Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, July 8, 2013

Lulu anyakua tuzo kwenye moja ya tamasha kubwa la filamu barani Africa.

 Elizabeth Michael maarufu kwenye bongomovie kama Lulu na maarufu kwenye mitandao ya kijamii kama hotlulumichael, hivi karibuni nyota yake imeendelea kung’aa tena kwenye tamasha kubwa la filamu africa. Kupitia category ya “Best Actress Swahili Movies” ambayo ilikuwa na ushindani mkubwa kutokana na uwepo wa wasanii wengi wa kike wanaofanya vizuri kwa sasa, lakini Elizabeth Michael a.k.a Lulu amenyakuwa tuzo hii kwenye tamasha la ZIFF ambalo ni maarufu na linahudhuriwa na wadau mbalimbali wa filamu kutoka sehemu tofauti duniani. Hivyo basi hii itakuwa ni fursa nyingine na nzuri kwa Lulu baaada ya wadau wa movie kumjua yeye na labda kufuatilia kazi zake kitu ambacho kinaweza kumsaidia kufika zaidi ya hapa alipo sasa kwa kupata kazi nyingine nje ya Tanzania. Lulu ameshinda tuzo hii kutokana na ushiriki wake kwenye movie ya Woman of principle. Movie hii iliandaliwa na kampuni ya RJ Company na kufanywa na Ray,Lulu na Nagris Mohamed kama washiriki wakuu.



No comments:

Post a Comment