Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, June 4, 2026

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ATUNUKIWA SHAHADA KUTOKA RUDN UNIVERSITY - URUSI





Na Beda Msimbe,TBN, Moscow

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) huku akiitoa shahada hiyo kwa Watanzania.

Shahada hiyo ilitolewa na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni,2026.

Rais Mhe. Dk Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania,

pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii,

Akizungumza baada ya kupewa shahada hiyo Rais Samia alisema kwamba heshima aliyopewa si ya mafanikio yake binafsi bali ni utambuzi wa juhudi na matarajio ya watanzania wote.

Alisema shahada hiyo ni ishara ya utambuzi wa dhamira ya pamoja ya Watanzania wote katika kuleta maendeleo,ushirikiano na ustawi wa binadamu.

“Nilipokea kwa furaha habari za kutunukiwa heshima hii,lakini mara moja nikatambua kwamba si yangu peke yangu. Ni heshima inayoitambua dhamira yetu ya pamoja ya maendeleo, ushirikiano na maendeleo ya binadamu” alisema Dk Samia.

Hii ni shahada yake ya nane kutolewa kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha alisema shahada hiyo  aliyopewa leo ni ishara ya urafiki wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi ikiwa ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya elimu katika kuunganisha mataifa.

Aidha alisema heshima hiyo inaakisi uhusiano wa kudumu kati ya nchi za Tanzania na Urusi ambazo zimeendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali hususani elimu kwa miongo kadhaa sasa.

Katika hotuba yake ambayo viongozi wa watanzania waliopo  Urusi na vyuo vya Urusi walisema ni iluiyiojaa mamlaka makubwa, Rais Samia alisema kwa miaka mingi watanzania walikuwa wanapata elimu inayochangia maendeleo  ya Tanzania katika Nyanja mbalimbali jambo ambalo pia  limeimarisha mahusiano ya watu wa pande zote mbili,

“Mama amezungumza nchi yetuj ina sifa sana. Tena sifa njema kwa kupata mwaliko wa Rais Vladmir Putin kuja hapoa ni kutambulika kwa Tanzania ni ishara njema na hotuba ya mama imeakisi matarajio” alisema Jefrey Mashauri Mwenyekiti wa wanafunzi wa Tanzania shirikishoi la Urusi (TASCARU).

Naye Mwenyekit wa watanznaia wanaoishi Urusi Pascal Gura alisema watanzania 300 wanaosihi hapo wameona fahari kubwa kukutana na kumsikiliza Rais Samia akionesha ni kwa namna gani kama Taifa Tanzania linaendelea kuwika.

Rais Samia katika hotuba yake alionesha jinsi Tanzania inavyoweza kufanikisha mambo wanaposaidiana na kushirikiana kwa maendeleo ya taifa.

Pia alikumbusha vijana kujipatia elimu huku wakizingatia kauli ya baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere ambaye alifundisha kwamba maendeleo lazima daima yaweke mwanadamu katikati ya kila jambo.

Aidha alitaka vijana kuangalia taifa lao na kwamba dokumentari iliyooneshwa kabla ya kutunukiwa shahada kuhusu maendeleo ya Tanzania inawaonesha dhamira ya watanzania na ni muhumu kwao watambue umuhimu wao kwa taifa huku huku wakiyaakisi maneno ya baba wa taifa katika utumishi wao.

Tangu kuanzishwa kwa chuo hicho miaka ya 1960 watanzania 1,100 wamepata utaalamu mbalimbali kupitia hucho hicho.Idadi hiyo ni kati ya wanafunzi 5000 ambao wamepata taaluma zao nchini Urusi katika Nyanja mbalimbali ikiwamo udaktari uhandisi na wataalamu wa sayansi.

Rais katika hotuba yake pia alizungumzia makubaliano kadhaa yaliyotiwa saini  yenye lengo la kuleta ushirikiano wa aina yake katika utafiti na elimu na ufundishaji.







TANZANIA NA URUSI ZIPO KATIKA HATUA ZA MWISHO MAKUBALIANO KUHUSU MATUMIZI YA FEDHA


 Na muandishi wa TBN, Urusi.    

 Tanzania na Urusi zipo katika hatua za mwisho za majadiliano za matumizi ya fedha za malipo kwa lengo la kuimarisha biashara baina yao.      

  Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo kwenye mahojiano na waandishi wa habari waliopo katika msafara wa ziara ya kitaifa ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Urusi.      

