Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, June 6, 2026

PUTIN AIKUBALI TANZANIAtin NA KUELEZEA JINSI ILIVYO MUHIMU

 


Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg

Rais Vladimir Putin wa Urusi amesema Tanzania ni lango kuu la kimkakati linalounganisha soko la Afrika Mashariki na masoko ya kimataifa.

Aidha amesema katika uchumi wa dunia unaozidi kubadilika kuelekea mifumo ya nguzo nyingi za kiuchumi, taifa la Tanzania umuhimu  mkubwa katika kuyfanikisha ustawi wa jamii mbalimbalio. 

Akizungumza Juni 5 katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg la mwaka 2026 Rais Putin amesema kuwa Tanzania katika utendaji ni taifa la kimkakati  katika ukanda wa Afrika Mashariki unaofanana na ule wa nchi ya Uzbekistan katika ukanda wa Asia ya Kati ikifanya kazi kama kiungo muhimu sana kati ya uchumi wa kikanda na vituo vikuu vya biashara ya kimataifa duniani. 

Kiongozi huyo amebainisha hayo wakati akizungumzia mataifa ambayo kutokana na nafasi zao za kijiografia na mahusiano yao ya kiuchumi yanageuka kuwa madaraja muhimu kati ya kanda tofauti duniani na kuongeza kuwa mataifa yenye uwezo wa kuoanisha maendeleo yao ya ndani na miunganisho madhubuti kwenye vituo vipya vya ukuaji wa uchumi wa kimataifa yanazidi kuwa muhimu wakati mifumo ya biashara ya kimataifa inavyoendelea kubadilika.

Kauli hizi nzito kutoka kwa Rais Putin zinakuja wakati ambao Tanzania inaendelea kupanua kwa kasi miundombinu yake ya usafirishaji ikiwemo bandari na njia za biashara za kikanda ili kuimarisha nafasi yake kama kitovu kikuu cha biashara kwa ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Kati na hivyo kutafsiri kwa vitendo malengo makubwa ya ukuaji wa kiuchumi.

Rais Samia Suluhu Hassana alishiriki katika jukwaa hilo amnbapo alipata nafasi ya kuelezea mambo mbalimbali yanayohusiana na uwekezaji na pia biashara.

Aidha alisema kwamba Tanzania ipo tayari kushirikiana na mataifa yoyote ikiwamo Russia ili kupeleka fursa mbalimbali za maendeleo kwa wananchi wake. Akijibu swali kwamba Russia ina vikwazo, Rais Samia alisema Tanzania haina vikwazo inafanyakazi na washirika wote wanaoitakia mema nchi yake.

mwisho

RAIS SAMIA AWASILI NCHINI AKITOKEA ZIARA YA MAFANIKIO URUSI

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Makamu wa Rais Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi pamoja na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tarehe 06 Juni, 2026 baada ya kuhitimisha Ziara yake ya Kitaifa, St. Petersburg nchini Urusi tarehe 05 Juni, 2026 kufuatia mwaliko wa Rais wa Nchi hiyo Mhe. Vladmir Putin.







Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere tarehe 06 Juni, 2026 baada ya kuhitimisha Ziara yake ya Kitaifa, St. Petersburg nchini Urusi tarehe 05 Juni, 2026

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ATANGAZA UTALII ALIPANIA SOKO LA URUSI

 

Na Beda Msimbe,TBN, Petersburg, Urusi

Ushirikiano wa miaka 65 ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi sasa unatafsiriwa kuwa daraja imara la maendeleo ya kiuchumi na kijamii, huku sekta ya utalii ikichukua mwelekeo mpya wa kimkakati kuvutia masoko ya kimataifa likiwemo la Urusi. 

Alisema anatambua soko la Urusi ni kubwa naTanzania ipo tayari kulihudumia kwa kuondoa vikwazo kadhaa ikiwamo kuwezesha kupatikana kwa safari za moja kwa moja kutoka Moscow hadi Dar es Salaam na Zanzibar.

Rais alisema hayo wakati akihutubia wawakilishi kutoka nchi 130 duniani zilizoshiriki mkutano wa kiuchumi wa kimkataifa wa Petersburg Juni 5, 2026.

