Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, August 9, 2013

MUME WA JOYCE KIRIA "HENRY KILEWO" AWALIZA WATU KWENYE MKUTANO WA HADHARA MABIBO - SAHARA

Leo akiwa anawahutubia wakazi wa mabibo-Sahara kwa mara ya kwanza toka atoke jela huko gereza la uyui- Tabora katika mkutano ambao mgeni rasmi alikua Mh. John Mnyika mbunge wa jimbo la Ubungo, Henry Kilewo aliwaliza baadhi ya wananchi waliofika katika mkutano huo. Hii kutokana na kuguswa na hotuba ya kamanda huyo wa chadema ambayo ilikua inaudhunisha kutokana na simulizi ya namna alivyokamatwa na kupelekwa jela na pia aliweza kutoa ushuhuda wa jinsi watu wengi wanyonge na maskini waliofungwa pasipo na hatia.

Kutoka kwenye chanzo cha habari hii alikiri kuwa kweli simulizi ile inasikitisha lakini bado alisisitiza kwa kusema "Hakuna dhambi kubwa hapa duniani kama uoga'" na  watatupiga kwa mabomu na watatu ua kwa risasi lakini na wao watakufa kwa presha ya dhambi.

No comments:

Post a Comment