 Alisema mataifa hayo mawili yatasaini hati za makubaliano kabla kumalizika kwa ziara.                

Alisema kuna urari wa biashara wa Dola za Marekani milioni 200 hivyo hatua hiyo ya kufikia makubaliano itafungua njia ya ushirikiano kwenye ufanisi katika masuala ya uwekezaji na biashara.                  

Alifafanua kuwa makubaliano hayo yatahusisha matumizi ya shilingi ya kitanzania.                        

Alisema Urusi ambayo ikishiriki katika ukombozi wa kisiasa sasa inakuja kusaidia ukombozi wa kiuchumi na iko mbele katika kilimo uchakataji na uzalishaji, mbegu bora, madini itakuwa msaada mkubwa katika utekelezaji dira ya maendeleo 2025 ambayo itaanza kitumika Julai mwaka huu.      

  Profesa Mkumbo alisema kuna manufaa makubwa katika ziara hiyo ni kuwezesha Ujenzi wa Reli ya Kusini kupitia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP). 

Aidha alisema ili kurahisisha mawasiliano katika utalii, Tanzania na Urusi zipo katika hatua ya mwisho ya kuingia makubaliano yatakayowezesha Shirika la Ndege la Tanzania kufanya safari za moja kwa moja kutoka Dar es Salaam hadi Moscow.

Wednesday, June 3, 2026

URUSI KUFUNGUA FURSA LUKUKI TANZANIA

 

Na muandishi wa TBN, Urusi.                 

 Urusi imesema taifa hilo litafungua fursa lukuki kwa taifa la Tanzania kwa manufaa ya pande zote mbili.

Aidha taifa hilo lenye miradi 70 yenye thamani ya dola za Marekani milioni434.22 ikiwa imewezesha ajira 3018 tanzania limesema kuwa litatangaza fursa hizo katika mkutano wa uchumi wa kimataifa kesho kutwa.             Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kikao chake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kiongozi wa Urusi Vladimir Putin amesema Urusi imekuwa ikifuatilia kwa makini mageuzi yanayofanyika nchini tanzania na wanaona inavyokua.        Amesema amekuwa na mazungumzo yenye manufaa makubwa kwa jamii ya pande zote mbili na kuahidi kuendelea na ushirikiano na Tanzania.        Naye rais Samia amesema kuwa ziara yake katika Shirikisho la Urusi ina umuhimu mkubwa wa kihistoria kwake binafsi na kwa taifa la Tanzania kwa ujumla. 

“Ziara yangu ina umuhimu wa pekee wa kihistoria kwangu binafsi na kwa nchi yangu. Imepita zaidi ya nusu karne tangu kufanyika kwa ziara ya mwisho ya kiserikali ya Tanzania nchini Urusi. Hivyo, kwangu hii ni safari ya kihistoria sana kuja Urusi kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa pande mbili, pamoja na maendeleo endelevu kwa wananchi wetu. Kwa niaba yangu na wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa mwaliko huu,” alisema Rais Samia.

Aidha, Rais Samia alikumbusha mchango mkubwa wa Urusi katika harakati za Tanzania za kupigania uhuru na kumpongeza Rais Putin kwa maadhimisho ya miaka 81 ya Ushindi katika Vita Kuu ya Pili ya Dunia yaliyofanyika Mei 9 mwaka huu.

Rais Samia aliwasili Moscow kwa ziara yake ya kwanza nchini Urusi, ambayo pia ni ziara ya kwanza ya kiongozi wa Tanzania nchini humo katika kipindi cha zaidi ya miaka 50, kwa ajili ya mazungumzo na Rais Putin.

Viongozi hao kwa mujibu wao walijadili masuala mbalimbali yanayohusu kuimarisha zaidi uhusiano wa kirafiki na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili. Vilevile, walibadilishana mawazo kuhusu masuala muhimu yanayohusu ajenda za kimataifa na kikanda.

Mwisho.

RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AWEKA SHADA KWENYE KABURI LA ASKARI ASIYEFAHAMIKA


 Na mwandishi wa TBN, Urusi

KENGELE kubwa iliyogongwa mara tisa, bendi ya jeshi ikiongoza nyimbo za maombolezo Rais Dk Samia Suluhu Hasan majira ya saa tano na dakika 23 aliweka shada la maua kwa kaburi la askari asiyefahamika, mjini hapa.

