Saturday, May 25, 2013

VITA YA GESI MTWARA: WABUNGEA WA CCM WACHARUKA...!

Dodoma: Wabunge wa CCM wamekuja juu na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuwafukuza kazi vigogo wa Serikali mkoani Mtwara, wakiwamo Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya kutokana na kile walichoeleza ni uzembe uliochangia vurugu zinazoendelea za wananchi kugomea gesi kutoka nje ya mkoa huo.

Askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakifanya doria katika mitaa ya Mji wa Mtwara

Wengine waliopendekezwa kuchukuliwa hatua ni kamati nzima ya ulinzi na usalama ya ngazi ya mkoa na wilaya ya Mtwara mjini, wakiwamo makamanda wa polisi.

Kutokana na hali hiyo, vigogo kadhaa mkoani humo wako hatarini kukumbwa na ghadhabu hiyo akiwamo Mkuu wa vikosi vya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Mkuu wa mgambo na Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Wabunge hao walikuwa wakitoa mapendekezo hayo kwenye kikao cha Kamati ya Wabunge wa CCM iliyofanya kikao cha dharura juzi usiku, mjini hapa.

Kikao hicho kiliongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, huku Spika wa Bunge, Anne Makinda ambaye wakati huo alikuwa kwenye kikao cha Kamati ya Uongozi wa Bunge, aliwakilishwa na Mwenyekiti wa Bunge, Jenista Mhagama.

Katika kikao hicho maalumu kilichokusudia kutoa ushauri kwa Rais Kikwete juu ya njia mwafaka ya kutatua hali ya machafuko, wabunge wengi wali kukasirishwa na jinsi hali ilivyo mkoani Mtwara.
Chanzo chetu kwenye kikao hicho kilieleza kuwa wabunge hao walichukizwa na jinsi Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya walivyokuwa wakipingana kimsimamo. Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Joseph Simbakalila, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mjini, Wilman Ndile na Kamanda wa Polisi Mkoa Linus Sinzumwa wamehusishwa.


Licha ya baadaye kuonekana kuwa kitu kimoja, wabunge hao walidai kuwa walishindwa kutumia nafasi zao katika kutatua tatizo hilo, ambalo hadi juzi Serikali ilisema walikuwa wamekufa watu watano, wakiwamo wanajeshi wa JWTZ waliofariki katika ajali wakati wakienda kutuliza machafuko.

Chanzo hicho kilieleza kuwa iwapo mapendekezo ya wabunge hao yatapelekwa kwa Rais Kikwete kama michango ya wabunge hao ilivyokuwa, huenda rungu likawaangukia pia viongozi wa kisiasa wa CCM mkoani humo. Miongoni mwa wanasiasa hao, chanzo hicho kimesema ni wale waliotoa kauli za waziwazi kuunga mkono msimamo wa kutoruhusu gesi kusafirishwa nje ya mkoa huo.

“Hapa wapo wabunge, madiwani na viongozi wa ngazi mbalimbali wa CCM,” kilieleza chanzo hicho.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge walipendekeza mkakati wa kutatua uzembe uliofanyika Mtwara, unapaswa kuchukuliwa kwa uangalifu usije ukasababisha madhara mengine kwa Chama na Serikali.

Walisema suala hilo halina budi kuchukuliwa kwa uangalifu hasa ikizingatiwa kuwa Chama cha CUF ndicho chenye nguvu mkoani humo ukilinganisha na vyama vingine vya upinzani.

Wabunge hao walikituhumu chama hicho kuwa kimekuwa kikijaribu kutumia vurugu hizo kama kigezo cha ushawishi wa kukubalika mkoani humo.

Thursday, May 23, 2013

MTWARA UPDATE.. GESI GESI WAR...!




