Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, November 21, 2014

Wahamiaji haramu ambao ni raia wa Ethiopia wamekamatwa wakiwa wamejificha vichakani

KILIMANJARO raia wa  nne kutoka nchini Ethiopia wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro baada ya kukamatwa wakiwa wamejificha vichakani.

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro, Geofrey Kamwela, amethibitisha kukamatwa kwa raia hao na kwamba walikamatwa  tarehe 19 Novemba mwaka 2014, majira ya saa moja asubuhi katika kijiji cha Kileo wilayani mwanga.

Kamanda Kamwela alisema raia hao  walikamatwa  wakiwa katika vichaka vya kijiji hicho wakihangaika kutafuta njia ya kupita.

Kamwela alisema katika upekuzi uliofanywa kwa raia hao hawakukutwa na  chochote wala nyaraka za kusafiria walikuwa hawana.

Alisema raia hao wametokea nchini Kenya na kuingia nchini kwa kutumia njia za panya na kwamba walikuwa wakipita  kuelekea nchini Afrika Kusini.

Kamanda aliwataja wahamiaji hao kuwa ni Tamru Haile(20) Adinal Samwel (17) Tekele Gebure (17)  na Solomon Adise (18) ambapo waliingia nchini kinyume cha sheria.

Alisema kukamatwa kwa raia hao kumetokana  na wananchi waliowaona na kuwatilia mashaka na kutoa taarifa kwa askari.

No comments:

Post a Comment