Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, August 8, 2012

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi yabaini Wanafunzi wengine sita wa shule za secondary wasio na sifa ...!

Wanafunzi waliojiunga na masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu katika shule za Serikali na baadaye kubainika kuwa hawajui kusoma na kuandika kwa ufasaha wanaendelea na masomo yao.

Imeelezwa kuwa katika baadhi ya shule za sekondari kwa wilaya za Korogwe na Moshi Mjini imebaini wanafunzi hao kuendelea na shule licha ya walimu kuwachuja na kutoa taarifa sehemu husika kama walivyo elekezwa.



Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Sekondari Mawenzi, Domin Kweka amesema kwa mujibu wa vigezo vilivyotolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kubaini wanafunzi wanaofaulu kujiunga na sekondari, wasio na sifa jumla ya wanafunzi sita walibainika.

Kweka ameongeza kuwa wanafunzi hao wameshindwa kabisa kufanya vizuri katika mtihani waliopewa jambo ambalo limeonesha ulakini katika kujiunga kwao na masomo ya sekondari, japokuwa wanaendelea na shule hadi sasa.

Aidha ameongeza kuwa tatizo hilo hujitokeza kila mwaka kwa wanafunzi wanaojiunga na kidato cha kwanza na hadi sasa katika madarasa mbalimbali wapo wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika.

No comments:

Post a Comment