Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, September 28, 2012

TAZAMA SOKO LA KILOMBERO ARUSHA PALIVYOCHAFUKA KWA MABOOM NA MOTO...!

Wamachinga zaidi ya mia mbili katika eneo la soko la kilombero mkoani Arusha walivamia eneo lililokuwa na uzio na kuvunjwa uzio huo na kuingia katika eneo hilo na kung'oa mabati na miti iliyokuwepo katika eneo hilo na kucanza kuchoma moto. Kwa maelezo ya wamachinga hao wanadai kwamba lilikuwa ni eneo la wazi kwa muda mrefu lakini baadaye eneo hilo likauzwa na madiwani bila kushirikisha serikali ya mtaa, kesi ikapelekwa mahakamani na ayeuziwa eneo hilo akasimamishwa kujenga na kesi ipo mahakamani, Jana asubuhi wafabiashara ndondogo maarufu kama wamachinga waliamua kuvunja uzio wa eneo hilo na kujigawia eneo hilo na polisi walikuja wakawa wanaangalia tuu baada ya kuona wingi wa wamachinga hao. Lakini baadae askari waliongezeka na kuanza kupiga mabomu ya machozi ili kuwasambaratisaha wamachinga hao....


Hali inavyoonekana kwa sasa Eneo la kilombero jijini arusha wananchi waamua kuchoma matairi
Wabomoa uzio wa eneo hilo lililokuwa limezungushiwa mabati

 Fire wamesha fika kwa ajili ya kudhibiti madhara yoyote ya moto

 Lilifika Gari moja kwanza

Polisi wakiwa eneo la tukio
Sasa Yamekuwa matatu na yote yamejaa FFU kwa ajili ya kulinda usalama wa wananchi..
Chanzo: ujanatz.blogspot.com

No comments:

Post a Comment