Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, October 30, 2014

Serikali mkoani Kilimanjaro imeagiza wakurugenzi watendaji wa halmashauri kutokupeleka fedha za miradi ya maendeleo kwenye ujenzi wa maabara

KILIMANJARO serikali Mkoani Kilimanjaro imetoa agizo kali kwa wakurugenzi watendaji  wa halmashauri za wilaya za mkoa huo, kutokubadilisha fedha za miradi ya maendeleo na kuzipeleka katika ujenzi wa maabara.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama , katika kikao cha kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC), ambapo aliwaonya wakurugenzi hao kutafuta njia mbadala za kujenga maabara na sio kutumia fedha za miradi ya maendeleo.

Amesema ujenzi wa maabara usizuie  shughuli zingine za miradi ya maendeleo kushindwa kukamilishwa  huku akisisitiza kuwa miradi yote inayotekelezwa katika halmashauri hizo ikiwemo, barabara, Maji, Afya na Kilimo ikamilishwe kwa wakati kam ambavyo imepangwa.

Aidha Gama amesema hata mvumilia Mkurugenzi atakaye bainika kuhamisha fedha za miradi ya maendeleo na kuzipeleka katika ujenzi wa maabara na badala yake aliwataka wakurugenzi hao kutafuta mbinu ambazo zitawawezesha kukamilisha maabara hizo kwa wakati.

Kwa upande wake Kaimu afisa elimu mkoa, Estomih Makyara amesema mkoa huo unakabiliwa na ukosefu wa maabara 333, ambazo hadi sasa hazijaanza kujengwa.

Amefafanua kuwa mkoa wa Kilimanjaro unajumla ya shule za sekondari za serikali 217, na kwamba maabara  zinazohitajika 651.

Aidha aliongeza kuwa maabara zilizopo ni 154,  sawa na aslimia 23.7, zinazoendelea kujengwa pamoja na umaliziaji wake ni maabara 169 sawa na asilimia 26.

No comments:

Post a Comment