Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, July 5, 2013

SI UNAJUA OBAMA HAKUPEWA ILE PHD NA OPEN UNV? HII NDIO HABARI MPYA KUHUSU PHD HIYO

Dar es Salaam. Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania (OUT), Profesa Tolly Mbwete amesema kuwa walichelewa kufanya mawasiliano na vyombo vinavyohusika ili kupata fursa ya kumkabidhi Rais wa Marekani, Barack Obama Shahada ya Heshima ya Uzamivu kama walivyokuwa wamepanga.

Profesa Mbwete akizungumza kwa njia ya simu alisema kuwa, ingawa Rais Obama ameondoka nchini bado wana njia mbili za kuweza kumkabidhi cheti ikiwa ni ishara ya kumtunuku shahada hiyo.

“Yule ni mtu mkubwa bwana ingetakiwa tufanye mawasiliano ya kupata nafasi kumkabidhi kwa miezi mitatu kabla, hata hivyo hiyo shahada kwa maana halisi tulishampa kwa sababu mkuu wa chuo ndiye mwenye mamlaka ya kuitoa, kilichokuwa kikisubiriwa ni kumkabidhi cheti tu na yeye atoe hotuba ya kuikubali,” alisema Profesa Mbwete.

Anasema kuwa, chuo hicho kitawasiliana na Ubalozi wa Marekani nchini ili kuona njia itakayotumiwa katika kumalizia mchakato huo.

“Kwa sasa kuna njia mbili za kumabidhi, sisi tunaweza kwenda ama tunaweza kukituma cheti hicho kupitia ubalozi na yeye akatuma hotuba yake,” alisema Profesa Mbwete.

No comments:

Post a Comment