Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, September 18, 2012

CAMERA YETU ILIVYOVINASA BARABARA YA KUTOKA MOSHI MJINI MPAKA WILAYA YA MWANGA MKOANI KILIMANJARO...!

 
Hii ni sanamu iliyopo katika keepleft cha YMCA

Gari hii yenye namba za usajili T584 AUW ilichomoka tairi ya nyuma na kupoteza muelekeo na kugonga mti uliokuiwa pembeni ya barabara na kusimama juu ya udongo uliokuwa karibu na mto.

 
Hili ni eneo la njia panda ya Himo kwenye mizani.

Hili ni soko la chekereni ambalo linauza vyakula mbali mbali na hapo utaona kuna nyanya, vitungu na pia kuna vituvingine vingi sana vinapatikana ndani ya soko hili na kwa bei rahisi sana. Japo wanafanyia biashara chini ya transformer ya umeme lakini hawana wasiwasi wowote.

 
King Jofa akifanya manunuzi kwenye soko la chekereni.


Huyu ni binti ambaye kwa mtazamo wangu nilijua ni mwanafunzi wa shule ya msingi lakini aliniambia kuwa ana umri wa miaka 16 na amemaliza darasa la saba mwaka juzi (2010)

Hawa ni mafundi wa Tanesco wakiwa juu ya nguzo katika zoezi la kubadilisha nguzo zilizochakaa na kuweka nguzo mpya.

Vijana wakijitahidi kujikwamua kiuchumi kwa kuuza kambale wa ziwa jipe maeneo ya kifaru.


Hiki ni kiwanda kilichopo maeneo ya kifaru na toka kimenza kufanya kazi ni takribani mwaka mmoja sasa, kinajihusisha na kutengeneza material ambazo zinaenda kutengeneza Wine, Wisk, Konyagi, spirit, rangi za nyumba na vinginevyo vingi sana.


King Jofa akiwa na Evelyne Mushi ambaye anafanya kazi Kilimanjaro Biochem ni Office assistant na pia ni important logistic .


 Mdogo wangu wa nguvu hakuwa na yeye alikuwa fasta kupata picha na Eveline Mushi wa Kilimanjaro Biochem.



Hili ni eneo la kisangiro ambalo lina shida sana ya maji na huwalazimu wakari wa eneo hili kwenda zaidi ya kilometa saba kutafuta maji. Kama unvyoona hapo ni wakazi wa eneo hili wakiwa na ndoo zao wa maji.




Hawa ni Bihawa upande wa kulia na Zulpha ni wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi kisangiro wakiwa wamepumzika eneowakimsubiri mwenzao, na huu ulikuwa ni muda wa saa nane na nilipo wauliza waliniambia wameruhusiwa kwenda nyumbani mapema ili wakajiandae na mitihani ya kumaliza darasa la saba.


Hii ni stand ya mwanga na hao ni baadhi ya abiria wakipanda gari lililokuwa limetokea Dar es salaam wakielekea maeneo ya Moshi mjini na Arusha.


King Jofa akiwa na Nuruh katika eneo la shule ya St. Theresa of Avilla iliyopo Mwanga na hapo Nuruh alikuwa akijiandaa na mtihani wa Geography.  


King Jofa akiiitetea taaluma yake ya IT katika  shule ya St. Theresa of Avilla.
HARD WORK PAYS.














No comments:

Post a Comment