Ambulance ya Manispaa Kwisha

  • Kuna madai ambayo hayajathibitishwa kwamba wanawake wanabakwa na maaskari, wanapigwa risasi kutokana na vijana wote kukimbia maporini.
  • Mwanamke anayekadiriwa miaka 25 mjamzito auawa kwa kupigwa risasi maiti ipo Ligula.
  •  Mwanafunzi wa CHUNO afikishwa hospitali  Ligula na majeraha ya risasi mguuni.
  • Maduka maeneo ya Magomeni yamechomwa moto ikiwamo pia mali za Askari magereza na uhalifu ukifanyika vidole vinawaelekea Polisi.
  • Afisa Usalama wa Taifa ambaye anamiliki nyumba ya wageni naye amevamiwa na kuporwa mali ikiwamo fedha katika gesti yake. Haijajulikana ni kiasi gani cha mali kilichopotea.
  • Mabomu yanaendelea kupigwa tofauti kwa sasa hayapigw mfululizo.
  •  Mabomu yametulia. Hali ya ukimya imetawala.
  • Mabasi 5 ya Champion yamebeba Wanajeshi yako njiani yanakuja.
  •  Serikali yatoa tamko yasema watu 91 wanashikiliwa.
  • Bunge laahirishwa tena. Kupisha uchunguzi na kuepusha uchochezi kutoka kwa baadhi ya wabunge. (Kwa mujibu wa Spika)
  •  Maeneo ya Magomeni, Chikongola, Nkanaledi, Mikindani  maaskari wanaingia majumbani mwa watu na kumsomba mtu yeyote ambaye ni mwanaume awe amehusika awe hajahusika na kumkamata. Pia inaripotiwa na uhalifu unafanywa na maaskari hao hao.  Jambo linaloamsha hisia kwa wananchi.
  • RPC anaongea na vyombo vya habari na kuwasihi wananchi waende makazini. Lakini kiuhalisia hali sio shwari.
  • Mahakama ya mwanzo ya Mitengo imechomwa moto
  • Mpaka sasa ni vita baina ya wananchi na maaskari. Mabomu yamesikika pamoja na milio ya risasi masaa 24. Na milio ya Risasi na mabomu inaendelea kusikika.
  • Raia wapatao 7 wameripotiwa kufariki (wengine walipelekwa hospitali ya Ndanda Ndogo na mmoja ameripotiwa kupokelewa Ligula.
  • Nyumba za viongozi zinaendelea kuchomwa moto.
  • Majibizano baina ya Polisi na Raia yanaendelea maeneo ya Magomeni, Nkanaledi na Mikindani.

  • Maduka yamefungwa na hakuna huduma zozote
Barabara zimewekwa vizuizi magogo na matairi yamechomwa moto. Hakuna njia ya kupita.  

Source: mtwarakumekucha blog

Arusha: Washirika sita wa ‘polisi wa bangi’ wakamatwa wakiwa na magunia 3..!