Katika jukwaa hilo la kiuchumi, Rais  Samia  alitangaza kuwa kuanzia Julai 2 mwaka huu, Shirika la Ndege la Tanzania, Air Tanzania, litaanza safari za moja kwa moja kati ya Dar es Salaam, Moscow, na Zanzibar kwa lengo la kuongeza idadi ya watalii hadi kufikia laki tano ifikapo mwaka 2030 na hatimaye milioni moja. 

Hatua hii inaenda sambamba na ushindi wa tuzo za kimataifa ambapo hifadhi ya Serengeti imetajwa kuwa bora zaidi Afrika na Zanzibar kupewa tuzo kama eneo bora la mikutano na mapumziko. 

Rais Samia alihitimisha kwa kutoa rai kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa na nchi za Afrika ziko tayari kukua kupitia mifumo yao kama soko huru la Afrika, akisisitiza kuwa Tanzania imefungua milango yote kwa wabunifu na wafanyabiashara wanaotaka kushiriki katika safari hii mpya ya mabadiliko.

mwisho

Friday, June 5, 2026

RAIS WA JMT. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AHITIMISHA ZIARA YAKE URUSI KWA KUINADI TANZANIA KATIKA JUKWAA LA BIASHARA ST. PETERSBURG




Na Beda Msimbe, TBN, St Petersburg
                
Rais Samia Suluhu Hassan leo anahitimisha ziara yake nchini Urusi kwa kushiriki katika kongamano la kibiashara kati ya Tanzania na Urusi sanjari na Jukwaa la Kimataifa la Biashara la St Petersburg.                     
Katika jukwaa hilo Rais Samia anatarajiwa kuinadi Tanzania katika sekta za uwekezaji na biashara.   
          
Ziara ya Rais Samia imekuwa na mafanikio makubwa hasa hakikisho la ushiriano wa karibu na Urusi katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu ya uendelezaji wa rasilimaliwatu na ukuzaji wa teknolojia.  

Ziara hiyo katika taifa lenye nguvu kubwa kiteknolojia, uchakataji na uzalishaji kwenye kilimo au viwandani imekuja wakati Tanzania inajiandaa kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050 inayolenga kulifanya taifa kuwa na pato la dola trilioni moja kwa mwaka.                       
Kwa sasa serikali imesema Pato la Taifa kwa mwaka 2025 lilikua kwa wastani wa asilimia 5.9 ikilinganishwa na asilimia 5.5 mwaka 2024 kauli ilitolewa na Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar wakati akiwasilisha Mapitio ya Utekelezaji na Mpango wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 na Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 bungeni Dodoma hivi karibuni.

Balozi Omar alisema ukuaji huo ulichangiwa na kuongezeka kwa mikopo kwa sekta binafsi, kuimarika kwa miundombinu ya usafiri na usafirishaji na kuimarika kwa shughuli za kilimo.

Alitaja sababu nyingine ni kuongezeka kwa uzalishaji wa madini na shughuli za ujenzi wa umma na binafsi na utekelezaji wa miradi ya kimkakati, hususani katika sekta za nishati, usafirishaji na huduma za jamii. 

Mwisho.


TTB YALENGA KUVUTIA WATALII WA URUSI AMBAO WATALIINGIZIA TAIFA DOLA MILIONI 500 KWA MWAKA

 


Na Beda Msimbe, TBN, Petersburg, Urusi

 BODI ya Utalii Tanzania (TTB) inajipanga kumega keki ya utalii inayotengenezwa na Urusi kwa lengo la kulipatia taifa zaidi ya dola za Marekani 500 kwa mwaka.

Zaidi ya wananchi milioni 13.4 wa Urusi hutalii sehemu mbalimbali duniani na kutokana na kuwa watumiaji wazuri wa vipato vyao, Tanzania ikipata angalau asilimia 1 ya watu hao ambacho ni sawa na watu 134,000 ambao wataingiza dola milioni 500.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TTB, Ephraim Mafuru katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la Petersburg (SPIEF’26) linaloendelea mjini hapa.

