Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, March 12, 2018

SHIRIKA LA AGPAHI LAANZA KAMBI YA WATOTO NA VIJANA YA WIKI MOJA MJINI MOSHI – MKOANI KILIMANJARO

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dr. Asha Mahita akiwa katika picha ya Pamoja na Vijana na Watoto Nje ya Ukumbi wa hotel ya Uhuru iliyopo Mjini Moshi, Mkoani Kilimanjaro. 
Toka mwaka 2011 Shirika la Arial Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI)  Iimekua Msaada mkubwa kwa watoto wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi (VVU) nchini Tanzania. Shirika hili la kimataifa lisilo la Kiserikali lilianzishwa kwa Msaada wa Elizabeth Glaser Pediatric Aids Foundation  (EGPAHI) huku lengo kuu likiwa kutokomeza Ukimwi kwa watoto  nchini Tanzania. Mpaka sasa ni Takribani Miaka saba Shirika hili limekua Msaada mkubwa kwa watoto hao wanaoishi na VVU kutimiza Ndoto zao.

Watoto na Vijana wakimpokea Mgeni Rasmi Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dr. Asha Mahita Katika Ufunguzi wa Kambi ya vijana na watoto Mapema  leo Mjini Moshi.

Kila Mwaka Shirika la AGPAHI huandaa Kambi ya watoto kutoka katika Mikoa sita inayofanya kazi nayo ambayo ni Mikoa ya Tanga, Simiyu, Geita, Mwanza, Mara na Shinyanga. Kambi hiyo hukusanya watoto kutoka katika vikundi vya watoto na vijana ambavyo huundwa katika Vituo vya Afya husika. Watoto hao huudhuria katika vikundi ili kujifunza mambo mengi ikiwa ni pamoja na kupata ushauri wa tiba na elimu kuhusu matumizi sahihi ya Dawa za Kupungua Maambukizi ya VVU (ARV’s). Vikundi hivyo huwezeshwa kwa msaada wa shirika la AGPAHI kwa msaada wa watu wa Marekani.  Kupitia vikundi watoto na vijana hupata fursa ya kuhudhuria kambi ya wiki moja inayoandaliwa na shirika la AGPAHI. 

Mgeni Rasmi aliwa katika picha ya pamoja na watoto pamoja na Uongozi,Madaktari na wataalamu wa masuala ya watoto nje ya ukumbi wa hoteli ya Uhuru mjini Moshi.

Leo Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga   Dr. Asha Mahita amefungua Kambi ya wiki moja ya watoto na vijana katika Ukumbi wa Hotel ya Uhuru  Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro. Dr. Mahita alitumia nafasi hiyo kuzungumza moja kwa moja na watoto takribani hamsini (50) kutoka Mikoa mitatu ya Tanga, Mwanza na Geita ambao wamehudhuria kambi hiyo. Watoto na vijana wenye umri wa miaka 10 – 17.

“Fursa hii kwangu ni fursa hadimu sana kukutana na watoto wengi kama ninyi wenye tumaini kuu na hari ya kutimiza ndoto, Nawahakikishia kuwa siku moja mtasimama na kuidhihirishia jamii kwa vitendo kuwa mnaweza, Cha muhimu ni kuzingatia matumizi sahihi ya dawa na kuendelea kuwepo kwenye huduma.” Alisema Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga.

Dr. Mahita akijibu swali la mmoja wa watoto waliomuuliza maswali leo.

Pia aliweza kukaa na watoto na kuzungumza nao kuhusu afya zao na kuwapa nafasi ya kuuliza maswali  kuhusu ufahamu wa  VVU / UKIMWI kitaalamu. Moja ya maswali hayo ni:- Njia za Maambukizi ya VVU, Faida ya kutumia dawa za kupunguza makali ya VVU.

Watoto na vijana wakiuliza maswali kwa Mgana Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dr. Mahita.


Hata hivyo AGPAHI waliweza kueleza dhumuni kuu la kambi hiyo Kuwakutanisha watoto na vijana ili kujifunza mambo mbalimbali kuhusu afya, Kutoa ushauri wa  Kisaikolojia kwa watoto wanaoishi na VVU, lakini pia kuwasaidia uangalizi wa afya zao na maendeleo ya afya zao. Ambapo katika kambi hii kuna Mtaalamu wa Saikolojia ambaye wakati wote wa kambi atatoa nafasi ya kuzungumza na kila mtoto kwa wakati wake ili kuweza kufahamu na kutatua yale ambayo yanawakabili kitaalamu. Lakini pia katika kambi hii kuna Madaktari Bingwa wa watoto  ambao wakati wote watakua wakiwahudumia watoto katika kipindi chote cha kambi.

Meneja mawasiliano Bi. Jane Shuma akielezea Dhumuni la Kambi ya vijana na watoto katika sherehe za ufunguzi wa kambi ya wiki moja mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro.


 AGPAHI wanaamini watoto kujifunza katika michezo ni moja ya Eneo sahihi hivyo basi  wamewashirikisha wawezeshaji wa Michezo ambao wameandaa mpango maalumu wa mafunzo kupitia Michezo kwa siku zote za kambi hiyo.

Mtoto akicheza katika kipindi cha elimu kwa njia ya Michezo.
Pia watoto walipata fursa ya kusikia machache na kuuliza maswali kutoka kwa Kijana Muelimishaji rika kutoka Mwanza ambaye ameshahudhuria  Kambi kadhaa za vijana. Muelimishaji rika huyo alieleza faida ya mafunzo ya kambi, ambayo ni kuweza kupata nafasi ya kuhudhuria mkutano wa Vijana wa Dunia huku yeye akiwakilisha Vijana wa Afrika.  “Nilihudhuria Mafunzo mwaka 2013, Nilifundishwa kujiamini na kuijua thamani yangu, Mafunzo haya yameniwezesha kuaminika na kuiona Thamani yangu.” Alisema  Muelimisha Rika.


Mtoto akiuliza swali kwa kijana Muelimishaji Rika baada ya kuzungumza na kuruhusu maswali.

“Moja ya changamoto Shirika inazokabiliana nazo ni watoto wengi waliozaliwa na VVU kujinyanyapaa na kutokubali hali ya kuishi maambukizi. Hii hupelekea kutokutumia dawa kwa usahihi, kupata magonjwa nyemelezi na kupelekea kifo, Changamoto nyingine ni jamii kuendeleza unyanyapaa na Ubaguzi kwa watoto…..ubaguzi  ambao hupelekea watu wanaoishi na VVU kujinyanyapaa wenyewe na kuona kwamba hawahitajiki kwenye jamii ndio maana shirika la AGPAHI linafanya kazi kwa karibu na wahudumu wa afya ili waweze kuwasaidia watoto  kutumia dawa kwa usahihi na kwa wakati pamoja na  kuhudhuria Kliniki  kila mwezi kama inavyoshauriwa” Alisema Jane Shuma Meneja Mawasiliano - AGPAHI



No comments:

Post a Comment