Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, July 13, 2015

Waendesha bodaboda kujengewa kituo maalumu kitakacho gharimu zaidi ya milioni 10

Katika kuwajengea waendesha bodaboda  pamoja na abiria wao mazingira bora na salama, mamlaka ya usafiri wa majini na nchi kavu Sumatra, imeanza kujenga kituo maalumu cha mfano  kitakacho gharimu zaidi ya shilingi milioni kumi za Tanzania, kwaajili ya waendesha bodaboda wa manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro .lengo likiwa ni kujenga vituo  zaidi ya 100 mkoani Kilimanjaro  

Kaimu afisa mfawidhi wa Sumatra mkoani Kilimanjaro Bwana Thadei Mwita, amesema hayo wakati wa ziara ya mkuu wa wilaya  ya Moshi Novatus Makunga, alipotembelea eneo la stand  kuu ya mabasi yaendayo mikoani panapojengwa  kituo cha mfano, cha waendesha bodaboda wa manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Nae Katibu wa waendesha bodaboda mkoani Kilimanjaro Rashidi Omari, amesema ujenzi wa kituo hicho umekuja  baada ya umoja wa waendesha bodaboda, kuomba serikali iwajengee, na kwamba kitasaidia kuwawezesha kutambuana hali itakayoepusha vitendo vya wizi kupitia mwavuli wa waendesha bodaboda.

Akizungumza mara baada ya kutembelea eneo hilo,  mkuu wa wilaya ya Moshi Novatus Makunga, amesema serikali ya mkoa wa Kilimanjaro imetenga maeneo ya kujenga vituo 100, na kwamba anawaomba wadau wa  maendeleo kuchangia ujenzi wa vituo hivyo ili kuwapatia waendeasha bodaboda ajira endelevu.

No comments:

Post a Comment