Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, December 22, 2012

JOCELYNE MARO NDIO ANYAKUA TAJI LA MISS EAST AFRICA...!


 
Jocelyne Maro Miss East Africa Tanzania akipunga mkono kwa mashabiki wake mara baada ya kutangazwa mshindi katika shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam akiwashinda warembo wenzake kutoka mataifa mbalimbali ya Ukanda wa Afrika Mashariki na nchi Jirani na Ukanda huo.
Jocelyne Maro Mtanzania wa kwanza kushinda taji hilo toka lilipoanzishwa amejinyakulia zawadi zenye thamani ya dola za kimarekani 30,000 likiwemo Gari aina ya Toyota Verossa, mara baada ya majaji kumtangaza mrembo huyo ukumbi mzima ulilipuka kwa shangwe huku watu mbalimbali wakimpongeza kwa ushindi wake.

 
Miss Eats Africa Jocelyne Maro akipiga picha ya pamoja na Miss Uganda Ayisha Nagudi mshindi wa pili katika shindano hilo kushoto  na Miss Burundi Ariela Kwizera ambaye alipata nafasi ya tatu katika shindano hilo.
 
Miss Eats Africa Jocelyne Maro akipiga picha ya pamoja na  warembo wenzake alioingia nao kwenye tano bora ya shindano hilo.
 
Miss Eats Africa Jocelyne Maro akiwa amepigwa na butwaa mara baada ya kutangazwa mshindi katika shindano hilo jana usiku.
 
Miss Eats Africa Jocelyne Maro akipongezwa na wenzake mara baada ya kushinda katika shindano hilo.
 
Warembo hawa ndiyo walioingia katika tano bora ya shindano la Miss East Africa.
 
Warembo hawa ndiyo walioingia katika kumi bora ya shindano la Miss East Africa.
 
MC wa shindano la Miss East Afrca Guetano Kagwa akitangaza warembo walioingia katika kumi bora kwenye shindano hilo.
Mkurugenzi wa Rena Event Rena Calist akizungumza katika shindano hilo huku MC Guetano Kagwa akimuangalia.
 
Warembo wakipita jukwaani na vazi la ufukweni.
 
Warembo wakipita na vazi la Ubunifu.
Mkurugenzi wa Rena Event Bw. Rena Calist wa pili kutoka kulia akifuatilia kwa karibu jinsi shindano lilivyokuwa likiendeshwa kulia ni mmoja wa maofisa wa Miss East Afrca John Momadi
 
Wageni waalikwa mbalimbali wakifuatilia shindano hilo.
Mwanamuziki Mad Ice akifunika kwa wimbo wake katika shindano hilo kama anavyoonekana akishangiliwa na mashabiki wake
 
The Voice Wonder nao wakifunika mbaya.
 
Mzungu Kichaa akaleta kichaa chake jukwaani na kuwaburudisha vya kutosha watu mbalimbali waliohudhuria katika shindano hilo.

No comments:

Post a Comment