Aidha Baada ya shughuli la uwekaji wa taji hilo katika eneo ambalo moto huwaka daima ikiwa ni kumbukumbu ya wapiganaji wa Urusi waliopoteza maisha katika vita kuu ya pili, gadi tatu zilipita kwa mwendo wa haraka na kutoa heshima kwa Rais Samia baada ya kupigwa kwa wimbo wa taifa la Tanzania.

Hali ya  askari katika uwanja huo walioonesha nidhamu ya hali ya juu ya kusimama tisti katika maeneo yao bila kutikisika , ubadilishanaji wa gadi za ulinzi na pia mwendo wa pole ambao ulimsindikiza Rais Samia kwenda kwenye tukio la uwekeaji wa shahada. Vilikuwa vitu vinavyovutia kuangalia.

Rais Samia ambaye yupo katika ziara ya kiserikali nchini hapa  baadaye alienda kukutana na mwenyeji wake Rais Vladmir Putin.

Zaidi ya maofisa 300 wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ wamepata nafasi ya masomo katika nchi ya Urusi kwa ajili ya shahada ya kwanza na ya pili.

Askari hao wameenda kujifunza masuala ya kupambana na ugaidi, sayansi na teknolojia,mafunzo ya kijeshi, ulinzi wa amani, ununuzi na uhifadhi wa silaha,namna ya kukabiliana na majanga.

Tanzania na Urusi zina ushirikiano wa kijeshi kwa kuzingatia makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi yaliyosainiwa mwaka 2016  na makubaliano ya mwaka 2018 ya ushirikiano wa kifundi wa kijeshi.

Tanzania yenye ukuaji wa uchumi wa asilimia 5.5 kwa mwaka 2024 na ikikadiriwa kufikia asilimia 6 mwaka huu na ikiwa na mkakati wa kuhakikisha kwamba Dira ya maendeleo ya mwaka2050 inatekelezwa ziara ya Rais Samia nchini Urusi inatarajiwa kuzaa matunda yanayotarajiwa  ya kuinua sekta ya ajira kukuza biashara na kuimarisha uwekezaji.

Mwisho

RAIS WA JA.HURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ANATARAJIWA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU NA CHUO KIKUU CHA RUDIN NCHINI URUSI

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye yupo hapa shirikisho la Urusi kwa ziara ya kitaifa anatarajiwa kutunukiwa shahada ya uzamivu na Chuo Kikuu cha Rudin nchini hapa.

Tuzo hiyo inatokana na kutambua kazi yake na mchango wake katika jami ya Tanzania na dunia katika masuala ya msingi yanayohusu Maisha ya binadamu.

Chuo cha RUDIN chenye wanafunzi wa kitanzania 570 kufikia mwaka 2025 katika miaka zaidi ya 65 ya RUDIN, watanzania 1,132 wamepitia chuo hicho.

RUDIN kimesomesha zaidi ya wataalamu 200,000 duniani na sasa ina watu 44,000 kutoka nchi 160 duniani. Chuo hiki ni cha 367 kwa ubora duniani kwa mujibu wa QS World University Ranking ya mwaka 2025.

Rais Dkt Samia ambaye amepokelewa jana na Waziri wa maendeleo ya Uchumi wa Russia Maxim Reshetnikov anatarajiwa kukutana na mwenyeji wake Rais Vladimir Putin na kufanya mazungumzo ya ana kwa ana kwa ajili ya kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi.

Aidha akiwa nchini hapa, akiwa kiongozi wa pili wa Tanzania kutembelea Urusi, ziara ya kwanza ikiwa imefanywa na baba wa taifa Mwalimu Julius Nyerere, atashiriki Jukwaa la uchumi la St Petersburg ambapo tanzania itanadi fursa za uwekezaji, na diplomasia ya Uchumi kwa viongozi, wawekezaji na watunga sera wa kimataifa.

Katika kufanikisha dira ya Maendeleo 2050 ziara hii ni kikolezo cha utekelezaji kwa mafanikio ya dira hiyo ambayo inahitaji raslimali watu wenye utaalamu na upeo mkubwa kusimamia na kuendesha miradi ya kimkakati itakayopelekea ajira, viwanda na biashara zitakazoingiza dola trilioni moja na kuwa katika uchumi wa kati wa juu.

Katika WhatsApp yake Rais Samia amesema Ziara hiyo ni muhimu hasa taifa linapoelekea kuanza utekelezaji wa Dira ya Taifa 2050 ambayo inataka ushiriki mkubwa wa sekta binafsi. "Tutafanya mazungumzo na wenyeji wetu yanayolenga kuimarisha ushirikiano katika sekta za kimkakati zinazogusa maisha ya wananchi." 

