Kampuni
ya Global Publishers & General Enterprises Ltd leo imetoa hundi ya
shilingi milioni 10 ikiwa ni sehemu ya mapato yaliyopatikana kwenye
Tamasha la Matumaini lililoandaliwa na kampuni hiyo kwa ajili ya
kuchangia ujenzi wa hosteli za wasichana nchini. Kampuni hiyo imetoa
hundi hiyo kwenye hafla fupi iliyofanyika katika Hoteli ya Atriums
iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment