Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, July 12, 2012

WAHAMIAJI HARAMU WAKAMATWA MKOANI KILIMANAJARO...!

Wahamiaji haramu kutoka nchini Ethiopia wamekamatwa na jeshi la polisi mkoani Kilimanajaro wakiwa wamejificha katika nyumba ya mfanya biashara moja wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro.
Kamanada wa polisi mkoani Kilimanjaro Robert Boaz amethibitisha kukamatwa kwa wahamiaji hao haramu katika kijiji cha Mbomai kata ya tarkea wilayani humo.
Alisema wahamiaji hao walikutwa wakiwa wamejifungia katika nyumba ya mfanyabisha Philemoni Mboyo almaarufu kwa jina la Mabula wakiwa safarini kuelea nchi Afka ya Kusini .
Aidha alisema kuwa pamoja na kukamtwa kwa wahamiaji hao haramu uchunguzi wakina unaendelea ili kubaini nyumba hiyo kama imekuwa ikihusika na kufanya biashara haramu ya kusafirisha binadamu na kwamba jeshi hilo linamsaka mfanyabishara huyo ili
Alisema kuwa ipo haja ya kufuatilia mtandao mzima wa wafanyabiashara hao wanao jushughulisha na biashara hiyo ili kukomesha tatizo hilo ambalo limekuwa kubwa mkoani Kilimanjaro.
Boaz alisema kumekuwa na wimbi kubwa la wahamiaji hao haramu nchi na kwamba jeshi la polisi mkoani Kilimanjaro limejizatiti kupambana na wimbi hilo kwa kutoa elimu kwa wananchi waishio katika maeneo ya mipaka ili kufahamu adhari za kuwalea watu hao majumbani mwao.

No comments:

Post a Comment