Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, September 26, 2012

NAIBU WAZIRI AMFUKUZA MWALIMU WA SEKONDARI ...!

Naibu waziri wa elimu na ufundi ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI akiwa anaongea na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Ilboru

Naibu Waziri wa elimu na ufundi Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi mwalimu wa shule ya Sekondari ya vipaji Maalumu ya Ilboru Mkoani Arusha mara baada ya kukutwa akiwa amelewa wakati wa kazi shuleni hapo

Hatua hiyo imekuja mara baada ya waziri huo kufanya ziara ya kawaida shuleni hapo kutafuta ufumbuzi wa tatizo la wanafunzi kupelekea kuandamana hadi ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kugoma kuingia darasani hivi karibuni

Majaliwa alilazimika kufanya hivyo wakati akiongea na walimu wa shule hiyo juu ya nini chanzo cha mgogoro huo,ambapo mwalimu huyo,Potin Jovita Sumawe, alinyanyuka na kuanza kuongea kama mtu aliyechanganyikiwa mbele ya Waziri huyo

“Nimemuagiza afisa utumishi kumpeleka hospitalini kwaajili ya kupimwa kama anamechanganyikiwa na ripoti iliyoletwa kwangu nikuwa alikuwa amelewa hivyo tunamsimamisha kazi na kuanza kupitia faili lake tuone kama anaweza kuonyeka ama laa!”alisema Majaliwa

Aidha aliongeza kuwa watumishi wote hawatakiwi kwenda kazini wakiwa wamekunywa au wametumia kilevyi cha aina yeyote huku akisisitiza kuwa mahali pa kazi sio mahali pa kunywa pombe kwa kufanya hivyo nikuvunja sheria ya utumishi wa umma

“Kama mtumishi wa umma anavunja sheria kwa kunywa pombe kazini atachukuliwa sheria kwa kuwa hata Yule mtoto aliyekabidhiwa kumfundisha anamfundisha kwa misingi ipi?wafanye kazi kwa maadili mema”alisema Majaliwa

Aliongeza kuwa hii sio hapa tu bali sehemu yeyote mfanyakazi wa serekalini au sekta binafsi haruhusiwi kufanya kazi akiwa  amelewa hivyo mtu yeyote akikutwa hivyo anastaili kufukuzwa kazi.

No comments:

Post a Comment