Mafuru alisema katika mikakati hiyo wanataka katika miaka 10 ijayo kufikisha watalii mara mbili ya hao na hivyo kuliingizia pato taifa la dola za Marekani bilioni moja.

Akiwa katika banda la Tanzania katika jukwaa hilo alisema anafurahi kwa Rais Samia kuendelea kuelekeza maono kwa vitendo katika kusaka wawekezaji.

Pia kufungua fursa za Watanzania kwa ziara zinazojumuisha  watendaji wakuu wa maeneo muhimu ya taifa kama miundombinu, utalii na madini ili diplomasia ya uchumi iwe na maana kwa taifa.

Mafuru amesema kama nchi wamedhamiria kuhakikisha wanafungua soko la Urusi kwani katika utamaduni wa utalii, wanaongoza duniani na wanaongoza pia kwa matumizi ya kifahari (anasa).

Alisema wamekuwa na mikutano mingi ya utafiti na kubaini watalii hao walikuwa wanashindwa kufika kutokana na umbali lakini kuanza kwa safari za Ndege za ATC za moja kwa moja zitapunguza muda wa kusafiri kwa wananchi hao na kuwa sehemu ya hamasa ya kuja kutembelea Tanzania.

Aidha alisema kwamba wakati umefika kwa wananchi wa tanzania kujifunza Kirusi kwa ajili ya kuvutia watalii ambao hufurahishwa ikiwa wataongozwa kwa lugha ya nyumbani kwao.

Akizungumzia jukwaa na kongamano alisema ziara ya Rais Samia nchini Urusi imekuwa na mafanikio makubwa ambayo yatachangia kukua kwa utalii na pia kusaidia sekta ya uwezekaji na biashara.

mwisho

Thursday, June 4, 2026

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ATUNUKIWA SHAHADA KUTOKA RUDN UNIVERSITY - URUSI





Na Beda Msimbe,TBN, Moscow

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Shahada ya Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi- (RUDN University) huku akiitoa shahada hiyo kwa Watanzania.

Shahada hiyo ilitolewa na Mkuu wa Chuo hicho Profesa Oleg Yastrebov kwenye hafla iliyofanyika Chuoni hapo Moscow nchini Urusi, tarehe 04 Juni,2026.

Rais Mhe. Dk Samia ametunukiwa Shahada hiyo ya Uzamivu kutokana na mchango wake katika Mageuzi ya sekta ya Elimu, juhudi zake za kuimarisha Diplomasia ya Tanzania,

pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania Kimataifa ikiwemo kupitia sekta ya Utalii,

Akizungumza baada ya kupewa shahada hiyo Rais Samia alisema kwamba heshima aliyopewa si ya mafanikio yake binafsi bali ni utambuzi wa juhudi na matarajio ya watanzania wote.

Alisema shahada hiyo ni ishara ya utambuzi wa dhamira ya pamoja ya Watanzania wote katika kuleta maendeleo,ushirikiano na ustawi wa binadamu.

“Nilipokea kwa furaha habari za kutunukiwa heshima hii,lakini mara moja nikatambua kwamba si yangu peke yangu. Ni heshima inayoitambua dhamira yetu ya pamoja ya maendeleo, ushirikiano na maendeleo ya binadamu” alisema Dk Samia.

Hii ni shahada yake ya nane kutolewa kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha alisema shahada hiyo  aliyopewa leo ni ishara ya urafiki wa muda mrefu kati ya Tanzania na Urusi ikiwa ni uthibitisho wa nafasi muhimu ya elimu katika kuunganisha mataifa.

Aidha alisema heshima hiyo inaakisi uhusiano wa kudumu kati ya nchi za Tanzania na Urusi ambazo zimeendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali hususani elimu kwa miongo kadhaa sasa.

