Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, August 27, 2012

Jinsi ambavyo Watoto wa Kike wengi wanashindwa kumaliza Shule kutokana na kurubuniwa na wanaume...!

Imebainishwa kuwa ni asilimia kubwa ya watoto wa kike hawamalizi shule kutokana na kupewa  mimba,kudanganywa na vitu vya thamani mbalimbali nakusababisa kutofikia malengo yao ya maisha.
Hayo yamebainishwa  na  muuguzi mkuu wa hospitali ya Mkoa wa manyara Theonestina Rwechungura wakati alipokuwa  akiongea  kwenye mjadala  ulioandaliwa na  mradi wa  Je Nifanyeje? Unaofadhiriwa  na watu wa USAID mjadala huo ulifanyika katika chuo cha  ufundi cha St Joseph kilichopo maeneo ya Dareda Halmashauri ya wilaya ya Babati Mkoani wa Manyara.
Alibainisha kuwa siku hizi si kama miaka ya nyuma kwa mtoto wa kike kumaliza shule au chuo kutokana na kuwa na tama,kudanganywa na vitu nakusababisha kukatishwa kwa masomo pamoja na kupata ujauzito.
Alisema kuwa mtoto wa kike anatakiwa kupatiwa elimu ya kutosha ili hapo baadaye aeweze kupambana na umaskini nasi kuwa tegemezi katika familia pamoja na jamii kwa ujumla.
Aliongeza  kuwa  ukimwi umekuwa wimbi  kila sehemu wanazungumzia  ukiwa shueleni,chuoni ili kuweza kutimiza malengo yao lazima wajiheshimu,kujitunza,kujiamini pamoja na kujithamini.
Aidha alisema kuwa ukiwa na tamaa utafanya vitendo viovu visivyofaa kwani tafiti za watoto wa kike wanakatishwa masomo kutokana na ujauzito hivyo wanatakiwa wajilinde ili kuweza kutimiza malengo yao.
Alisema  kuwa wasichana wanatakiwa wajifunze kusema hapana na wajifunze kukataa bali waendelee na masomo yao wajieupushe  na mambo ya vishawishi ndio chanzo cha vishawishi.
Kwa upande wake  mratibu wa mradi huo kutoka ‘Je Nifanyeje Diana Nsindagi  aliongeza  kuwa mradi huo unalenga vijana hasa wa kike ili kuwawezesha kufanya maamuzi sahihi ya kiafya na kijamii amewataka watoto wa kike wasome kwa bidii ili kutimiza ndoto zao za baadaye.
Pia alitaja  mambo muhimu ya kuzingatia ili kuweza kufanya maamuzi sahihi ya kiafya na kijamii ni jiamini,jithamini,jitambue,jiheshimu,jiwekee malengo,tambua mila na desturi zinazokuzunguka,tambua jamii inayokuzunguka na imani yao.
Wakichangia  mjadala huo   washiriki hao ambao ni  vijana wakike  wamesema kuwa watoto wa kike wanatakiwa  wawe na msimamo na maamuzi sahihi ili baadaye weweze kusonga mbele,wawe na mpenzi mmoja,wamshawishi mpenzi kupima afya,kutumia kondomu pia waepuke na makundi mbalimbali.

No comments:

Post a Comment