Huyu nfio Dereva wa pikipiki aliye sababishiwa ajali na trafiki.
Dereva wa pikipiki akiwa amekaa chini muda mfupi baada ya kupata ajali.
Kituko
cha mwaka kimetokea leo mchana muda wa saa saba huko Arusha mjini,
baada ya Trafiki mmoja (hayupo pichani) kumkamata Dereva wa Bodaboda
(pichani aliyeumia) na kumpa maelekezo ya kupeleka Pikipiki hiyo kituo
cha polisi! cha ajabu wakiwa njiani Dereva Bodaboda alibadili nia na
kutaka kuelekea sehemu tofauti na kituoni! hali hii ilimfanya Polisi
kushtukia ujanja huo wa dereva huyo wa bodaboda na kuanza kushika usukani na kulazimisha pikipiki ipelekwe kituo
cha Polisi, kwa hatua hii Pikipiki hiyo iliendeshwa na watu wawili hadi
kituo cha Polisi ilipotokea ajali hii.
No comments:
Post a Comment