Akiwa
ndio mchezaji aliyesajiliwa kwa fedha ndefu kutoka nchini Tanzania,
Mbwana Ally Samatta anaishi ambayo ni mcheza soka wa kimataifa anastahili
kuishi.
Akiwa
ameuzwa kwa dola za kimarekani zaidi ya 100,000, kwenda TP Mazembe
kutoka Simba, Mbwana Samatta analipwa kiasi cha dola 5000 kwa mwezi
ambayo ni sawa na shilingi millioni 7.5 huku akichukua marupurupu ya
kutosha.
Mbwana
Samatta amekuwa akicheza na kuperfom kwa kiwango kikubwa katika kila
nafasi anayopata anapoichezea klabu yake na kwa kiwango alichoonyesha
kuna uwezekano mkubwa mkataba wake utaboreshwa zaidi na kuendelea kuvuna
mkwanja mrefu zaidi.
Kwa
sasa hivi Samatta amenunua gari la kisasa zaidi Chrysler Crossfire la
mwaka 2006 ambalo limemgharimu takribani millioni 50 za kibongo.
Ikiwa
Samatta ataendelea kucheza kiwango alichonacho sasa, basi ni dhahiri
tutaendelea kuona akiishi kwenye majumba ya kifahari huku akipush magari
ya gharama zaidi.
Chanzo: lukemusicfactory
No comments:
Post a Comment