Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, June 19, 2013

Kibanda azidi kufunguka, CHADEMA kikaangoni


Mnamkumbuka mhariri ABSALOM KIBANDA? AMBAE ALITEKWA NA KUTESWA?, amesema yafuatayo kuhusu wahusika ambao walimfanyia vitendo hivyo vya kinyama ambavyo vimempa ulemavu wa kudumu wa jicho lake. Nanukuu;
"Acha niliseme hili jamani pengine moyo wangu utatulia. Mmoja wa watu walio nishambulia ana fanana kwa sura na umbile la Ludovick Rwezaura yule kada wa CHADEMA aliyewekwa ndani na Lwakatare ambae nimemuona kupitia magazeti na mitandao ya kijamii. Nimeshangazwa sana mtu huyu yupo karibu na baadhi ya wahariri wenzangu na hata msaidizi wangu bwana Ansbert Ngurumo, bado napata shaka ni kuwa watu wana fanana au?"


 Ndugu Ludovick ambae kwa sasa bado yupo mahabusu, alikuwa ni mfanyakazi wa CHADEMA makao makuu, chini ya kurugenzi ya ULINZI na USALAMA kabla ya kukutwa na mkasa wake ambao ndio umemuweka rumande mpaka hivi sasa. Kuwepo kwa kijana huyu kwenye hii kurugenzi na maelezo ya bwana Kibanda nadhani wana-JF mnaweza ku-connect dots.
CHADEMA ukweli ni kwamba mwaka 2013 umekuwa mwaka 'tasa' kwenu, kwani mikakati mingi ya kichama imekuwa ikibuma na mbaya zaidi ni pale mpaka siri za ndani ya chama kuzagaa mitaani, haya yote ya kubuma na kuvuja kwa siri ovyo ovyo hivi, kuna sababishwa na 'uchanga' wenu katika kusimamia shughuli za kichama, mna safari ndefu sana.



Source: DIRA YA MTANZANIA.

No comments:

Post a Comment