Rais Yoweri Museveni wa Uganda amebuni jopo maalumu
litakalochunguza
kisa cha kuanguka kwa helkopta 3 za jeshi la nchi yake huko
nchini Kenya
siku ya Jumapili.
Jopo hilo litakaloongozwa na aliyekuwa mkuu wa majeshi ya
Uganda
Jenerali Salim Saleh linatarajiwa kutafiti chanzo cha ajali
hiyo ambapo
wanajeshi wawili wamethibitishwa kufariki dunia.
Wakati huo huo Rais Mwai Kibaki ametuma risala za rambirambi
kwa Rais
Museveni ambapo pia amemuahidi kwamba serikali ya Kenya
itashirikiana
na jopo hilo ili kupata ukweli wa chanzo cha mkasa huo.
Mapema jana, mabaki ya Helikopta mbili za Jeshi la Uganda
zilizokuwa
zimeripotiwa kutoweka yalipatikana katika msitu wa mlima
Kenya.
Wanajeshi wawili wa Uganda wamethibitishwa kufariki dunia
huku wengine
wanne wakiwa bado hawajulikani walipo.
Jumla ya wanajeshi 15 wa UPDF waliokuwa kwenye helikopta
hizo
wameokolewa.
No comments:
Post a Comment