Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, June 22, 2012

WEMA NA JOKATE NUSURA WAZICHAPE!!



MASTAA wa kike wanaotambiana Bongo, Wema Sepetu na Jokate Mwegelo, ilibaki kidogo wazichape kavukavu kisa kikiwa kilekile, msanii anayetingisha katika Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’.
Chanzo chetu makini kimenyetisha kwamba mtiti huo ulitokea Ijumaa Mei 25, mwaka huu katika Ukumbi wa Blue Pearl, Ubungo, Dar ambapo kulikuwa na Shindano la Miss IFM, 2012.
CHANZO KINADADAVUA
Katika ‘event’ hiyo, Wema alikuwa mmoja wa majaji waliochagua washindi wakati Jokate alifika kama mdau wa urembo huku uwepo wa Diamond ukiwa kwa ajili ya kupiga shoo.
“Wema alikuwa mmoja wa majaji, Jokate alikwenda kama shabiki tu, lakini mambo yalianza kuharibika baada ya mshindi kutangazwa ambapo Jokate hakuridhishwa na matokeo.
“Hata hivyo, watu walisema ni chuki zilizosababishwa na wivu wa kimapenzi kwa Diamond,” chanzo kilieleza.
JOKATE ALIANZA HIVI
Habari zinasema kwamba, Jokate aliamua kupita mbele ya meza ya majaji na kumuuliza Wema kama yeye aliridhika na matokeo yale.
“Ilikuwa balaa, Jokate alikwenda kwenye meza ya akina Wema (majaji), akaanza kumuuliza, yaani huyu ndiyo mshindi mliyetuchagulia? Miss gani anakuwa hivyo?” kilisema chanzo na kuongeza:
“Kifupi alikuwa akitoa kejeli kwa majaji hasa Wema kwa vile aliwahi kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya dunia.”
WEMA AKAMALIZA
Baada ya chokochoko za Jokate ambaye inasemekana alikuwa ‘amechangamka’ kidogo, Wema alijibu mashambulizi kwa staili ya aina yake, alikaa kimya akiendelea na shughuli nyingine.
“Ukimya wa Wema ukasababisha Jokate azomewe kwa sauti kubwa na mashabiki huku wakimsonya. Kiukweli bila ushabiki, Wema alionesha ukomavu siku ile.
“Kama naye angepandisha hasira, ilibaki kidogo sana wakung’utane, maana Jokate alionekana dhahiri kutaka ugomvi lakini mashabiki wakaununua kwa kumzomea. Aliabika sana,” kiliendelea kupasha chanzo hicho.
DIAMOND AAMSHA SOO UPYA
Wakati Diamond akiwa jukwaani ‘akipafomu’ wimbo wa Nimpende Nani? ikawa kama ameamsha ‘muziki’ upya kabisa kwa upande wa Jokate.

No comments:

Post a Comment