Katika hotuba yake ambayo viongozi wa watanzania waliopo  Urusi na vyuo vya Urusi walisema ni iluiyiojaa mamlaka makubwa, Rais Samia alisema kwa miaka mingi watanzania walikuwa wanapata elimu inayochangia maendeleo  ya Tanzania katika Nyanja mbalimbali jambo ambalo pia  limeimarisha mahusiano ya watu wa pande zote mbili,

“Mama amezungumza nchi yetuj ina sifa sana. Tena sifa njema kwa kupata mwaliko wa Rais Vladmir Putin kuja hapoa ni kutambulika kwa Tanzania ni ishara njema na hotuba ya mama imeakisi matarajio” alisema Jefrey Mashauri Mwenyekiti wa wanafunzi wa Tanzania shirikishoi la Urusi (TASCARU).

Naye Mwenyekit wa watanznaia wanaoishi Urusi Pascal Gura alisema watanzania 300 wanaosihi hapo wameona fahari kubwa kukutana na kumsikiliza Rais Samia akionesha ni kwa namna gani kama Taifa Tanzania linaendelea kuwika.

Rais Samia katika hotuba yake alionesha jinsi Tanzania inavyoweza kufanikisha mambo wanaposaidiana na kushirikiana kwa maendeleo ya taifa.

Pia alikumbusha vijana kujipatia elimu huku wakizingatia kauli ya baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere ambaye alifundisha kwamba maendeleo lazima daima yaweke mwanadamu katikati ya kila jambo.

Aidha alitaka vijana kuangalia taifa lao na kwamba dokumentari iliyooneshwa kabla ya kutunukiwa shahada kuhusu maendeleo ya Tanzania inawaonesha dhamira ya watanzania na ni muhumu kwao watambue umuhimu wao kwa taifa huku huku wakiyaakisi maneno ya baba wa taifa katika utumishi wao.

Tangu kuanzishwa kwa chuo hicho miaka ya 1960 watanzania 1,100 wamepata utaalamu mbalimbali kupitia hucho hicho.Idadi hiyo ni kati ya wanafunzi 5000 ambao wamepata taaluma zao nchini Urusi katika Nyanja mbalimbali ikiwamo udaktari uhandisi na wataalamu wa sayansi.

Rais katika hotuba yake pia alizungumzia makubaliano kadhaa yaliyotiwa saini  yenye lengo la kuleta ushirikiano wa aina yake katika utafiti na elimu na ufundishaji.







TANZANIA NA URUSI ZIPO KATIKA HATUA ZA MWISHO MAKUBALIANO KUHUSU MATUMIZI YA FEDHA


 Na muandishi wa TBN, Urusi.    

 Tanzania na Urusi zipo katika hatua za mwisho za majadiliano za matumizi ya fedha za malipo kwa lengo la kuimarisha biashara baina yao.      

  Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo kwenye mahojiano na waandishi wa habari waliopo katika msafara wa ziara ya kitaifa ya Rais Samia Suluhu Hassan nchini Urusi.      

 Alisema mataifa hayo mawili yatasaini hati za makubaliano kabla kumalizika kwa ziara.                

Alisema kuna urari wa biashara wa Dola za Marekani milioni 200 hivyo hatua hiyo ya kufikia makubaliano itafungua njia ya ushirikiano kwenye ufanisi katika masuala ya uwekezaji na biashara.                  

Alifafanua kuwa makubaliano hayo yatahusisha matumizi ya shilingi ya kitanzania.                        

Alisema Urusi ambayo ikishiriki katika ukombozi wa kisiasa sasa inakuja kusaidia ukombozi wa kiuchumi na iko mbele katika kilimo uchakataji na uzalishaji, mbegu bora, madini itakuwa msaada mkubwa katika utekelezaji dira ya maendeleo 2025 ambayo itaanza kitumika Julai mwaka huu.      

  Profesa Mkumbo alisema kuna manufaa makubwa katika ziara hiyo ni kuwezesha Ujenzi wa Reli ya Kusini kupitia mfumo wa Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP). 

Aidha alisema ili kurahisisha mawasiliano katika utalii, Tanzania na Urusi zipo katika hatua ya mwisho ya kuingia makubaliano yatakayowezesha Shirika la Ndege la Tanzania kufanya safari za moja kwa moja kutoka Dar es Salaam hadi Moscow.