Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, October 11, 2012

MUWASA WAWASHUSHA WAANDISHI WA HABARI NJIANI KWA KISINGIZIO CHA BAJETI...!

MAMLAKA ya Majisafi na taka Manispaa ya Musoma mkoani wa Mara (MUWASA) imewashusha waandishI wa habari njiani waliokuwa katika ziara ya Naibu waziri wa maji na umwagiliaji Dk.Eng.Binilith Mahenge  kwa madai  ya kisingizio cha ufinyo wa bajeti.

Baadhi ya Waandishi wa habari wa magezeti ya mbalimbali mkoani hapa wameshushwa katika eneo la ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Manispaa ya Musoma na  Afisa Mahusiano wa  Mamlaka hiyo Emmanuel Ruyobya  hali ambayo ni imeonekana kuwa ni udhalilishaji.

 “Kiukweli huu ni udhalilishaji kwani sisi tuna vyombo vyetu ambavyo tunavifanyia kazi na si lazima tulipwe posho sasa huyu yeye anasema bajeti finyu wakati sisi hatujaomba posho” alisema mmoja wa waandishi wa
habari walioshushwa katika gari hiyo.

Akisoma taarifa  ya Maendeleo na Changamoto zake katika ofisi ya mkuu wa mkoa kwa Naibu,Katibu Tawala wa mkoa hupo Climent Lujaji alimuagiza mkurugenzi wa MUWASA Genes Kaduri kuwaweza waandishi hao katika suala la usafiri ili waweze kushiriki katika ziara hiyo ambapo mkurugenzi huyo alimkubalia .
 
Aidha Baada ya kuondoka katika eneo la ofisi wa mkoa waandishi wa habari hao walishishwa katika gari hiyo kwa madai hayo na kwamba wameishaalika waandishi wao .

“Kama Katibu Tawala wa mkoa  ndiye kawaambia muje 
nendeni  awalipe na kuwatafutia usafiri.,alisema Afisa mahusiano  Ruyobya kwa jaziba kubwa.

Tabia ya kuwashusha waandishi wa habari  si la mara ya kwanza katika ziara mbalimbali zinazofanywa na viongozi kama hao mkoani hapa hususani katika vyombo habari  vya magazeti kubaguliwa  na hata hivi karibuni 5 Oktoba mwaka huu  imefanyika ziara ya Naibu waziri wa Nishati na Madini Stephen Masele  ambapo pia vyombo vingine vimebaguliwa.

Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji  Binilith Mahenge  ameaza ziara yake ya kujua maendeleo na changamoto zake  mkoa wa Mara  ambapo imeanzia katika halmashauri ya wilaya ya Manispaa ya Musoma,Butiama kukagua  chanzo cha maji cha Mugango –Kiabakari, Rorya,Serengeti na kumalizia wilaya ya Bunda.

No comments:

Post a Comment