"Aidha, tutashiriki majukwaa ya biashara na uwekezaji na kutatangaza fursa zilizopo nchini, pamoja na kufungua zaidi fursa za masoko kwa bidhaa za Tanzania nchini Urusi."

Mwisho

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AMEWASILI JIJINI MOSCOW KWAAJILI YA YA ZIARA YA KITAIFA NCHINI URUSI





 Na Beda Msimbe, TBN, Moscow

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Vnukovo, uliopo Jijini Moscow kwa ajili ya Ziara ya Kitaifa, nchini Urusi

Katika ziara hii ya kihistoria ikifanywa kwa mara ya pili katika historia ya uhusiano wa Tanzania na Urusi, ya kwanza ilikuwa ni miaka ya 1960 iliyofanywa na baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, Rais Samia anaendeleza kampeni kubwa ya kuhakikisha Tanzania inanufaika pia kiuchumi na uhusiano mzuri na mataifa mbalimbali

 Kwa mujibu wa shughuli atakazofanya Rais Samia akiwa hapa nchini kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia, kisiasa, kiuchumi na kihistoria baina ya Tanzania na Urusi,Rais amekuja kuiweka Tanzania katika ramani ya uwekezaji kwa ushiriki wake katika mkutano mkubwa wa uwekezaji jijini St Petersburg na pia kuona namna ya kutengeneza raslimali watu ambayo taifa inahitaji sana katika kufanikisha utekelezaji wa dira ya maendeleo ya 2050. 

Alipowasili nchini hapa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Vnukovo, Jijini Moscow  majira ya saa mbili na dakika 25 usiku , japo jua bado lilikuwa linawaka,  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokea heshima ya wimbo wa Taifa pamoja na gwaride.

Rais Samia alipokewa uwanjani na Waziri wa Maendeleo ya Uchumi wa Shirikisho la Urusi Mhe. Maxim Reshetnikov. 

Kwa mujibu wa ratiba leo asubuhi ataanza na kuweka shada ka maua kwa kaburila askari asiyejulikana kabla ya kwenda Ikuku ya Kremlin kwa mazungumzo na Rais Vladmir Putin.

mwisho

Friday, May 29, 2026

MIAKA 18 BAADAYE: JK AKUTANA TENA NA CATHERINE, BINTI ALIYEFANYIWA UPASUAJI WA MOYO AKIWA NA MIAKA MINNE


Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo Mei 29, 2026 amekutana tena na Bi. Catherine P. Conrad Minja, aliyefanyiwa upasuaji wa moyo kwa mafanikio akiwa na umri wa miaka minne katika taasisi ya  Muhimbili Orthopaedic Institute  (MOI) miaka 18 iliyopita.

Wakati huo madaktari bingwa wa Moyo wa Taasisi ya Moyo ya JKCI walikuwa wakitumia majengo ya MOI kabla jengo lao halijakamilika.

Mara ya kwanza wawili hao walikutana Novemba 14, 2008 wakati Dkt. Kikwete akiwa Rais alipokwenda kumjulia hali Catherine  hapo MOI baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo mapema wiki hiyo. Wakati huo Catherine alikuwa mmoja wa wagonjwa wa mwanzo kufanyiwa upasuaji huo katika taasisi hiyo.

Miaka 18 baadaye, Catherine amekua na sasa ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa Shahada ya Udaktari katika Chuo Kikuu cha Kairuki  jijini Dar es salaam.

Alifika ofisini kwa Rais Mstaafu kumsabahi na kumshukuru kwa mchango wake katika kuanzisha na kuimarisha huduma za matibabu ya magonjwa ya moyo nchini.

Dkt. Kikwete alimpongeza Catherine kwa kutimiza ndoto yake ya kusomea udaktari, jambo ambalo aliahidi kulifanya alipokuwa mtoto. Alisema amefurahishwa kumuona akiwa mwenye afya njema na akijiandaa kulitumikia taifa kupitia taaluma ya tiba.

Kwa upande wake, Catherine alisema anatamani kuwa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo ili kuwasaidia wagonjwa wenye changamoto kama aliyowahi kupitia yeye mwenyewe, akieleza kuwa hiyo itakuwa ni moja ya njia ya kumshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha na afya njema.