Waziri Mkuu Mizengo Pinda Bungeni.
NA MAGRETH KINABO – MAELEZO, DODOMA
Waziri
Mkuu Mizengo Pinda amesema kwamba mtu yoyote ambaye anona hakutendewa
haki kuhusu kufungiwa kwa Gazeti la Mwanahalisi anaweza kufafuta
utaratibu mwingine wa kwenda mahakamani.
Kauli
hiyo ilitolewa leo Bungeni na Waziri Mkuu Pinda wakati akijibu swali
la Kiongozi wa Kambi ya Upinzania Bungeni , Freeman Mbowe lililouliza
kuwa Julai 30, mwaka huu, Serikali ililifungua gazeti la
Mwanahalisi kwa muda usiojulikana kwa kutumia sheria ya magazeti ya
mwaka 1976.
Maadam katika siku za hivi karibuni serikali imetambua umuhimu wa mahakama ni
Kwanini wamelifungua gazeti hili badala ya kulipeleka mahakamani na wahusika wapate nafasi ya kujitetea kabla ya kuhukumiwa?
Akijibu
swali hilo , Waziri Mkuu Pinda alisema ni kweli serikali imechukua
hatua hiyo, lakini imechukua hatua hiyo kwa kuzingatia sheria na
taratibu za nchi na “
mtu
yoyote kwa msingi wa sheria hiyo anaona hajatendewa haki ni juu yake
kutafuta utaratibu mwingine wa kwenda mahakamani,” alisema Waziri Mkuu
Pinda.
Katika
swali lake la nyongeza la kiongozi huyo lililouliza kuwa Sheria
iliyotumika imekuwa ikilalamikiwa na wadau wengi na vyombo vya habari
kwa muda mrefu . Je wewe huamini kwa kutumia sheria hiyo ni kunyima haki
na ni msisitizo wa utawala usio bora?
Akijibu
swali hilo Waziri Mkuu Pinda alisema “ Mimi siamini hivyo kwa sababu
sheria hiyo imetungwa na Bunge tukufu na kuwa bado inatumia ni sheria
halali, sisi tutaendelea kuitumia mpaka hapo itakapobadilishwa.
No comments:
Post a Comment