Kamanda wa Polisi mkoani Arusha Leberatus Sabas akionyesha bangi iliyokamatwa jana
Polisi mkoani Arusha, imekamata magunia mengine 30 ya dawa za kulevya aina ya bangi kwa watu sita ambao inadaiwa ni washirika wa polisi wawili, waliokamatwa na magunia 18 ya bangi katika maeneo ya Himo mkoani Kilimanjaro.
Kamanda wa Polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema watuhumiwa hao, walikamatwa Mei 19 saa 10 jioni katika Kijiji cha Kisimiri juu, Kata ya Ngaramtoni wilayani Arumeru.
“Wakati askari hao, waliokamatwa mkoani Kilimanjaro, polisi mkoani Arusha pia tulikuwa katika msako wa kuwatafuta watuhumiwa wengine wanaoshirikiana na polisi hao, katika biashara ya kusafirisha bangi kutoka Arumeru kupeleka nchini Kenya,” alisema Sabas.
“Siku za karibuni tulipata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba kuna mtandao wa wahalifu wanaoshirikiana na baadhi ya polisi wasiyo waaminifu,” alisema Kamanda Sabas.
“Watuhumiwa hawa walifanikiwa kukimbia kabla ya kukamatwa na kutelekeza bangi hiyo kwenye nyumba zao”alisema Sabas.
Kamanda Sabas alisema uchunguzi wa tukio hilo, ukikamilika watuhumiwa hao, watafikishwa mahakamani.
Habari zilizopatikana baadaye jana kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz kuwa askari wawili waliokamatwa juzi na magunia 18 ya bangi, watashtakiwa katika mahakama za kiraia kama wakosefu wengine.
Wakati huo huo, Kamanda Sabas jana alikiri kuwapo taarifa ya kuuawa Watanzania watatu nchini Kenya kwa tuhuma za ujambazi na kupatikana na bunduki ya polisi aina ya Sub Mashine Gun (SMG).
Watanzania hao,Tigiki Pasto,Steven Webo na mmoja ametambulika kwa jina moja la Kadogoo, waliuawa Mei2, mwaka huu baada ya kuvamia wafanyabiasha na kuwapora na kuwaua wawili.
Hata hivyo, baadaye walizingirwa na wananchi hao na kuuawa na ndipo waliipata bunduki hiyo mali ya polisi.
“Ni kweli tukio hilo lipo, ila sasa kwa kuwa linahusisha nchi mbili, linashughulikiwa kwa taratibu nyingine za nchi na nchi”alisema Kamanda Sabas.
Hata hivyo, alikiri pia kushikiliwa kwa polisi wawili kwa uchunguzi kutokana na kupotea kwa silaha hiyo, kwenye ghala la polisi Wilaya ya Ngorongoro.
Matukio ya polisi kujihusisha kwenye vitendo viovu yalikuwa yakilalamikiwa kwa siku nyingi bila kuchukua hatua. Lakini tangu mwaka huu uanze Polisi makao makuu wametangaza kuwasafisha polisi wote wanaojihusisha katika matukio maovu.


source:mwananchi

Wednesday, May 22, 2013

HALI YA MTWARA YAZIDI KUWA MBAYA.. FUJO ZAZIDI KUTAWALA. NYUMBA ZAZIDI KUCHOMWA MOTO...!


 Hadi kufikia saa hii (3:00 pm) kuna taarifa kwamba ofisiza CCM (maeneo ya Mdenganamadi na Majengo) zimechomwa moto; askari wanne wameuawa pamoja na wananchi kadhaa. Wananchi wanatumia baruti za kulipulia samaki kuwalipua majengo na askari.Hatari iliyopo ni kuchomwa kwa jengo la ofisi za mkuu wa mkoa. Yote haya ni.
kupinga bomba la gesi kujengwa kuelekea DSM.

SOURCE: Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha SAUT-TWARA
**************
Habari zilizoifikia Maisha Times muda huu zinaripoti kwamba hali sio nzuri huko Mtwara, kwa ufupi hali ni tete na hakuna amani, mabomu ya machozi yanarindima muda huu na huduma zote za kijamii zimefunngwa hakuna usafiri, masoko, maduka na bar zote zimefungwa, daladala, Taxi na Bodaboda hazifanyi kazi. Kwa ujumla kinachoendelea ni mapambano makali kati ya Jeshi la polisi na wananchi wenye hasira wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato wa gesi ilihali nchi ikiwa haina sera inayosimamia nishati hiyo.
Kufuatia Kambi ya Upinzani kuukataa mpango wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara Mpaka Dar es salaam ilihali Waziri wa Nishati akisoma hotuba yake kwa hisia kali na mbwembwe na kusema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar es salaam Wananchi wa Mtwara wacharuka!


Daraja la Mikindani limevunjwa hakuna mawasiliano Mtwara na Dar es salaam.

Baadhi ya Wananchi wamepora Silaha na wanazitumia kujibu mashambulizi ya Jeshi la Polisi (habari haijathibitishwa rasmi)

Jengo la Ofisi ya CCM saba saba limechomwa moto.

Nyumba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi), Hawa Ghasia yachomwa moto.

