Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, June 1, 2015

HOTEL YA DOUBLETREE BY HILTON YA JIJINI DAR YAFANYA USAFI WA MAZINGIRA YANAYOIZUNGUKA HOTEL HIYO


Mkurugenzi mkuu wa Hotel ya Double Tree by Hilton nchini Tanzania, Bw.Ian Mclachan (wa pili kutoka kushoto) akifanya usafi katika ufukwe wa Bahari inayoizunguka Hoteli ya Double Tree huku akishirikiana bega kwa bega na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara wa Hoteli ya Double Tree By Hilton, Bw. Yehia Elmansoury (wa kwanza kushoto).
Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Double Tree by Hilton, Bw. Florenso Kirambata(kushoto) akifanya usafi wa mazingira katika fukwe inayoizunguka hoteli hiyo ya jijini Dar es Salaam huku akiwa pamoja na mmoja wa wafanyakazi wa hoteli hiyo.
Baadhi ya uchafu uliokuwa katoka fukwe ya Bahari inayoizunguka Hoteli ya Double Tree by Hilton ya jijini Dar.
Wafanyakazi wa hoteli ya Double Tree ya jijini Dar es Salaam wakifanya usafi maeneo yote yanayoizunguka hoteli hiyo.
Wafanyakazi wa hoteli ya Double Tree ya jijini Dar es Salaam wakiongozwa na Mkurugenzi mkuu wa Hotel ya Double Tree by Hilton nchini Tanzania, Bw.Ian Mclachan (wa kwanza kulia) wakiwa na mifuko ya uchafu katika picha ya pamoja mara tu ya kumalizika kwa usafi uliofanyika kwenye fukwe zinazoizunguka Hotel hiyo.
Wafanyakazi wakiweka uchafu kwenye gari la kubebea taka mara baada ya kumaliza kufanya usafi
Viongozi na wafanyakazi wa Hoteli ya Double Tree by Hilton ya jijini Dar es Salaam wakiwa kwenye picha ya pamoja nje ya Hotel hiyo mara baada ya kumaliza kufanya usafi.


Na Geofrey Adroph

No comments:

Post a Comment