Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, July 24, 2013

AFUMWA AKIFANYA NGONO MAKABURINI.....,

LICHA ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani watu wengi kuogopa kufanya maovu, jimama anayekwenda kwa jina la Joyce Benson (34), amefumwa akifanya ngono katika makaburi ya Malapa, Buguruni jijini Dar.







Joyce amekamatwa usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita saa nane katika maeneo hayo akifanya biashara haramu ya kuuza mwili wake katika makaburi hayo kwa njia ya kujipatia fedha.
 

Joyce mwenye umbile la miraba minne alipatwa na fedheha kubwa baada ya majirani zake kusikia habari hizo na kuanza kumlaani.

Mbali na Joyce pia siku hiyo machangudoa wengine 14, waliokuwa wakifanyia vitendo vya ukahaba kwenye makaburi hayo walikamatwa.

Joyce na wenzake hao walifikishwa katika Mahakama ya Jiji (Sokoine Drive) ili sheria ifuate mkondo wake.

Wakiwa mahakamani hapo, mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Richard Magodi aliwasomea tuhuma za kufanya ukahaba na kumfanya hakimu wa mahakama hiyo, Timoth Lyon kupigwa na butwaa.

Hata hivyo, Joyce na wenzake walikana kufanya kosa hilo ambapo hakimu, Lyon aliwaambia washitakiwa kuwa dhamana iko wazi kama watatimiza masharti.

Licha ya dhamana kuwa wazi, jimama huyo alijikuta akipandishwa kwenye karandinga na kupelekwa Gereza la Segerea baada ya kukosa mdhamini huku baadhi wakichomolewa na wadhamini wao.

No comments:

Post a Comment