Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, June 22, 2012

MAMA WEMA SEPETU KICHEKESHO!!!





MAMA wa Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu ametoa kichekesho cha mwaka baada ya kufanya mahojiano na Tv moja ya jijini Dar akilenga kumsafisha mwanaye kwa kuwananga marafiki na magazeti pendwa, Ijumaa lina ripoti kamili.
Katika mahojiano hayo, Mama Wema ‘alibwabwaja’ mengi huku akitupia lawama makundi mengine wakiwemo marafiki wa kiume wa mwanaye.
AJISIFU KUMLEA WEMA VIZURI
Bila soni wala aibu, mzazi huyo alijisifu kumlea VIZURI Wema, jambo lililoibua maswali miongoni mwa watazamaji wa runinga hiyo huku wengine wakiomba kamusi ya Kiswahili sanifu ili kujua maana ya neno ‘vizuri’.
“Japo sikumnyonyesha lakini mwanangu nimemlea vizuri. Ana maadili mazuri ya Kiafrika,” alisema mama huyo.
AFUNGUKA BILA BREKI
Katika mahojiano hayo aliyoyafanya Juni 19, mwaka huu, mama huyo aliwashushia lawama mashoga wa mwanaye akisema walimpoteza Wema kwa kumpeleka kwa waganga wa kienyeji kipindi cha nyuma na kumfanya awe ‘mawengemawenge’.
“Nimehangaika sana usiku na mchana kumfanya mwanangu arudi kwenye hali yake ya kawaida. Marafiki zake walimpoteza, walimpeleka kwa waganga kitendo ambacho kilichangia kwa kiasi kikubwa kumpoteza mwanangu, akawa mtu asiyejielewa,” alifunguka bila breki.
ALIKOROGA, ATALINYWA
Kwa kauli hizo tu, Ijumaa lilipokea simu nyingi kutoka kwa mastaa na wasomaji wa kawaida wakidai kuwa mama huyo alikuwa amewachekesha kwani tangu kipindi hicho kilipokwenda hewani siku hiyo, marafiki wote wa Wema waliamua kujichenga na kumwachia maisha ya peke yake huku wakidai kama anataka kuishi kwa raha atafute kisiwa cha kuishi huko.
“Mdomo uliponza kichwa, sisi ni marafiki zake na tunafanya naye kazi kwa upendo mkubwa lakini kwa kauli ya mama tunaonekana tunajipendekeza. Acha aishi dunia ya peke yake,” alisema mmoja wa waigizaji kiwango hapa Bongo.

TURUDI KWA MAMA WEMA
Akiendelea kuropoka mambo bila kuanika ushahidi wa wazi, mama huyo alisema marafiki wote wa Wema ni wanafiki na kama mwanaye anataka marafiki wa kweli, ni yeye mama, dada yake Wema (pengine yule anayeishi Kumekucha- Sinza) na ndugu wengine wa karibu.
ETI WEMA MAMBO SAFI
Mama Wema alifunguka kuwa katika kipindi hiki ambacho mwanaye mambo yake yanamwendea vizuri hataki marafiki wanafiki wanaomfuatafuata Wema kwa lengo la kumchafua.

No comments:

Post a Comment