Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, August 17, 2012

NHIF YAISAIDIA ZAHANATI YA MBUTU...!

Zahanati ya Mbutu iliyopo Kata ya Somangila Manispaa ya Temeke ambayo imechangiwa shilingi milioni tatu na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa ajili ya ujenzi wa Wodi ya akina mama.
 
Diwani wa Kata ya Somangila, Aisha Mpanjila akionyesha hundi ikiwa ni msaada uliotolewa na  mfuko wa bima wa afya NHIF .
 
Meneja wa Kanda ya Temeke Imelda Likoko akibadilishana mawazo na Mganga wa Zahanati ya Mbutu

 Na Mwandishi Wetu
DIWANI wa Kata ya Somangila, iliyopo Temeke, Aisha Mpanjila amesema kuwa
kitendo cha Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya cha kusaidia Zahanati ya Mbutu
kitahamasisha wananchi wengine kuchangia ujenzi unaoendelea katika
zahanati hiyo na hatimaye kumaliza tatizo la miundombinu.

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, jana ulikabidhi hundi yenye thamani ya sh.
Milioni tatu kwa lengo la kusaidia ujenzi wa wodi ya akina mama na watoto.

Akipokea msaada huo, Diwani Mpanjila alisema kuwa NHIF imeonesha njia na
imekuwa mfano wa kuigwa hasa kwa kutambua mahitaji ya wananchi katika
sekta ya afya.

"Kweli nyie ni Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya…pamoja na kusaidia
wanachama wenu katika huduma za matibabu lakini mmekwenda mbali zaidi kwa
kutoa hata msaada wa kuboresha vituo vya kutolea huduma msaada ambao
unamgusa kila mtu…nawapongeza sana," alisema.

Kutokana na hali hiyo, Diwani huyo alitumia fursa hiyo kuwaomba wananchi
wa maeneo hayo ambao ni wanufaika wa moja kwa moja na zahati hiyo kuunga
mkono Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuchangia ili ujenzi wa wodi
zilizopo zikamilike na zianze kutumika mara moja.

Naye Mjumbe wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Mariam Wilmore amesema NHIF imeguswa na matatizo ya wakazi wa kata hiyo hivyo itaendelae kusaidia kadiri ya uwezo wake.
 
Zahanati ya Mbutu inahudumiwa zaidi ya wakazi wa mitaa SITA inayozunguka kata hiyo.

No comments:

Post a Comment