Lodge/Hotel (Shengena) inayoaminika kwamba ndiyo waliyofikia Askari wa Jeshi la Polisi (FFU) kutoka mikoa ya jirani kwaajili ya operation inayoendelea imechomwa moto.

Milio ya risasi na mabomu ndicho kinachosikika.

Nyumba kadhaa za watumishi wa Serikali zimechomwa maeneo ya Shangani. (habari haijathibitishwa rasmi)

Ni magari ya FFU ndio yaliyopo barabarani nayo yanapata wakati mgumu kupita kwasababu ya mawe na magogo makubwa yaliyowekwa na Wananchi.

Askari kadhaa wamekufa (habari hii haijathibitishwa rasmi)

Baadhi ya watu kadhaa wamechukuliwa na askari kwakuwa wamepita jirani na gari yao.

Yadaiwa askari wengi waliokuja si wa Mtwara, wengi wametoka Masasi na Lindi.

Ving'ora vinalia hovyo. Watoto wamefungiwa mashuleni walimu wamekimbia.

Vituo vya Redio vya Mtwara havizungumzii hali hii ya hatari bali vinapiga Muziki pengine vinakusanya matukio na habari ya majanga haya ili Wananchi wayapate.

Mabomu yanapigwa mfululizo maeneo ya Magomeni-Mtwara, mpaka sasa takriban mabomu 20 na ushee yameshapigwa.

Wakati waziri wa Nishati akisoma hotuba yake kwa hisia kali na mbwembwe na kusema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar Kauli mbiu ya Wananchi wa Mtwara ni "Gesi haitoki hata kwa bomba la peni"
Wananchi walalamikia kituo cha Television na Radio TBC kuzuia na kukata mawimbi yake kutoonekana wala kusikika katika Mkoa wa Mtwara kwa muda. Hatimaye hivi Punde matangazo yarejea.

Hili linaendelea wakati bajeti ya nishati na madini ikiendelea kujadiliwa muda huu Bungeni.
Endelea kuwa nasi mpaka hapo baadae ambapo tutaweza kukujuza zaidi kile ambacho kinaendelea kutukia Mtwara.

Source: JamiiForum

HII NDIO VITA MPYA KATI YA "CCM" NA "CHADEMA"...!

MWENENDO wa Bunge la Bajeti linaloendelea mjini hapa, umebaini kuwa vita ya maneno, fitna kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), sasa imehamia bungeni, Tanzania Daima Jumatano limebaini.

Moto wa vita hiyo kati ya vyama hivyo hasimu, umekolezwa zaidi baada ya Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete kufanya mkutano wa kimkakati na wabunge wa chama chake mjini hapa.

Duru za siasa kutoka ndani ya kikao hicho cha wabunge na rais, zilieleza kuwa Rais Kikwete aliwataka wabunge hao wa CCM wajipange kukabiliana na hoja za CHADEMA ambazo katika siku za hivi karibuni zimeonekana kulitikisa Bunge kiasi cha kiti cha spika kuamua kutumia kanuni kandamizi kuzizima.

Wabunge wa CCM bila kujali uzito wa hoja, wameamua kukabiliana na hoja zozote za wabunge wa CHADEMA hata kama zina maslahi kwa taifa.

Tayari CHADEMA kimeeleza kubaini mbinu hizo, kikidai kuwa hata kitendo cha Spika Anne Makinda kukatisha hotuba ya msemaji wao katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Joseph Mbilinyi ilikuwa sehemu ya utekelezaji wa mkakati huo.

Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika alisema kuwa hatua hiyo ndiyo iliwafanya wasikubali kubadili hotuba yao hiyo kuanzia ukurasa wa kwanza hadi wa 14 kama ilivyotakiwa na spika kwani ni kinyume na kanuni ya 63 (2).



Kanuni hiyo inasema kuwa mbunge yeyote anayekuwa akisema bungeni hatachukuliwa anasema uongo iwapo atafanya rejea ya habari.

