Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, January 28, 2013

HATIMAYE LULU ATAKIWA KUTIMIZA MASHARTI YA DHAMANA ILI AREJEE URAIANI...!


MAHAKAMA kuu kanda ya Dar es salaam leo imetangaza dhamana ya mwigizaji muigizaji Elizabeth maarufu kama Lulu endapo atatimiza masharti aliyopangiwa ambayo ni  kuwasilisha hati yake ya kusafiria, kutosafiri nje ya Dar es salaam, kuripoti mahakamani kila siku ya kwanza ya kila mwezi pamoja na wadhamini wake wawili ambao kila mmoja adhamini kwa shilingi milioni ishirini za kitanzania.

Upande wa familia ya Lulu wamesema masharti yote yaliyotajwa wanaweza kuyatimiza leo leo hivyo wanasubiri tu jibu la msajili ambae ndio anatakiwa kuhakikisha hayo masharti yametimia kisha ruhusa ya kumkabidhi Lulu kwa familia yake itolewe.

Taarifa za ndani ni kwamba uwezekano wa Lulu kuachiwa upo kuanzia january 29 2013 ambayo ni kesho kwa sababu kuna watumishi wawili wa serikali ambao wapo kikazi mkoani Pwani na ndio walitakiwa kutia saini dhamana ya Lulu wakiwa ni sehemu ya masharti.

No comments:

Post a Comment