majaribio. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka TAMISEMI anayeshughulikia elimu nje ya mfumo rasmi na Elimu ya Watu Wazima, Odilia Mushi wakati akizungumza katika mkutano uliokutanisha wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), na taasisi mbalimbali za serikali. 


Mkurugenzi Msaidizi kutoka TAMISEMI anayeshughulikia elimu nje ya mfumo rasmi na Elimu ya Watu Wazima, Odilia Mushi akizungumza kuhusu maandalizi ya serikali kuupokea mradi wa Global Learning XPRIZE.

“Kama serikali mradi unapomalizika tunaangalia namna ya kuuendeleza. Tutaendelea kushirikiana na halmashauri zetu zilizoko kwenye mradi wauone kama ni wa kwao na kwamba badala ya watoto kuzurura mitaani wanaendelea kujifunza,” amesema Mushi na kuongeza. “Tunaagiza wale wahusika, wadau wa elimu katika ngazi zote za kijiji hadi mkoa wa Tanga waone kama hiki kilicholetwa kwetu ni zawadi,na ni lazima kuuendeleza ili kupunguza watoto walioko nje ya mfumo rasmi; kwa maana hiyo inatakiwa tuwe na ushirikiano kuona changamoto baada ya huu mradi kumalizika ili kuzifanyia kazi.” 
Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Faith Shayo akizungumza kuhusu mradi wa Global Learning XPRIZE.

Akielezea utekelezaji wa mradi huo tangu ulipoanza na ulipofikia, Afisa Msaidizi wa Mradi kutoka UNESCO, amesema hadi sasa watoto zaidi ya 2000 kutoka vitongoji 141 katika wilaya 6 za mkoa wa Tanga wamenufaika na mradi huo. “Baada ya miezi 15 ya mradi kukamilika, mradi utakabidhiwa kwa serikali ili kuendelea kuusimamia. , ambapo tumekutana leo Tarehe 13/3/2018 na wawakilishi kutoka Baraza la Mitihani la Tanzania (BMT) , Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na TAMISEMI ili kuweza kuangalia ni jinsi gani watoto walio katika mradi wataingia katika mfumo rasmi katika ngazi husika,” amesema.


Wadau mbalimbali wakichangia katika mkutano uliokutanisha wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), na taasisi mbalimbali za serikali kuhusu mradi wa Global Learning XPRIZE.





Washiriki wa mkutano uliokutanisha wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), na taasisi mbalimbali za serikali kuhusu mradi wa Global Learning XPRIZE.