Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, August 17, 2013

IFAHAMU SAFARI NA MAFANIKIO YA CASSIM MAARUFU KAMA BABI D'e Conscious

 Babi akiwa kwenye Fiesta Road show 2012.

Babi akisherehesha katika mahafali ya Green Bird College iliyopo katika Mwanga mkoani Kilimanjaro.

 Babi akisherehesha Miss Moshi 2013.

Babi akiwa na Luiza Nyoni Mbutu wa Twanga pepeta kabla ya Show ya Tigo Bonanza Dodoma

 Babi akiwa na Masanja Mkandamizaji wakisherehesha kwenye Miss kilimanjaro Launch part

 
 Babi akiwa anafanya Panone Road show.

 Babi akiwa katika studio za 96.5 Kibo fm Radio, akifanya kipindi.

 Babi akiwa na warembo wa Miss kilimanjaro 2013 wakifanya Tourkatika makampuni mbalimbali yaliyotoa udhamini.

Babi akiwa kwenye Tigo Bonanza katika viwanja vya CCP mjini Moshi.

 Babi akiwa kwenye Tusker Carnival Uwanja wa Ushirika.


Babi akiwa kwenye Vodacom Road show.
 
CASSIM ni mtoto kwanza kati ya watoto watatu wa Familia ya Mr. & Mrs. Shaaban Mwinyi. Mwaka 2001 alijiunga na Shule ya Sekondari Mawenzi iliyopo mjini Moshi. Baadae alijiunga na ufundi katika gereji ya Sawaya iliyopo majengo mjini Moshi kwa sasa inafahamika kama Kilimanjaro. 
 
Baada ya hapo alipata mafunzo ya Facilitation skills na kufanya kazi katika shirika la White Orange Youth kwa muda wa mwaka mmoja na mwaka 2006 alipata kazi katika shirika lingine liitwalo Child Health and Social Ecology aliajiriwa kwa mkataba wa mwaka mmoja kama Assistant Facilitator. 
 
Baada ya mkataba kuisha akapata nafasi ya kufanya katika mradi wa Family Health International katika mradi wa Ishi Campaign akiwa kama Youth Advisory Group Wakati akifanya kazi hiyo aliweza kufanya kazi ya muda katika shirika la Kikristo la YMCA kama Facilitator katika kitengo cha Education.
 
Mwaka 2008 alienda Nairobi katika Mafunzo ya East Africa Leadership and Citizenship Program akiwakilisha Tanzania, anakiri kuwa mafunzo aliyoyapata yalimfanya ajitambue kuwa ana uwezo binafsi na anaweza kufanya kitu chochote. Maana alifundishwa kujiamini na Kufanya kitu na sio kujaribu. Baada ya kumaliza mafunzo hayo mjini Nairobi alirudi Moshi na wazo la kutengeneza Film yenye kiwango cha juu ambapo kwa kipindi hicho film za Tanzania zilikua za kiwango cha chini sana ilibidi nitafute watu ambao wanaweza fanya kazi ndipo akawapata jamaa ambao waliweza kukubali wazo lake na kujitolea muda wao kuhakikisha kuwa Cassim anafikia lengo lake. 
 
Jamaa hao ni Julius Masaoe ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Phijema video Production, Benson Jackson ambaye ni Muandishi wa habari, Hamis Kitunga huyu ni kijana Mjasiriamali na Thomas Munuo huyu ni Director wa Viafrica. Hapo ndipo ikazaliwa Kampuni ya Africa Film. Baadae aliweza kuandika films nyingi za Kibongo na kuziuza film kama “Zawadi ya Birthday” ya JB, “My Heart” na nyingine nyingi. Pia Cassim anafanya kazi kwenye kituo cha radio kinachoitwa “Radio Kibo Fm” iliyopo mjini Moshi. 
 
