Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, April 14, 2014

TAZAMA YANGA ILIVYOWASILI MOSHI KUKABILIANA NA TIMU YA PANONE FC.

Leo majira ya saa nne na nusu Asubuhi ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro mashabiki mbalimbali wa Mpira wa miguu hususani Mashabiki na wanazi wa Timu kongwe ya mpira wa Miguu Daresalaam Yanga African Walikua katika barabara kuu ya Moshi Arusha kuipokea Timu ya Yanga.
Basi la Yanga likiwa nje ya kituo cha Mafuta cha Panone kilichopo weruweru nje kidogo ya Mji wa Moshi.

Timu ya Yanga ambayo inatarajia kushuka dimbani hapo kesho katika Mechi ya kirafiki dhidi ya Timu ya Panone Fc ambayo ni  Mabingwa wa Ligi Daraja la Tatu mkoa wa Kilimanjaro. Mchezo huo uliodhaminiwa na Panone and Co. Ltd. na Ngiloi Ulomi enterprises, huku wakishirikiana na wadau mbalimbali wa mpira wa Miguu mkoani Kilimanjaro ambao ni Ngorika bus Service, Kili Fm Radio, Kifaru oil, Malindi Night Club, Ibra Line, Marenga Investment co. Ltd na  Moshi fm Radio. Katika kufanikisha hilo Panone wamejiandaa kuhakikisha Historia ya Kimichezo inavunjwa kwani Yanga imewahi kucheza ndani ya Kilimanjaro Miaka 23 iliyopita.
Mchezaji wa Yanga Didie Kavumbagu akifurahia Mandhari ya Mji wa Moshi.

Tukizungumza na Kocha mkuu wa yanga  Hans Plujim kuhusiana na mchezo huo baada ya kuwasili mjini Moshi mkoani Kilimanjaro. Amesema anategemea kutumia Mchezo huo wa Kirafiki na timu ya Panone FC kama mchezo wa Maandalizi wa mechi yao ya mwisho dhidi ya timu ya Simba Sport Club. Akizungumzia kikosi atakachokichezesha amesema anategemea kuchezesha wachezaji ambao watacheza na Simba ndio maana amebeba wachezaji 21 kwa ajili ya mchezo huu.

Meneja wa Panone and Co. Ltd Gido Marandu akiwa na Kocha Mkuu wa Yanga Hans Plujim na Kocha Msaidizi ndugu Mkwasa Baada ya Kuwapokea Katika Kituo cha Mafuta Cha Panone Kilichopo Weruweru leo Asubuhi.

Akizungumza nasi Meneja wa Panone and Co. Ltd kwa kanda ya Kaskazini ndugu Gido marandu amesema Kampuni imejiandaa vizuri kuweza kuhakikisha kilakitu kinakwenda sawa na Timu ya Yanga imeshawasili. Hata hivyo alitaja Viingilio nitakua shilingi 10,000 kwa viti maalumu na 7,000 kwa viti maalumu B na shilingi 5,000 kwa Mzunguko. Kuhusu suala la Ulinzi alisema ulinzi uko wa Kutosha kutoka kwa Jeshi la Polisi na Kampuni ya ulinzi wenye Dhamana ya kuhakikisha ulinzi unakua hapo.

Alimaliza kwa kusema “Huu ni wasaa wa washabiki na wapenzi wa timu ya Yanga ndani ya mkoa wa kilimanjaro baada ya miaka mingi kukosa mchezo mkubwa ndani ya mkoa wetu na huu ndio mwanzo tu”

Mchezaji wa Yanga Mrisho Ngasa Akiwa ametulia katika Gari baada ya Kuwasili Moshi.

No comments:

Post a Comment