Huku hali ya mshikemshike ikiendelea kushuhudiwa 
katika jengo la Westgate lenye maduka, ufyatulianaji risasi umesikika 
ndani ya jengo hilo lenye maduka na mikahawa zaidi ya themanini.
 
                     Milio hiyo ilidumu kwa dakika tatu na kufuatiwa 
na moshi mkubwa juu ya jengo hilo. Hakuna taarifa kamili kuhusu 
kilichosababisha moshi huo.
                     
Wapiganaji wa Al shabaab wamewateka 
nyara raia ambao idadi yao haijulikani. Walikuwemo ndani ya jengo 
wakiendelea na shughuli zao kuanzia Jumamosi mchana wakati wapiganaji wa
 Al shabaab walipowavamia na kuanza kufyatua risasi kiholela.
                     
Inaarifiwa kuna maiti kumi katika ghorofa ya kwanza ya jengo hilo.
Aidha wapiganaji hao wanaoaminika kuwa wanachama wa Al Shabaab ni kati ya kumi na kumi na watano na bado wangali ndani ya jengo hilo.
Ripoti zinasema kuwa ufyatulianaji mkubwa wa risasi pamoja na milipuko imesikika katika jengo hilo kwa takriban dakika 15.
Harakati za kuendelea kumaliza operesheni hiyo zinaendelea lakini hali ya mateka walio ndani ya jengo hilo inaendelea kudorora.
                     
Aidha wapiganaji hao wanaoaminika kuwa wanachama wa Al Shabaab ni kati ya kumi na kumi na watano na bado wangali ndani ya jengo hilo.
Ripoti zinasema kuwa ufyatulianaji mkubwa wa risasi pamoja na milipuko imesikika katika jengo hilo kwa takriban dakika 15.
Harakati za kuendelea kumaliza operesheni hiyo zinaendelea lakini hali ya mateka walio ndani ya jengo hilo inaendelea kudorora.
Wakenya waliofanikiwa kuondoka katika jengo la Westgate kwa usaidizi wa polisi
                     Rais Kenyatta amesema kuwa jeshi linajitahidi kuhakikisha kuwa linakabiliana vilivyo na wanamgambo hao.
                      
Helikopta za polisi zinazunguka juu ya jengo 
hilo pamoja na ndege za kijeshi kushika doria. Vikosi vya usalama 
vinaendelea na operesheni kujaribu kuwanusuru waathiriwa wakati hali 
ikiwa ni ya ati ati katika eneo la shambulizi.
                      
Awali jeshi la Kenya lilisema limeweza kudhibiti
 jengo hilo lote ingawa bado limetaja hali kuwa tete mno hasa katika 
kujaribu kuwaokoa mateka waliosalia ndani ya jengo hilo.
                      
Ripoti zinasema kuwa watu 69 wamefariki katika 
shambulizi hilo la Al Shabaab kufikia sasa huku 175 wakijeruhiwa. Baadhi
 wametibiwa na kuondoka hospitalini. Baadhi ya majeraha waliyopata ni 
majereha ya risasi na kutokana na guruneti ambalo Al shabaab 
waliwarushia wale waliokuwa ndani ya mikahawa siku ya Jumamosi.
                      
Kundi hilo limekiri kutekeleza shambulio hilo 
kutokana na hatua ya Kenya kupeleka majeshi yake nchini Somalia ili 
kukabiliana na wapiganaji hao.
Source: TheChoice Blog 
 
 
 
No comments:
Post a Comment