“Hivyo kambi kunukuu ripoti za Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Jukwaa la Wahariri (TEF), ile ya Kamati ya Waziri Emmanuel Nchimbi, makala ya Ndimara Tegambwage, Kamati ya Kulinda Waandishi wa Habari Ulimwenguni (CPJ) na Tume ya Haki za Binadamu haijavunja kanuni,” alisema.

Mnyika alifafanua kuwa CCM inafanya siasa bungeni kwa kuitumia vibaya kanuni ya 64 (1) (c) inayozuia mambo yanayosubiri uamuzi wa mahakama na kwamba ndiyo maana aliwahi kukata rufaa kuhusu jambo hilo.

“Kwa hiyo tulibaini mkakati wao huo wa kutaka kuzima hoja yetu iliyokuwa ikizungumzia vitendo vya utekaji na utesaji wa wanahabari ili kudhibiti hoja zenye ukweli,” alisema Mnyika.

Hata hivyo, kwa jinsi mjadala wa hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari ulivyoendeshwa na Spika Makinda, imeonesha wazi kuwa kuna upendeleo kwa wabunge wa CCM hasa wanapochangia kujibu hoja za CHADEMA.

Mathalani Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Kigoma, Sabrena Sungura (CHADEMA) jana alizuiliwa na spika kunukuu makala ya mwandishi nguli nchini Tegambwage iliyochapishwa katika gazeri la Tanzania Daima ikiwataja waandishi wa habari waliowahi kupata vitisho, kuumizwa na kuuawa.

Licha ya kanuni za Bunge kumpa fursa ya kufanya hivyo, lakini katika hali ya kushangaza spika alimtaka asiendelee kuzungumza suala hilo kwa madai kuwa ni uchochezi kwa kuwa matukio mengine kesi zao ziko mahakamani.

Lakini muda mfupi baadaye, Mbunge wa Viti Maalumu, Mkoa wa Iringa, Ritta Kabati wakati akichangia alidai kuwa Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), aliwachochea vijana mjini humo wafanye vurugu na hivyo vijana hao zaidi ya 50 kufikishwa mahakamani.

Licha ya Kabati kuzungumza suala hilo kwa makusudi wakati akijua liko mahakamani, si spika wala Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyeshtuka kumzuia kuendelea kufanya hivyo, badala yake wabunge wa CCM walizidi kumpigia makofi.

Hata Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba katika mchango wake aliwashambulia wabunge wa CHADEMA hususani Mnadhimu wao Mkuu, Tundu Lissu akidai kuwa wanahitaji kupelekwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kujifunza uzalendo waache kuzungumza kauli za uchochezi bungeni.

Pamoja na kwamba Komba alidanganya Bunge kwa vile Lissu amepitia JKT mwaka mmoja kupitia Oparesheni Programu ya Chama mwaka 1989 hadi 1990, Spika wa Bunge naye aliunga mkono akisema apelekwe huko mwaka mmoja.

Wabunge wengi wa CCM waliochangia hotuba hiyo, walijaribu kuvishambulia vyombo vya habari wakidai vinawaandika sana CHADEMA kuliko wabunge wengine.

Katika kile kinachoonesha kuwa wabunge wa CCM wanaumizwa na mwenendo wa vyombo hivyo kuwapa nafasi kubwa viongozi wa upinzani kuliko wale wa serikali, Mbunge wa Viti Maalumu, Tuahida Nyimbo (CCM) alishauri uwekwe utaratibu wa habari kutangazwa kwa kufuata itifaki.

Mbunge huyo alisema inashangaza kuona taarifa za habari zinaanza kuwaonesha watu wengine kama wabunge wanaofanya vurugu bungeni na ile ya rais anayeelezea maendeleo inawekwa mbali.

Katika kuhaha huko kujinusuru bungeni, CCM katika kikao chake baina ya wabunge na Rais Kikwete, iliwanyoshea vidole wabunge wake watatu ikipinga hatua yao ya kuikosoa serikali kwa mtindo unaowapa nguvu CHADEMA.

