Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, November 19, 2014

Watu 16 wafikishwa mahakamana kwa kosa la kuchoma moto mali za muwekezaji

 
KILIMANJARO watu 16 ambao ni wakazi wa kijiji cha miti mirefu na Sanya  Juu Wilayani Siha Mkoani Kilimanjaro, wamefishikishwa katika mahakama ya wilaya ya Hai kwa makosa matatu ya  kuvamia shamba la Mwekezaji wa kampuni ya Tanganyika Film and Safari Tawi  la Ndarakwai  na kuchoma mali mbalimbali  zenye zaidi ya thamani ya shilingi  bilioni  1.7

Akisoma hati ya mashtaka mahakamani hapo mwendesha mashtaka Roymax Membe,  mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo Denis Mpelembwa, amesema kuwa watuhumiwa hao wote kwa pamoja walitenda  makosa hayo  kwa kuvamia shamba la Ndarakwai linalomikiwa na mwekezaji Peter Jones  mnamo Novemba  14   mwaka huu.

Alisema kuwa watuhumiwa hao walitenda kosa la kwanza  la kuingia ndani ya shamba la Ndarakwai na kuchoma magari 6 ya kambi ya utalii ya Ndarakwai  yenye thamani ya shilingi  milioni 450  ambapo ni kinyume na makaosa ya jinai  kifungu cha 299 ya makosa ya jinai ya mwaka 2002.

Amesema watu hao pia walitenda kosa la pili  la kuharibu mali kwa makusudi za mwekezaji huyo,  zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1   ambapo kosa la tatu watuhumiwa hao walichoma mali za mwekezaji huyo zenye thamani ya shilingi milioni 210  kinyume na kifungu cha 326 (i) ya makosa ya jinai ya mwaka 2002.

Membe aliwataja watuhumiwa hao ambao wamefikishwa katika mahaka hiyo kuwa ni Matey Hilita (42), Julias Daudi (45), Elipokea Sefano (42), Andrea Elias (67), Alex filipo (30),  Victor Joakimu (32), Dicksoni Mallya (38), wote wakazi wa kijiji cha Miti Mirefu.

Wengine waliofikishwa mahamakani ni Dicksoni Kweka (62), Emanueli Isaya (17), wakazi wa Sanya Juu, Erick Wilsoni (27), Rael Paulo (26), Bibiana Charles (36), Hellen stepahano (39), Hellen Daudi (26), na Monika Rongai (42) wote wakazi wa kijiji cha Miti Mirefu.

Hata hivyo mwendesha mashtaka huyo aliieleza mahakama hiyo kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakalika na kuiomba mahakama kutowapa dhamana watuhumiwa hao kutokana  na thamanani halisi ya vitu vilivyoharibu bado haijajulikana.

Hata hivyo  watumuhiwa wote wamekana mashtaka hayo, na  hakimu Mpelembwa alikubali ombi la mwendesha mashtaka huyo na  kutoa siku saba awakilishe thamani halisi ya uharibifu huo na kesi imeairishwa hadi tarehe 2 Desemba mwaka huu itakapotajwa tena.

No comments:

Post a Comment