Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, September 30, 2012

UONGOZI WA KIJIJI WALALAMIKIA UTENDAJI MBOVU WA DIWANI KUTOKANA NA TOFAUTI ZA VYAMA…!



Afisa mtendaji wa kijiji cha kondeni Stella K. Massawe (Kushoto) akiwa na Mwenyekiti wa kijiji cha kondeni Bw. Lyimo (Kulia). Wakiwa kwenye kikao cha kujadili maendeleo ya kijiji cha Kondeni


Baadhi ya wajumbe waliohudhuria katika kikao cha kujadili maendeleo ya kijiji cha Kondeni


Uongozi wa kijiji cha kondeni kilichopo katika kata ya Mwika kusini, jimbo la Vunjo umejikuta katika utata ambao mpaka sasa hawajajua hatima yao kwa kile wanachokilalamikia kuwa ni utendaji mbovu wa diwani wa kata hiyo. Mtafuru huo ambao unasemekana ni wa muda mrefu ila siku za karibuni ulionekana kufikia hatua mbaya pale alipokuja mkandarasi wa barabara ya kutoka kilacha mpaka msae ambayo ni barabara yenye takribani kilometa ishirini lakini mpaka sasa barabara hiyo imetengenezwa kutokea kwa betueli mpaka msae ambayo ni takribani kilometa mbili tu na mkandarasi huyo tayari amesha chukua vifaa vyake katika eneo hilo kitendo ambacho kinaashiria kuwa ameshamaliza kazi hiyo na utengenezaji wa barabara hiyo. Na toka achukue vifaa hivyo tayari umeshapita muda wa wiki mbili. Watendaji hao walikuwa wakitupa lawama kwa diwani kwa kusema walimuona diwani wao akiwa na mkandarasi wa barabara hiyo lakini hawajui ni nini kinachoendelea kati ya mkandarasi huyo na diwani.
Walizidi kulalamika kwa kusema ni rahisi sana kwa viongozi walioteuliwa na wananchi kula rushwa kuliko watendaji ambao wameajiriwa na serikali. Pia waliendelea kulalamikia barabara hiyo kuwa haikutengenezwa kwa kiwango kinachotakiwa. Watendaji hao wanalalamika wakisema wanashindwa kufanya kazi na diwani kwa kuwa wana tofauti za hitikadi za vyama kwa kusema kuwa diwani huyo ni kutoka chama cha CHADEMA lakini watendaji hao ni kutoka CCM kwa maana hiyo wanashindwa kufanya kazi kwa kushirikiana ili kuleta maendeleo katika kijiji chao na ndio sababu ameweza kusaini mikataba na mkandarasi wa barabara bila kuwashirikisha watendaji wa kijiji. Pia waliendelea kueleza kuwa wamekuwa wakizuia ukataji wa miti katika katika kata hiyo lakini diwani amekuwa akiwaruhusu wanakijiji kukata miti katika kijiji anachoishi lakini kwa vijiji vingine haviruhusiwi kukata miti. 


King Jofa akifanya mahojiano na Diwani wa kata ya Mwika Kusini Charles Kawiche.

Nilimtafuta Diwani wa kata hiyo ya Mwika kusini ili kuweza kufahamu zaidi kuhusu tuhuma dhidi yake. Nilifanikiwa kumpata na Diwani huyo na alinieleza haya “Mimi naitwa Charles Kawiche ni Diwani wa kata ya Mwika mashariki na pia ni Mwenyekiti wa kijiji cha kitongare, kero kubwa katika kata hii ni tatizo la maji, kata ya kaskazini kuna maji na nikafuatilia ili angalau tupate hata maji kwa masaa mawili kwa siku lakini imeshindikana, lakini kwenye kikao na mbunge Mh. Lyatonga Mrema lakini pia mpaka sasa hatujapata muafaka wa maji. Kwa swala la barabara tayari nimelifuatilia na kwa taarifa ya mwisho ni kwamba mkandarasi anatakiwa kuja kurudia kutengeneza barabara upya ila kwa kuwa watendaji wangu wana haraka na hawajui ni nini kinaendelea ndio maana wanalalamika na wakati hawajui lolote. Swala la ukataji wa miti kwa hapa kwenye kata ni kweli ila huwa wanakata miti wakajua mimi nimeenda kwenye vikao, ila wakijua nipo hawakati miti na tayari nimeshashika chenso mbili zilizokuwa zinakata miti na kuzipeleka ofisini. Kuhusu tofauti za hitikadi za vyama ni kweli lakini mimi nilishawaeleza kuwa mimi nafanya kazi na yeyote aliyetayari kufanya kazi bila kujali hitikadi za vyama." Hayo ndio aliyoyaeleza Diwani.

Swali la kujiuliza ni je nani mkweli kati ya Diwani na Watendaji wa kijiji???

No comments:

Post a Comment