Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, September 26, 2012

Marais wa Sudan na Sudan Kusini wafanikiwa katika mazungumzo yao. ..!

Rais wa Sudan Omar al-Bashir akipeana mkono na Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir mjini Addis Ababa.

Viongozi wa Sudan na Sudan kusini Jumanne walifanikiwa kupata maendeleo makubwa katika siku yao ya tatu ya mazungumzo kwenye mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.

Rais Omar Al  Bashir wa Sudan na mwenzake  wa Sudan Kusini  Salva Kiir , wamekuwa wakifanya majadiliano mjini  Addis Ababa tangu  Jumapili.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nchi za nje wa Sudan, El Obeid Al Morawah amesema, Jumanne  katika siku ya tatu ya mazungmzo nchi hizo mbili zilikubaliana . lakini anasema bado kuna vizuizi kuhusiana na suala la mzozo wa kumiliki eneo la Abyei lenye utajiri wa mafuta.

Nchi hizo pia zinajadili kubuni eneo lisilokuwa na shughuli za kijeshi kwenye mpaka wao, eneo la kilomita 23. Lakini suala hilo pia bado linabaki kuwa suala gumu.

Mkutano baina ya marais hao wawili uliopangwa kufanyika Jumanne  asubuhi uliahirishwa hadi jioni. Msemaji Al Morawah anasema ikiwa nchi hizo mbili za Sudan zinaweza kukubaliana juu ya Abyei na eneo la kilomita 23, basi masuala mengine yalosalia yanaweza kutatuliwa vilevile. 

Chanzo:  www.voaswahili.com

No comments:

Post a Comment