Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, September 20, 2012

HELKOPTA YA SYRIA YAANGUKA DAMASCUS...!

Televisheni ya taifa nchini Syria imeripoti kuanguka kwa helikopta ya kijeshi karibu na mji mkuu Damascus baada ya kugongana kidogo na ndege ya abiria ambayo iliweza kutua salama.
Inaarifiwa kuwa ndege ya abiria ilikuwa imewabeba watu miambili.
Taarifa hiyo inasema ndege ya abiria ilitua salama katika uwanja wa ndege wa Damascus.
Mapema, duru za upinzani zilidai kuwa waasi ndio waliidungua helikopta hiyo.
Serikali imekuwa ikitumia helikopta na ndege nyinginezo katika harakati zake dhidi ya waasi.
Mwezi jana wapiganaji wa upinzani walidai kuidungua helikopta nyingine ya serikali.

No comments:

Post a Comment