Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, October 21, 2012

WAISLAMU MNAOFANYA VURUGU SOMENI HAPA ...!

SERIKALI imetakiwa kuwa makini katika usajili wa Taasisi mbalimbali hususan zinazohusiana na masuala ya dini ikiwa ni pamoja na kufuatilia huduma za taasisi zilizosajiliwa nchini ili kudhibiti taasisi zinazojisajili tofauti na kazi wanazofanya.

Aidha, imetakiwa kuchunguza taasisi zote zinazofanya huduma na zile zisizosajiliwa wasifanye shughuli yoyote mpaka wasajiliwe huku wakidhibiti mapema taasisi au mtu ambaye ni hatari kwa nchi bila kusubiri hali kuwa mbaya kwani inasababisha kuota mizizi na kusababisha madhara kwa wasio na hatia.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tanzania Islamic Peace Foundation (TIPF), Shekhe Sadik Godigodi alipozungumzia vurugu zilizojitokeza hivi karibuni Dar es Salaam na Zanzibar huku akitaka polisi kuchukua hatua zaidi kwa kuhakikisha vurugu zenye mrengo wa kidini zinafika mwisho.

Alisema mara nyingi Serikali imekuwa ikielezwa kuhusu kundi la ‘Uamsho’ Zanzibar ambalo limesajiliwa kuwa linachochea vurugu ikiwa ni tofauti na walivyosajiliwa lakini imekuwa ikisita kuwafutia usajili wao lakini kwa matukio ya sasa iifike wakati kuwe na umakini zaidi kwenye usajili.

Alisema kwa kitendo cha Jumuiya hiyo kuhisi kiongozi wao amechukuliwa na Polisi na kufanya vurugu wameenda kinyume na dini ya Kiislamu inayotaka kuchunguza na kuwa na uhakika kabla ya kuanza kudai haki kama kweli unastahili, “Ukiangalia suala ya Shekhe Ponda amekuwa akisumbua serikali kwa muda mrefu na kujiamulia mambo huku akisababisha vurugu kwa kutumia taasisi ambayo haijasajiliwa lakini serikali imekuwa kimya bila kumchukulia hatua, suala lililofanya kuota mizizi na kujiongezea wafuasi kila kukicha,” alisisitiza.

Alitaka Serikali kutowapuuza watu au vikundi kama hivyo ambavyo vinatishia kuharibu uso wa nchi na kujenga chuki kwa jamii kwa mambo ambayo yanaweza kushughulikia bila kusababisha migongano au kuchoma moto makanisa.

Aliwapongeza Wakristo kwa utiifu na kuheshimu sheria kutokana na uzalendo walioonesha na kuwasihi kuendelea kuwa na moyo huku vyombo husika wakichukua sheria dhidi ya wahalifu kwani yeye hafikirii kuwa hawana uwezo wa kulipiza kisasi bali uvumilivu walionao ndio uliowafanya kutofanya hivyo.

---
via HabariLeo

Source: http://www.wavuti.com

No comments:

Post a Comment