Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, September 29, 2012

HATIMAYE HK AREJEA HEWANI BAADA YA SAUTI YAKE KUTOKUSIKIKA KWA TAKRIBANI MWEZI MMOJA…!


Halima Kassim aka HK

Mwanadada mahiri katika tasnia ya habari upande utangazaji anayetangaza na kituo cha radio KILI FM kilichopo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro anayefahamika kwa jina la Halima Kassim aka HK amerejea ofisini baada ya sauti yake kutokusikika radioni kwa takribani mwezi mmoja. Ukimya huo umezua maswali mengi kwa wasikilizaji wa radio hiyo na kuwapa mashaka kuwa labda ameacha kazi kwenye kituo hicho cha radio.
Nilifanya juhudi za kumtafuta ili kufahamu ukweli kuhusu hayo ambayo yanazungumzwa na watu mitaani, nilifanikiwa kumpata na kumuuliza machache. Kwanza nilimchokoza kumuuliza eti wewe ndio Halima kassim wa radio KILI FM?  “kwanza alitabasamu kidogo na kunijibu haswaaa! mimi ndio Halima Kassim wa radio KILI FM lakini wengi hupenda kuniita HK” nilitaka kwanza kufahamu mengi kuhusu HK na familia yake na hichi ndicho alichonijibu “kwetu tumezaliwa watatu na wote ni wadada mimi ni mtoto wa pili katika familia ya Bw. na Bi. Kassim Lema, chakula ninachokipenda ni ugali na mboga za majani, kitu nisichokipenda kwenye maisha yangu ni kuumizwa akili au mtu kucheza na akili yangu, kitu kizuri ambacho kila nikikikumbuka huwa nafurahia sana ni siku nilipotangazwa kua Mtangazaji bora katika kituo changu cha radio (Radio KILI FM) na tukio baya ambalo sitaweza kulisahau ni siku nilipo faint na kuumia baada ya kuambiwa mama yangu amefariki dunia muda mfupi tu baada ya kuachana nae” Alinijibu HK.
Swali lililofuata ni hili hapa, nimesikia watu wengi wakizungumza mengi kuhusu wewe kutokusikika radioni kwa takribani mwazi mmoja sasa je ni nini kinaendelea kwa sasa kuhusu wewe na KILI FM radio?  “Namshukuru mwenyezi Mungu kwa uzima nilionao kiukweli mimi nilikuwa likizo na hivi leo ndio nimerejea ofisini muda si mrefu wasikilizaji wa KILI FM radio watanisikia hewani maana nimekuja kuwapa wasikilizaji kile ambacho walikikosa kwa takribani mwezi mzima, Pia nashukuru nilipata muda wa kupumzika ikiwa ni pamoja na kutembelea ndugu jamaa na marafiki sehemu mbalimbali kama Dar es salaam, Arusha na Machame kwa bibi” hayo ndio aliyoweza kunijibu HK.

Team nzima ya www.kingjofa.blogspot.com inakutakia kazi njema.

No comments:

Post a Comment