Baraza kuu la waislamu (BAKWATA) mkoani Kilimanjaro limekana
kuhusika
juu ya vipeperushi vinavyosambazwa kushawishi watu
wasishiriki katika
sensa ya watu na makazi inayotarajia kufanyika usiku wa
kuamkia
augusti 26 mwaka huu.
Akizungumza katika kikao cha dharura cha baraza hilo,shekhe
mkuu wa
mkoa wa Kilimanjaro Sheikhe Shaban Rashid amesema wao kama
baraza
hawahusiki na vipeperushi hivyo na kwa yeyote anayehusika
yafaa
kuchukuliwa hatua kali.
Sheikhe Shaban ameyasema hayo baada ya kukamatwa kwa watu
sita
wilayani mwanga na wilayani same ambapo amesema kitendo cha
kusambaza vipeperushi hivyo kwa dini ya kiislamu ni aibu
kwani ni kuipinga
serikali kwa kutotii maagizo yake ambayo ni kwa manufaa ya
wananchi
wake na waislamu pia.
Kwa upande wake mwenyekiti wa baraza hilo sheikhe Ramadhan
Salim
amewataka waislamu mkoani hapa kuwapuuza wanaosambaza
vipeperushi
hivyo na kuunga mkono jitihada za serikali ili kufanikisha
zoezi hilo
ambalo ni kwa manufaa ya taifa zima na waislamu kwa ujumla
sanjari na
kuwaonya wale wanaotaka kugomea zoezi hilo kutokufanya hivyo
kwani ni
kinyume na taratibu za dini ya kiislamu.
No comments:
Post a Comment