Licha ya kufanya kazi kwenye kituo cha radio pia ni presenter kwenye matamasha mbalimbali na kati ya matamasha ambayo amewai kuyafanya ni kama Fiesta, Promotion mbalimbali, Matamasha ya Vodacom, Tigo, Airtel, event za TBL na hata za mashirika ya kijamii. NGO's. Mashindano ya Miss Kilimanjaro, Miss Utalii, Miss Simanjiro. Road Shows nyingi sana na mengine mengi sana. Mwishoni mwa mwezi wa nane atakua pale Tabora katika uwanja wa Ally Hasan Mwinyi kutakua na Bonge la Event litakalowashirikisha wasanii wa Bongo Movies na wasanii wa Muziki wa Bongo flavor. Pia nafundisha watu wanaopenda kuwa ma Presenter chini ya kampuni ya Somjo Dj's. 
 
 Nikapata fursa ya kumuuliza tofauti kati ya Presenter na MC? “Tofauti ya Presenter na Mc kwanza MC lazima uvae suti au suruali ya kitambaa halafu uchomekee ila Presenter unavaa hata kaptula ila swaga ndio zinahusika MC anafanya kitu uniform yaani MC wanafanya vitu vya kufanana kuanzia mavazi mpaka mpangilio wa matukio kitu ambacho kwa Presenter huwezi kukiona kabisa. 
 
Mfano ratiba za ma MC huwa hivi Kufungua kwa sala Utambulisho Kufungua shampeni, kukata Keki, kula Chakula, kutoa Zawadi, Nasaha kutoka kwa wazazi na Kufungua mziki yaani hiyo ndo ratiba yao labda vipengele vipishane cha juu kiwe chini cha chini kiwe juu ila hicho cha kwanza lazima kianze. 
 
Presenter huwa hawafanani swaga yani ukimkuta leo hapa kesho ni mwingine anaweza anza kwa kudondosha show au story ya kufurahisha. Yaani yeye anapewa anaambiwa kinachotakiwa kufanyika tu ila Presenter anafanya mpangilio wa shuhuli nzima. So mimi mtu akiniita MC sipendi kabisa japo njaa ikizidi nakula hata mifupa yaani nafanya hata u MC. 
 
Mfano Mahafali ya Green bird School na Green Bird College nafanyaga mimi ila huwa siwi MC nakuwa Presenter japo wananiita Mc ila wananiambiaga sifanani na ma MC huwa nacheka sana wanaposema hivyo najua hawajui kama Mimi ni zaidi ya MC. Kwa upande wa Changamoto ambazo anakutana nazo ni nyingi sana kwanza ni kwenye malipo malipo si makubwa sana kulingana na kazi na pia Vishawishi ukiwa si mgumu unaweza ukafa na ngoma (UKIMWI) maana watoto wazuri wanataka ku date na wewe sababu wanaona kuwa Presenter ni mtu maarufu na kila wasichana wengi wanapenda kuwa na watu maarufu. 
 
Wakati mwingine anakua barabarani akitangaza tamasha mfano la wanamiziki mtu anakuja anaomba tiketi ya free kutoka kwako bila kufikiri unafanya kazi ya watu na hauhusiki na ukimwambia ukweli anakwambia unaringa. Mafanikio aliyoyapata ni mengi kama kuwasomesha wadogo zake wawili, elimu ya sekondary, ameweza kujisomesha mwenyewe Uandishi wa Habari, anaishi kwake na ana maisha mazuri pina ana network kubwa sana ya kazi na makampuni mbalimbali na hata watu binafsi wanamuamini.
 
Kwa sasa anamiliki Movie Lab ambayo inaitwa “The Music Lab” ipo meneo ya Majengo mjini Moshi ambapo unaweza kupata Movies za aina zote Latest na Music ya aina zote kuna Mashine ya kuandika tishet na Jersey, Vikombe na hata ku print picha katika nguo. stiker, vifaa vya simu na muda si mrefu kutapatikana simu za bei rahisi kuanzia elfu kumi na kuendelea juu. Matarajio yake ya baadae ni kuwa na kampuni ya Marketing and Promotion na kuwa Presenter mwenye heshima kubwa sana Tanzania na nje ya Tanzania.
 
Ukitaka kumpata Cassim kwa ajili ya kazi piga simu +255717636358 utaweza kumuuliza chochote na atakupa majibu ya uhakika.

No comments:

Post a Comment