Wabunge hao ni Kangi Lugola (Mwibara), Deo Filikunjombe (Ludewa) na Luhaga Mpina (Kisesa) ambao hata hivyo wote wameapa kuendelea na msimamo wao wa kuikosoa serikali na kupinga ufisadi pale watakapobaini upungufu.

Mmoja wa wabunge hao ambae aliomba kuhifadhiwa jina, aliliambia gazeti hili jana kuwa wanachokifanya ni kukemea ufisadi serikalini na kupinga uzembe kwa baadhi ya mawaziri.

“Mafisadi wanatishika na msimamo wetu, sisi hatuna mpango wa kukibomoa chama ila tunakisaidia kwa kuwasema hao wanaojificha humo na kujifanya wakereketwa wakuu,” alisema.

Wabunge hao watatu pamoja na wengine baadhi wa chama hicho wamekuwa mwiba mkali kwa mawaziri kutokana na kuzipinga bajeti zao.

Mfano Lugola hivi karibuni aliwashambulia wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), akitishia kuwataja baadhi yao na watendaji wanojihusisha na rushwa pamoja na biashara ya dawa za kulevya.

Filikunjombe na Mpina nao wamekuwa na msimamo wa kukataa kuunga mkono bajeti za serikali zinazokuwa hazina maslahi kwa wananchi.

Katika kikao hicho cha CCM, Kikwete aliwataka wabunge kuendelea kuisimamia serikali pale inapobidi, lakini akawasihi wafanye hivyo kwa staha bila kutumia maneno makali akitumia mfano “serikali imevaa miwani ya mbao” kauli aliyowahi kuitumia Filikunjombe hivi karibu akimaanisha si sikivu.

Chanzo chetu ndani ya kikao hicho kilieleza kuwa Mbunge wa Sikonge, Said Nkumba ndiye alikuwa mwiba mkali kwa kuwashambulia wabunge hao, akidai wamekuwa na tabia isiyokoma.

Nkumba ambaye si mara yake ya kwanza kuwashambulia wenzake hao, alipendekeza kuwa kama wanataka ni heri wakahamia CHADEMA kuliko kuendelea kuivua nguo Serikali ya CCM.

Chanzo: Tanzania Daima

SOMA ZIARA ATAKAYOIFANYA RAISI OBAMA WA MAREKANI KATIKA NCHI TATU ZA AFRICA IKIWEMO TANZANIA...!

president-barack-obama
Rais Barack Obama wa Marekani anatarajia kutembelea bara la Afrika mwezi ujao (Juni) ambapo atatembelea mataifa ya Senegal, Afrika kusini na Tanzania. 

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa Ikulu ya Rais nchini Marekani Jay Carney, raisi Obama amepangiwa kufanya ziara hiyo kati ya tarehe 28 mwezi Juni hadi tarehe 3 mwezi Julai ambako atakutana na viongozi wa serikali, biashara na wa mashirika ya kijamii kwa lengo la kuhimiza amani na ustawi wa bara Afrika.

Taarifa hiyo imefafanua kuwa Raisi huyo wa Marekani atasisitiza umuhimu wa uhusiano kati ya Marekani na nchi za Afrika ikiwemo kupanua ukuaji wa kiuchumi, uwekezaji na biashara pamoja na kuboresha asasi za kidemokrasia.

Mara ya mwisho kwa raisi Obama kutembelea nchi ya bara la Afrika ni mwaka 2009 alipozuru Ghana.

Tuesday, May 21, 2013

Prof Jay amejiunga na chadema mchana huu...!

BREAKING NEWS : Prof. Jay ajiunga CHADEMA

Msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, Joseph Haule (Prof. Jay) amejiunga rasmi leo na chama cha CHADEMA.
 
 




Hizo ni baadhi ya picha zikimuonesha Prof. Jay akipokea kadi ya CHADEMA na kujiunga rasmi na chama hicho au kuvaa gwanda kama wasemavyo wenyewe. — at Bungeni Dodoma.