Mrembo wa Ilala, Magdalena Roy, usiku
 wa kuamkia leo amefanikiwa kunyakua taji la mrembo wa pili kuingia 
hatua ya nusu fainali ya Redd's Miss Tanzania 2012 baada ya kuwashinda 
warembo wengine 29 na kutwaa taji la Top Model.
Magdalena aliibuka mshindi katika 
shindano dogo la Redd's Miss Tanzania lililofanyika usiku wa kuamkia leo
 katika Hoteli ya Kimataifa ya Naura Springs jijini Arusha.
Kwa matokeo hayo Top Model, 
Magadalena Roy anaungana na Miss Photogenic, Lucy Stephano katika nusu 
fainali hiyo na kukaa tayari kusubiri warembo wengine 13 watakaoungana 
katika Nusu fainali hizo.
Taji la TOP MODEL lilikuwa linashikiliwa na mrembo wa Temeke, Mwajabu Juma.
Mrembo kutoka Mkoa wa Mara na Miss 
Kanda ya Ziwa 2012, Eugene Fabian nae alifanikiwa kutwaa taji la Ubalozi
 wa Hotel ya Naura Spring ya jijini Arusha. 
Egene alitangazwa kunyakua taji hilo 
usiku wa kuamkia leo wakati wa shindano dogo la Redds Miss Tanzania 2012
 la kumsaka Top Model ambaye pia ataingia katika hatua ya 15 bora ya 
Shindano hilo la taifa la Miss Tanzania. Awali taji la Balozi wa Naura 
Spring Hotel lilikuwa likishikiliwa na Neema Joel.
picha zaidi zitawajia baadae kidogo. 
 


 
 
No comments:
Post a Comment