Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, July 29, 2012

VAZI LA WOLPER LASHANGAZA UMATI KWENYE UZINDUZI WA ALBUMU ZA INJILI...!


Wengi tumezoea kumuona gwiji wa filamu za kibongo Jackline Wolper katika mavazi ya tite jeans, vimini, na bluzi zenye kuonyesha umbile lake lilivyo, Lakini hivi karibuni Wolper alialikwa kwenye tamasha la uzinduzi wa albamu za injili mkoani Iringa ambako mwanadada Wolper alishangaza umati kwa muonekano wa  tofauti sana,, maana alikuwa amevaa gauni refu la la heshima sana na kwa kweli alipendeza kupita maelezo.Na uvaaji huo umempa heshima kubwa kutokana na kuendana na maadili.
Katika uzinduzi wa huo alikuwa na msanii mwenzake, Masanja Mkandamizaji ukipenda unaweza kumuita mchungaji mtarajiwa na wengine walikuwa ni waimbaji wa nyimbo za dini..

Ingawa Wolper si mvaaji nusu uchi sana lakini gauni hilo lilimsitiri na kumpendeza haswa pamoja na kuwa ni mrefu na zito.

Mwenyewe anasema alivaa hivyo ili kuendana na tukio husika."“Ninajua kuwa mimi ni nyota kwa sasa najaribu kwenda na matukio katika uvaaji wangu nguo, siwezi kuvaa vazi la disco kanisani au msikitini," alisema na kuongeza;
"Leo hii ni uzinduzi wa albamu ya Masanja Mkandamizaji ambaye ni msanii mwenzetu nasi tumekuja kumsindikiza, nami namtukuza Mungu hata katika kuvaa kama unavyoniona nikiwa katika gauni safi tena la kiheshima,”alisema alipokuwa akihojiwa na muwakilishi wa kingjofa blog.

No comments:

Post a Comment