Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, July 7, 2012

MAPAJA YA UWOYA YAMLIZA MCHIMBA MADINI MIRERANI...!

 Irene Uwoya.
 Mchimba madini .
Stori: Imelda Mtema, aliyekuwa Mererani
MAPAJA ya mcheza filamu mkali Bongo, Irene Uwoya yamemtoa machozi mchimba madini maarufu ‘Mwanaapolo’ wa mgodi wa Florida uliopo Mererani, Manyara.
Tukio hilo ambalo ni sawa na kituko, lilijiri hivi karibuni wakati staa huyo na wenzake wa Bongo Movie walipotinga eneo hilo kwa ajili ya uzinduzi wa filamu moja ya msanii mwenzao.
Ilikuwa wakati wasanii hao wakiingia kwenye mgodi huo kwa lengo la kujifunza uendeshaji wake kuanzia kuchimba madini, ilipofika zamu ya Uwoya, sauti ya kilio kikubwa ilisikika kutoka kwa Mwanaapolo huyo aliyejulikana kwa jina la Hamad Hussein.
“Aaaash! Weweeee! Weeee, dada unaniumiza wewe, dadaaa jamani,” alisema mchimba madini huyo akimkazia macho Uwoya huku wenzake wakishangilia kumuunga mkono.
Njemba huyo aliendelea kupiga kelele huku akivua kofia na shati hali iliyomfanya paparazi wetu amfuate kumuuliza kulikoni.
“Hapana dada, niache tu yule dada ni mzuri. Sijawahi kuona mwanamke mwenye mapaja mazuri kama huyu, nipo hapa kwa zaidi ya miaka minne. Sasa jamani amenichanganya, navua nguo zote sasa hivi siwezi kuvumilia,” alisema Hamad huku akilia.
Baada ya Irene kutoka shimoni, jamaa huyo alipaza sauti tena na kumrushia kofia Irene ili aivae lakini kwa bahati mbaya staa huyo alishaingia ndani ya gari na kwenda kwenye mgodi mwingine.

No comments:

Post a Comment