Maandamano ya sherehe ya kilele cha maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama mkoani Singida.
Mkuu
wa wilaya yya Singida Mwalimu Queen Mlozi akikopea maandamano ya magari
kwenye sherehe za maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani
mkoa wa Singida yaliyofanyika kimkoa kwenye uwanja wa Namfua mjini
Singida. (Picha zote na Nathaniel Limu).
Na. Nathaniel Limu.
Mkoa wa Singida unakusudia kuendesha zoezi maalumu la ukaguzi wa magari na pikipiki, ili kuwabaini watu wanaong’oa alama za usalama barabarani na kuzifunga kwenye vyombo vyao.
Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi ametangaza kiama hicho kwa wahalifu hao wakati akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani kimkoa yaliyofanyika kwenye uwanja wa namfua mjini Singida.
Amesema pamoja na uzembe wa madereva, mwendo kasi, ulevi na elimu duni ya usalama barabarani, sababu nyingine ya ajali nyingi kutokea ni kutokuwepo kwa alama muhimu za usalama barabarani.
Mlozi amesema uchunguzi unaonesha wazi kuwa nyingi ya alama hizo ikiwemo viakisi mwanga hung’olewa na kufungwa kwenye magari na pikipiki za watu binafsi.
Takwimu zinaonesha kuwa katika kipindi cha Januari hadi Agosti mwaka huu jumla ya watu 83 wamekufa na wengine 192 kujeruhiwa kutokana na ajali 158 mkoani Singida.
Chanzo: Mo blog
No comments:
Post a Comment