Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, November 21, 2014

Wananchi watakiwa kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura

KILIMANJARO wananchi katika manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro wametakiwa kujitokeza kwenye zoezi  la uandikishaji wa  wapiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Disemba 14 mwaka huu.

Wito huo ulitolewa jana na Msimamizi mkuu wa uchaguzi katika Manispaa ya Moshi, Shaaban Ntarambe, wakati akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake mjini Moshi.

Alisema wakazi wote katika manispaa ya Moshi wanawajibu wa kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi la kujiandikisha kupiga kura kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ili kuweza kutimiza haki ya kikatiba ya kupiga kura na kuchagua viongozi wanaofaa.

Aidha alisema zoezi la uandikishaji wapiga kura linatarajiwa kuanza Novemba 23 mwaka huu na kumalizika Novemaba 29 mwaka huu na kwamba vituo vitafunguliwa saa 1:30 na kufungwa saa 10:00 jioni.

Aliongeza kuwa zaidi ya vituo 102 vitatumika katika zoezi hilo kwenye kata zote 21 na mitaa yote katika manispaa ya Moshi na kwamba halmashauri hiyo imejipanga vizuri kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa.

Katika hatua nyingine Ntarambe alisema ulinzi wa wananchi umeimarishwa katika vituo hivyo na kwamba wananchi wasiogope kujitokeza kwa kuhofia hali ya ulinzi na usalama wao.

No comments:

Post a Comment