Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, June 22, 2012

DIAMOND AJIRUDI KWA WEMA!!!



WASWAHILI husema ‘penzi ni kikohozi, kulificha huwezi’, usemi huo ulidhihirika Juni 15, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Golden Tulip jijini Dar ambapo kulikuwa na shindano la kumpata Miss Dar City Centre wa mwaka 2012/13.
Katika shindano hilo, staa wa Muziki wa Bongo Fleva anayeng’aa vizuri kwa sasa, Naseeb Abdul ‘Diamond’ alijikuta akilazimishwa na nguvu ya umma kujirudi kwa mchumba wake wake wa zamani, Wema Isaac Sepetu.
ISHU ILIANZA HIVI
Wakishuhudia tukio la ‘Platinumz’ kujirudi kwa Wema, wapiganaji wa Ijumaa Wikienda walimsikia msanii huyo akipindisha kwa makusudi mashairi ya wimbo wake wa Nimpende Nani? akianza kumsifia Wema Sepetu huku akimaanisha kuwa anachoimba anakifahamu na kutaja cheo ambacho mrembo huyo alikuwa nacho usiku huo, cha ujaji.
WIMBO HALISI UKO HIVI:
“…yasiwe kama ya Wema Sepetu, kila siku magazeti,
ajue nidhamu na mila ya kwetu, mjuzi kupeti-peti,
simtaki ka’ Uwoya ni mtemi ana hasira, mpole kama Jokate, ila sauti ka’ Wema akiwa analia, kicheko kama cha Fetty…”

WIMBO WA UKUMBINI ULIKUWA HIVI:
“…asiwe kama Jaji Sepetu kila siku magazeti, ajue nidhamu na mila ya kwetu, mjuzi kupetipeti, simtaki ka’ Uwoya ni mtemi ana hasira, mpole kama … (akakaa kimya na kuacha mashabiki wakimalizia kwa kusema, Wemaaa).”
Diamond akaendelea: “Ila sauti kama ya Jaji Sepetu akiwa analia, mpole kama … (akakaa kimya kwa mara nyingine na kuwaacha mashabiki wamalizie ambapo walisema kwa sauti za juu, Wemaaaaa.”
Akiendelea kubadili mashairi ya wimbo wake huo, Diamond alidiriki kuacha baadhi ya majina ya warembo wengine aliowataja, Jokate na Fetty na kuingiza vipande ambavyo viliashiria kumwangukia mrembo huyo.
MKUU WA WILAYA TEMEKE AUNGA MKONO
Tukio jingine la kufurahisha ambalo liliandika historia ya aina yake ni pale Diamond alipouliza mashabiki wake kwa kutumia ‘maiki’, Nimpende Nani? ambapo Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Bi. Sophia Mjema aliungana na mashabiki kujibu: “Wemaaa.”

No comments:

Post a Comment