Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, December 9, 2012

Mji wa Jowhar - Somalia wakombolewa...!

Nchini Somalia askari wa kikosi cha Umoja wa Afrika pamoja na wanajeshi wa Somalia wameuteka mji wa Jowhar kutoka wapiganaji wa Kiislamu, al Shabaab. Mkazi mmoja alisema wanajeshi hao waliingia bila ya pingamizi. Kupoteza mji wa Jowhar ni pigo kubwa kwa al-Shabaab.

Mji huo uko kilomita 90 kaskazini ya Mogadishu, kwenye barabara kuu ya Somalia inayounganisha majimbo ya kusini na kati. Pia uko katikati ya eneo la kilimo kikubwa cha nchi. Jowhar ilikuwa ikidhibitiwa na al-Shabaab tangu wanajeshi wa Ethiopia walipoondoka Somalia mwaka wa 2009.

Ulikuwa mmoja kati ya miji mikubwa iliyokuwa bado mikononi mwa al-Shabaab. Tangu mwaka 2011 al-Shabaab imepoteza makambi yake kadha.

Chanzo - BBC Swahili

No comments:

Post a Comment